Tuesday, May 07, 2013

SALAMA JABIR "AKINYONYWA ULIMI" NA NJEMBA HADHARANI......!!



Mambo  vipi jamani....

Katika  pitapita   zangu nimefanikiwa  kumnasa  live  Salama Jabir  akinyonyana  ndimi  bila  chenga  na  mwenzake...!!

Nashindwa  kuthibitisha  huyo  wa  pili  ni  nani  na  ni  jinsia  gani....nikimwangalia  haraka  haraka  naona  kama  ni  mwanaume  na  namfananisha  na  mdogo  wake    Wema   Sepetu  aitwaye  Bill Sepetu.....

Nikijaribu  kukaza  macho  kwa  kwa  makini,  huyo  wa  pili  namuona  kama  ni  mwanamke  kutokana  na vazi  lake.Hicho  cha  mabegani  nakifananisha   na  sidiria  za  akina  dada....!!

Yaani  nimeumiza  macho  mpaka  yanauma...Nashindwa  kuyaamini  macho  yangu  kuhusu  Salama Jabir. Sikutegemea..!!
Chanzo Gumzo la Jiji

KIKOSI CHA MIZINGA WAFUNIKA DAR CHID BENZI ADUNDWA NA PINA

 Mc mwenye VVU 
Nash Mc


 alifanya poa Usiku wa kikosi na mizinga 21


 Kala Pina



FBI WAFIKA ARUSHA KUCHUNGUZA TUKIO LA KIGAIDI LA KANISA KUPIGWA BOMU



MAJASUSI wa shirikisho la ujasusi la nchini Marekani wamefika jijini Arusha kusaidiana na wapelelezi wa nchini Tanzania katika uchunguzi wa tukio la kushambuliwa kwa bomu kwa waumini wa kanisa katoliki na Balozi wa Vatican nchini siku ya jumapili.
Magesa alitoa taarifa hiyo wakati akitoa taarifa ya Mkoa kwa waziri Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda alipozuru eneo la tukio na kuwatembelea wagonjwa waliolazwa katika hospitali mbalimbali na kuwapa pole.

Wakati maafisa hao wakifika jijini humo tayari vyombo vya usalama vinawashikilia watu zaidi ya 10 miongoni mwao wakiwemo watu wanne kutoka Saudia Arabia ambao waliwasili nchini kupitia uwanja wa ndege wa Kilimanjaro(KIA) siku moja kabla ya tukio.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo alisema kuwa watu hao walikamatwa muda mfupi wakiondokanchini kupitia mpaka wa Namanga kuelekea nchini Kenya baada ya tukio kutokea.
Hata hivyo taarifa hiyo haikuweza kutoa ufafanuzi zaidi na kwamba taarifa zaidi juu ya upepelezi zitatolewa kadri muda na wakati utakavyoruhusu.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 7, 2013

DSC 0007 83e8a

DSC 0006 a102d

FAHAMU KUHUSU DIAMOND PLATNUM KUBORONGA HUKO LONDON...... ADAM NDITI ANAYECHEZEA CHELSEA AMBWATUKA


Mtanzania ambaye kwa sasa ni raia wa Uingereza na anayechezea klabu ya Chelsea, Adam Nditi ameiponda show ya Diamond mjini Reading nchini humo na kudai ilikuwa ni aibu tupu.

adam na diamond 
“Diamond jana manyago aibu tupu waswahili lazima tubadilike it’s embarrassing,” ametweet.
  
“Hajafanya jambo lolote ila shoo ilikuwa very unprofessional kwenye tangazo walisema inaanza saa 3 usiku jamaa amefika saa 1 asubuhi.”
 
“Jukwaa lilikuwa ovyo kama vile watu hawajalipa kumuuona mmoja Wa wasani wanaotamba bongo nyimbo zilikuwa zinapigwa redioni alikuwa haimbi.”

Kwa sasa Diamond yupo ziarani nchini Uingereza.

Rais Jakaya Kikwete Afanya mabadiliko ya uongozi kwenye halmashauri za majiji manne kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji na Kuwateua na kuwapandisha vyeo wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa wawili kuwa wakurugenzi wa majiji



Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi), Hawa Ghasia

--
Rais Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya uongozi kwenye halmashauri za majiji manne kwa lengo la kuongeza ufanisi wa utendaji.

