Sunday, June 18, 2017

OLE SENDEKA AWAKUBALI WAPINZANI MSIBANI KWA MAMA YAKE

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amesema tofauti za itikadi za kisiasa zisitumike kuwagawa Watanzania, bali ziwe chachu ya kufanikisha maendeleo.

Ole Sendeka aliyasema hayo jana, wakati wa kuaga mwili wa mama yake Raheli Sendeka kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Engarenarok jijini Arusha.

Alisema baada ya kutokea kwa msiba huo, viongozi wa kwanza kufika nyumbani kwake kumpa pole walikuwa mbunge na diwani wa Chadema, hivyo amepata somo kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuondoa umoja na upendo wa Watanzania. Alisema mbunge wa kwanza kufika nyumbani kwake Ngarenaro jijini hapa ni wa Siha mkoani Kilimanjaro (Chadema), Dk Godson Mollel na diwani wa Ngarenaro (Chadema), Issaya Doita.

MAJERUHI WA LUCKY VINCENT KUREJEA NCHINI MWEZI WA NANE

Watoto watatu walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea nchini baada ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Pia, Nyalandu ameandika katika mtandao huo kuwa watoto hao; Doreen Mshanga, Saidia Ismael na Wilson Tarimo wanategemewa kutembea tena.

Hata hivyo, kwa sasa Doreen, atahamishiwa katika kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya uti wa mgongo cha Madonna katika mji wa Lincoln, Nebraska.

“Katika watoto wote hao watatu, Doreen ni muujiza mkubwa zaidi,” amesema Nyalandu.

UTHAMINI MOYO WAKO, KAA MBALI NA MAUMIVU

HAKUNA ubishi kuwa mapenzi yanachukua nafasi kubwa sana katika maisha ya binadamu, ipo dhahiri kwamba mapenzi yanaweza kuleta furaha maishani mwako lakini wakati huohuo  maumivu, mateso na karaha.

Watu wengi bado wanalizwa na mapenzi na hii ni kwa sababu hawafuati kanuni sahihi za mapenzi. Ndiyo… mapenzi yana kanuni zake.

Kwa bahati mbaya kabisa, kwa sasa mapenzi yamegeuzwa na kuwa kama kitu cha kujaribu au kufanyia biashara ndiyo maana yanawatesa wengi.

Lakini ni kwa nini mapenzi yaendelee kututesa?  Au ni kwa sababu hatujui maana halisi ya mapenzi? Hebu tuyaangalie mapenzi kwa jicho la tatu, kisha tuchukue hatua.

MAPENZI NI NINI?
Katika hali ya kawaida, mapenzi hayaelezeki kuwa ni nini. Ni vigumu sana mtu kukueleza maana ya mapenzi ndiyo maana kila mtu ana uelewa tofauti juu ya suala hilo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...