Thursday, December 25, 2014

MAREKANI: IS HAIKUANGUSHA NDEGE YETU

 Wapiganaji wa IS wakibeba mabaki ya ndege waliodai kuidungua huko Syria 
 
Wapiganaji wa kundi la Islamic State wamesema kuwa waliidungua ndege ya jeshi la muungano ,lakini Marekani inasema kuwa ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hilo si kweli.
Jordan ni miongoni mwa mataifa manne ya kiarabu yaliopo katika muungano wa majeshi yanayoungwa mkono na Marekani ambayo yameanzisha mashambulizi dhidi ya wanamgambo wa IS.
Ndege hiyo aina ya F-16 ni ndege ya kwanza ya jeshi hilo la muungano kupotea katika maeneo yanayodhibitiwa na IS tangu mashambulizi yaanze mnamo mwezi Septemba.
Rubani wa ndege iliodaiwa kudunguliwa na wapiganaji wa IS akamatwa
Picha za IS zinamuonyesha rubani wa ndege hiyo akikamatwa. Wamemtaja rubani huyo kuwa Moaz Youssef al-Kasasbeh. Wakati huohuo Jordan imesema kuwa hasara iliyopata ya kupoteza ndege yake moja ya kivita, katika anga linalodhibitiwa na waasi wa Islamic State, haitayumbisha majeshi yake kuendelea kukabiliana na matendo ya kigaidi.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...