Aidha amewateua na kuwapandisha vyeo wakurugenzi wa mamlaka za serikali za mitaa wawili kuwawakurugenzi wa majiji.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini Dodoma, Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, (Tamisemi), Hawa Ghasia, alisema mabadiliko ya uongozi yamefanyika katika halmashauri za majiji yaArusha, Mwanza, Dar-es- Salaam na Mbeya.

Alisema wakurugenzi walioteuliwa na kuhamishwa ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa yaTabora, Sipora Liana kuwa Mkurugezni wa Jiji la Arusha na Mkurugenzi wa mji wa Njombe, Hassan Hida kuwa Mkurugenzi wa jiji la Mwanza.

Ghasia alisema wakurugenzi waliohamishwa ni wa Jiji la Dar es Salaam, Musa Zungiza kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Mbeya na Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza. Wilson Kabwe, kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es salaam.

KAULI YA BUNGE KUHUSU MLIPUKO WA BOMU HUKO ARUSHA

KAULI YA SERIKALI BUNGENI KUHUSU MLIPUKO ULIOTOKEA KATIKA KANISA KATOLIKI LA YOSEFU MFANYAKAZI PAROKIA TEULE YA OLASITI, ARUSHA MJINI, TAREHE 5 MEI, 2013.


Mheshimiwa Spika,

kwa mujibu wa Kanuni ya 49 (1) ya Kanuni zaKudumu za Bunge, Toleo la Aprili, 2013, naomba kuwasilisha Taarifa yaawali kuhusu tukio la mlipuko uliotokea katika Kanisa Katoliki la MtakatifuJoseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasiti, Jijini Arusha tarehe 5 Mei, 2013 saa4:30 asubuhi.

Mheshimiwa Spika,
mnamo tarehe 5 Mei, 2013 saa 4:30 asubuhikulitokea mlipuko katika kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi,Parokia ya Olasiti, jijini Arusha. Mlipuko huo ulitokea muda mfupi baada yakuanza kwa ibada ya uzinduzi wa Parokia. Mgeni Rasmi katika uzinduzialikuwa ni Balozi wa Vatican nchini na Mjumbe wa Baba Mtakatifu, AskofuFransisco Mantecillo Padilla. Aidha, alikuwapo mwenyeji wake AskofuJosephati Lebulu wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha. Katika uzinduzi huoinakadiriwa kuwa kulikuwa na zaidi ya watu 2000. Wakati Mgeni Rasmiakiwa ametoka nje ya Kanisa akijiandaa kukata utepe kama ishara yauzinduzi mtu alirusha kitu chenye ukubwa wa ngumi kuelekea eneo kulipokuwa na mkusanyiko wa watu ambapo baada ya kutua kulitokeakishindo na mlipuko mkubwa. Mlipuko huo ulisababisha taharuki miongonimwa waumini na kusababisha watu kukimbia ovyo.

BARAZA KUU LA WAISLAMU LALAANI VIKALI MLIPUKO WA BOMU NDANI YA KANISA KATOLIKI

TAMKO LA BARAZA KUU LA WAISLAMU WA TANZANIA BAKWATA JUU YA MLIPUKO WA BOMU - ARUSHA

Assalaam alaykum warahmatullahi wabarakaatuh.

Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA, limepokea kwa masikitiko makubwa tukio la kurushwa bomu Kanisani na kusababisha upotevu wa maisha na majeraha kwa watu wengi wakati wa sherehe ya uzinduzi wa jengo la Kanisa la Parokia ya Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Orasiti, Arusha.


Kimsingi hili ni jambo la kusikitisha, kukera na kufadhaisha sana kutokea hapa nchini. 
Watanzania kwa miaka mingi, tumezoea hali ya utulivu na amani na tukio kama hili ni changamoto kwa usalama wa Watanzania wote nchi nzima Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania BAKWATA linalaani kitendo hicho cha kikatili na inaviomba vyombo vya dola kufanya jitihada zote kuhakikisha wahusika wanakamatwa na wanachukuliwa hatua, kwani msiba huu ni wetu sote, Wakristo na Watanzania wote.

Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania mimi Sheikh Issa Bin Shaaban Simba Mufti wa Tanzania nawapa pole wafiwa wote katika tukio hilo na kuwaombea dua majeruhi na Mwenyezi Mungu (SW) awape tahfif na wapone haraka na kurudi katika shughuli zao za kila siku.

Wabillahi Tawfiiq.

SHEIKH ISSA BIN SHAABAN SIMBA.
MUFTI NA SHEIKH MKUU WA TANZANIA BARA.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...