Saturday, October 04, 2014

MIAKA 15 YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA BABA WA TAIFA MWL. J. K. NYERERE

Mwalimu J. K. Nyerere na aliyekuwa Rais wa Msumbiji marehemu Samora Machel.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WABUNGE KUANDAMANA NA KENYATTA ICC


Rais Uhuru Kenyatta akiwasili katika mahakama ya kimataifa ya ICC

Idadi kubwa ya wabunge nchini Kenya wanajiandaa kuandamana na Rais Uhuru Kenyatta katika mahakama ya kimataifa ya ICC,Uholanzi ambako anatarajiwa kuhudhuria kikao maalum kuhusiana na kesi inayomkabili katika mahakama hiyo.
Kenyatta ametakiwa kufika mbele ya mahakama hiyo tarehe nane mwezi huu huku kiongozi wa mashitaka Fatou Bensouda akilalamika kuwa Kenya imekataa kushirikiana na mahakama hiyo kuhusiana na ushahidi dhidi ya Kenyatta.
Mapema wiki hii, mahakama hiyo ya ICC ilitupilia mbali ombi la Rais Kenyatta, la kutaka kikao hicho cha Octoba 8 kuhairishwa au aruhusiwe kutumia video. Majaji wa Mahakama hiyo walimuagiza Uhuru kufika binafsi mbele yao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TOFAUTI YA DINI YAVUNJA NDOA INDIA

Ndoa ya kihindi
Maafisa wa polisi katikati mwa India wamefutilia mbali harusi kati ya mwanamume mkristo na mwanamke wa kihindu baada ya shinikizo kutoka kwa makundi ya kihindu yenye mrengo wa kulia.
Wanandoa hao wawili kutoka Madhya Pradesh walitoroshana na kuoana katika sherehe ya kihindu bila ruhusa ya familia ya msichana.
Baada ya makundi hayo ya Kihindu kupinga hatua hiyo na kutishia kushambulia majengo ya serikali,maafisa wa polisi katika eneo hilo waliwasaka wapenzi hao na kuwalazimisha kuachana.
Waandishi wanasema kuwa hatua hiyo ya makundi ya kihindu imekuwa ya kawaida katika jimbo hilo katika siku za hivi karibuni. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MESSI AKUTWA NA KESI YA KUKWEPA KULIPA KODI

messi
Nyota wa Barcelona Lionel Messi anakabiliwa na kesi ya kukwepa kodi,majaji nchini Hispania wamethibitisha tuhuma hizo.
Ikumbukwe Messi alikuwa akikabiliwa na tuhuma za ukwepaji kulipa kodi kwa muda sasa.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...