Thursday, December 25, 2014

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WATU WOTE KHERI YA CHRISTMAS

 Heri ya X-mass kwa wadau wote wa blog hii. Tafadhari usisahau ku-like page yetu ya facebook ya Jambo Tz.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA KICHWA CHA MUHONGO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo. 

Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umelitaka Bunge kuiwajibisha Serikali ikiwa Rais Jakaya Kikwete atashindwa kutekeleza maazimio ya Bunge ikiwamo kumng’oa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Wakizungumza hapa jana, viongozi hao walisema endapo Rais atashindwa kumwajibisha Profesa Muhongo, basi wabunge wao watawasilisha hoja na kushawishi wengine kupiga kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu na umoja huo utaitisha maandamano nchi nzima.
Mwenyekiti mwenza wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba alihoji kwa nini Rais Kikwete anasita kumwondoa Profesa Muhongo wakati Bunge lilishatoa maazimio.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UKAWA WATAKA SHERIA YA MAADILI INAYODHIBITI MAOVU

Viongozi wa Ukawa.

Viongozi wa UKAWA

VYAMA vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), vimetaka sheria ya maadili itungwe upya ili kuweka uwazi wa watu wote kuona taarifa ya mali za viongozi.

Vyama hivyo vinaamini hatua hiyo, itasaidia wananchi wote kujua mali halisi za viongozi na pia itasaidia kupunguza ufisadi, kutokana na wananchi kutambua ukweli wa mali za viongozi wao.
Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa umoja huo, Profesa Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu hatua zinazostahili kuchukuliwa, kutokana na suala la uchotwaji wa fedha katika akaunti ya Tegeta Escrow.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

VIJIJI 45 KUPATA UMEME MARA

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesema vijiji 45 mkoani Mara vinatarajiwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Alisema hayo katika ziara yake ya siku sita katika mkoa wa Mara, lengo likiwa ni kukagua na kuzindua miradi ya umeme vijijini inayosimamiwa na REA awamu ya pili kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco).
Alisema ziara yake iliyohusisha wilaya za Musoma, Tarime, Rorya, Bunda na Serengeti, ililenga kubaini na kukagua mahitaji ya umeme katika wilaya hizo ili vijiji vilivyokosa umeme kwenye awamu ya pili, viingizwe katika awamu nyingine ya umeme vijijini. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

CHENGE, NGELEJA KUADHIBIWA NDANI YA SIKU 21 ZIJAZO

Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti bungeni, Andrew Chenge


Wenyeviti watatu wa Kamati za Bunge waliopendekezwa kuwajibishwa na Bunge hilo katika sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow wataondolewa katika nyadhifa zao ndani ya siku 21 zijazo, imeelezwa.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema jana kuwa utekelezaji wa maazimio ya Bunge kwa upande wa mhimili huo wa dola utafanyiwa kazi mapema mwakani.

“Hilo litatekelezwa wakati wa Kamati za Bunge ambazo zitaanza mwishoni mwa wiki ya pili ya Januari mwakani kwa kamati husika kuchagua wenyeviti wapya.”

Wenyeviti hao ni wa Kamati ya Nishati na Madini, Victor Mwambalaswa, William Ngeleja wa Katiba, Sheria na Utawala na Andrew Chenge wa Kamati ya Bajeti. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC07568
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KESI YA MH. NASSARI YAAHIRISHWA

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari  

Kesi ya kuchoma moto bendera ya CCM inayomkabili Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari jana iliahirishwa na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Maji ya Chai, Ndikilo Mbise kutokana na Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Maji ya Chai, David Mwita kuwa safarini.
Akiahirisha kesi hiyo, Mbise alisema itatajwa tena Januari 20 mwakani.Mbise alisema Hakimu Mwita amepata msiba, hivyo amekwenda nyumbani kwao mkoani Mara huku, hakimu mwingine wa mahakama hiyo akiwa likizo.
Mbise alisema ameahirisha kesi na kuipangia tarehe nyingine kwa kuwa ni mlinzi wa amani wa eneo hio.
Katika kesi hiyo, Nassari ambaye hakuhudhuria mahakamani hapo kutokana na kuwa safarini, anatuhumiwa kuchoma bendera ya CCM Desemba 15, saa 11 jioni katika eneo la Maji ya Chai. Bendera hiyo yenye thamani ya Sh250,000 ilikuwa mali ya Raphael Moses.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa ataendelea kuwa nje kwa dhamana ya wadhamini watatu ya Sh1.5 milioni kila mmoja. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

