Monday, November 11, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBER 11, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS

.
.

,
,

VAN PERSIE AIZAMISHA ARSENAL, MAN UNITED WAFUFUA MATUMAINI YA UBINGWA

article-2497133-1954DA9800000578-907_634x446_f36bf.jpg
MHOLANZI Robin van Persie amezamisha klabu yake ya zamani, Arsenal akiifungia bao pekee la ushindi Manchester United na kuirejeshea matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England.
Van Persie alifunga bao tamu kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa kitaalamu na Wayne Rooney dakika ya 27 Uwanja wa Old Trafford.
Kikosi cha United kilikuwa; De Gea, Smalling, Vidic/Cleverley dk45, Evans, Evra, Valencia, Jones, Carrick, Kagawa/Giggs dk78, Rooney na Van Persie/Fellaini dk85.
Arsenal; Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta/Gnabry dk82, Flamini/Wilshere dk61, Ramsey, Ozil, Cazorla/Bendtner dk78 na Giroud.

TAARIFA RASMI YA ZITTO KABWE KUHUSU KINACHOITWA “TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA”

Zitto-Kabwe_c2a4f.jpg
Tamko rasmi la Ndugu Zitto Z. KABWE (MB) kuhusiana na kinachoitwa "Taarifa ya Siri ya CHADEMA"
Ndugu Wanahabari,
NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
"Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu
mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.

KENYA YAIUNGA MKONO TZ A.MASHARIKI

131110120158_amina_mohamed_304x171_bbc_nocredit_860b3.jpg
Amina Mohamed,waziri wa mambo ya nje wa Kenya
Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutoka Jumuia ya Afrika Mashariki kuipongeza Tanzania kwa hatua yake ya kutangaza bayana kwamba haiko tayari kutoka katika jumuiya hiyo kama ilivyodhaniwa.
Wasiwasi kuwa Tanzania ingejitoa kutoka jumuia ya Afrika Mashariki ulitokana na hali iliyojitokeza kwa baadhi ya nchi za jumuia hiyo kuendesha mikutano yao bila kuishirikisha Tanzania na Burundi.
Baadhi ya wanasiasa na wananchi nchini Tanzania walitaka nchi yao iachane na jumuia hiyo wakizishutumu Kenya, Rwanda na Uganda kuitenga Tanzania hata katika mikutano ya masuala yaliyohitaji maamuzi ya jumuia.
Kufuatia mfarakano huo, ulionekana kutishia uhai wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, wiki hii alilihutubia bunge la Muungano wa Tanzania mjini Dodoma, katikati ya nchi na kutangaza bayana kuwa Tanzania haitatoka katika jumuiya ya Afrika Mashariki, kwani imefanya kazi kubwa kuifufua na kuiunda upya baada ya kusambaratika mwaka 1977.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...