FILAMU YENYE UTATA YAWEKWA MITANDAONI

Filamu ya the Interview iliozua utata 
 
Kampuni ya Sony Pictures imesema kuwa sinema yenye utata ya ucheshi kuhusu namna ya kumuuwa kiongozi wa Korea Kaskazini, imewekwa katika mitandao Nchini Marekani.
Kampuni hiyo inasema kuwa imechagua njia ya kusambaza sinema hiyo kupitia mitandao ya digitali, ili kuruhusu watu wengi zaidi kutizama sinema hiyo iitwayo, 'The Interview'.
Uzinduzi wa awali wa filamu hiyo ulizingirwa na utata wa mashambulizi ya kimitandao ambapo Marekani ililaumu Korea Kaskazini kwa hitilafu hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Na BBC

MAREKANI: IS HAIKUANGUSHA NDEGE YETU

 Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria 
 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.
Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Rubani wa ndege iliodaiwa kudunguliwa na wapiganaji wa IS akamatwa
Picha za IS zinamuonyesha rubani wa ndege hiyo akikamatwa. Wamemtaja rubani huyo kuwa Moaz Youssef al-Kasasbeh. Wakati huohuo Jordan imesema kuwa hasara iliyopata ya kupoteza ndege yake moja ya kivita, katika anga linalodhibitiwa na waasi wa Islamic State, haitayumbisha majeshi yake kuendelea kukabiliana na matendo ya kigaidi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MARUFUKU YA EBOLA YATOLEWA SIERRA LEONE

Maafisa wa afya wakibeba miili ya watu waliofariki kutokana na Ebola nchini Sierra leone taifa hilo limetoa marufuku ya siku tatu kazkazini mwa taifa hilo ili kukabiliana na ebola. 
 
Serikali ya Sierra Leone imetangaza siku tatu za marufuku kaskazini mwa taifa hilo, ili kuruhusu jitihada za kukabiliana na kuenea zaidi kwa ugonjwa hatari wa Ebola.
Msemaji wa serikali amesema kuwa maduka na masoko yatafungwa na hakuna magari ya abiria au pikipiki zitakubaliwa kwenye barabara za eneo hilo.
Sherehe za makanisa kuadhimisha sherehe za siku ya Krismasi pia zimepigwa marufuku.
Sierra Leone ni mojawapo ya mataifa ya Afrika magharibi ambayo yalikumbwa pakubwa na ugonjwa huo wa ebola. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MWAMBUSI AISUKA UPYA MBEYA CITY

Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
 
Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi amesema tatizo kubwa kwa sasa katika kikosi chake ni safu ya ushambuliaji ambayo ameendelea kuisuka ili wafanye vyema Ligi Kuu Bara itakapoendelea.

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwambusi alisema vijana wake wapo ‘fiti’ na wana ari mpya ya kurudisha heshima yao kwa mashabiki wao huku akisema kuteleza siyo kuanguka, kwani yalitokea hivi karibuni ndani ya klabu hiyo yamepita na sasa wanakuja kivingine.

“Ukiangalia mechi zilizopita tulipata mabao mawili tu, na raha ya mpira wa sasa ni kufunga mabao mengi, hivyo nimeona ushambuliaji ni tatizo kubwa, lakini tunaendelea na maboresho katika safu hii,” alisema Mwambusi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAXIMO "MKAKATI WANGU UMENIONDOA YANGA"




Kocha Marcio Maximo 


Kocha Marcio Maximo amesema hana kinyongo na uamuzi wa uongozi wa Yanga kumuondoa, ingawa umefuta ghafla mkakati wa kutaka klabu hiyo iendeshwa kwa weledi.

Maximo na msaidizi wake Leonard Neiva walisitishiwa mikataba yao baada ya Yanga kufungwa na Simba 2-0 katika mchezo wa Nani Mtani Jembe mwezi huu, ikiwa ni takriban miezi mitano tangu aje nchini.

Akizungumza muda mfupi kabla ya kupanda ndege kurudi kwao Brazil jana, Maximo alisema hana kinyongo na uamuzi huo, lakini akaitaka klabu hiyo kongwe kuendeleza soka la vijana na kutengeneza mindombinu kama inataka kupata mafanikio makubwa katika soka.

Alisema katika muda mfupi aliokuwa klabu hiyo, alijenga misingi ya utendaji kazi wa kisasa ndani na nje ya uwanja kwa wachezaji ili waweze kujitambua katika kazi yao, lakini jambo hilo limeishia njiani. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PLUIJM NA PHIRI WAJIGAMBA

Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm




Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm na mwenzake Patrick Phiri wa Simba wametamba kuibuka na ushindi dhidi ya Azam na Kagera Sugar wakati mechi za Ligi Kuu ya Vodacom zitakapoingia raundi ya nane kuanzia kesho.

Pluijm alisema kuwa anaiheshimu Azam FC kama moja ya timu bora kwenye ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, lakini hana hofu yoyote.

“Nawaandaa vyema vijana wangu waibuke na ushindi kwenye pambalo hilo kwa sababu litatuweka kwenye nafasi nzuri nje na ndani ya uwanja,” alisema Pluij
m. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...