Saturday, July 20, 2013

SIKILIZA WIMBO WA MZEE MAGARI...!!!


Daaaah! Mzee Magari kweli kipaji kipo hebu chukua dakika chache kusikiliza wimbo huu afu dondosha comment yako.

AJALI MBAYA: KICHWA CHA MWANAMKE CHANASA KWENYE KIOO...!!!


Wakimtoa Dereva kwanza
Wakianza kumuokoa yeye
Hatimaye ameokolewa
Mwanamke mmoja raia wa China amenusurika kifo baada ya gari aliliokuwa amepanda kupata ajali mbaya iliyomsababishia yeye kunasa kakita kioo cha Mbele maeneo ya Jimbo la Guanxi, Mwanamke huyo ambaye jina lake halikuweza kufahamika alikuwa kashapoteza fahamu huku damu nyingi zikimtoka katika kioo hicho.

Juhudi za ziada zilifanywa na askari wa kikosi cha zimamoto na uokoaji kwa kukitanua kioo hicho kwa ustaadi mkubwa huku wakihakikisha hawamkati zaidi mwanamke huyo.

KIKOSI CHA WAASI NCHINI KONGO M23 CHAWEKA PICHA YA PASSPORT YA ASKARI WA JWTZ WALIYEMKAMATA ASUBUHI YA LEO AKISHIRIKIANA NA FDLR

m23-tanzania-twitterchristopher-george-yohana 

Waasi wa M23 wa DR Congo, wanadai kuwa wamemkamata askari wa Tanzania anayeitwa Christopher George Yohana, wakati akishirikiana na waasi wa Rwanda (FDLR) wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya maelfu ya Watusi mwaka 1994.

Waasi hao wa M23 wameweka picha ya passport ya mateka huyo kwenye mitandao ya kijamii ya Facebook na Twitter. Kwa mujibu wa chimpreports.com,   M23 wameripoti kumkamata askari huyo akiwa na bunduki aina ya AK47 yenye serial number 1372. Ifuatayo ni kauli ya M23 waliyoweka Facebook ikiambatana na picha hiyo ya Passport Juu hapo:
“Leo Fdlr zikiongozwa na askari toka Tanzania zilivamiya Positions zetu pale Kinyadonyi Na Nkwenda huko Rutshuru. Zilikuta Vijana wanazisubiri, walizicapa na kuzikimbiza alafu zikaaca Askari wa Tanzania Nyuma tukamunasa, ivi tuko naye tuko na mupa cayi na mukate anywe. Serikali ya tanzania isiwe na hofu hatutamufanya kitu, tutamucunga muzuri. sisi hatuko kama wale wa criminals wa FARDC ambao wanatukanaka hata maiti, na wenye Wanabakaka watoto wa myaka sita, sisi ni jeshi la Mungu. Kesho mutaona Video yake, Cliquer apa uone passport ya ule askari ya tanzania ambaye tulikamata”

WASTARA JUMA .... "WANAUME WALIO MSAIDIA SAJUKI WAMENIGEUKIA NA KUNITAKA KIMAPENZI"


Wastara Juma amefunguka kuwa wanaume wengi waliokuwa wakimsaidia wakati mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ akiwa mgonjwa wanamgeuka na sasa wanamtaka kimapenzi.
Akizungumza kupitia Kipindi cha Take-One katika Runinga ya Clouds chini ya Zamaradi Mketema, Wastara alisema baadhi ya watu ambao walikuwa karibu naye wakati Sajuki anaumwa sasa hivi wamegeuka na kumtaka kimapenzi, jambo ambalo linamuumiza na kumshangaza mno.

Bishosti huyo alisema kuwa tofauti na wanaume hao ambao walikuwa wakimpa sapoti kipindi hicho, bado wapo wengine kibao kutoka nje na ndani ya nchi ambao wanatuma maombi kwake lakini anawaona wote ni matapeli na wanamtamani tu hivyo hayupo tayari kuingia kwenye uhusiano wa aina hiyo.

ANGALIA PICHA ZAIDI ZA MAPOKEZI YA MIILI YA MASHUJAA WA TANZANIA WALIOUAWA DARFUR ILIVYOPOKELEWA LEO JIJINI DAR




 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiwaongoza wananchi na viongozi wengine kupokea Miili ya Askari wa Jeshi la kulinda amani, waliopoteza maisha katika Jimbo la Darfur, wakati miili hiyo ilipokuwa ikiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo jioni.




 MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, leo jioni amewaongoza watanzania kupokea Miili ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan kutokana na shambulizi la ghafla. 



Miili hiyo imewasili kwa ndege maalum katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere – Terminal one (Air Wing) leo jioni majira ya saa kumi.

"HAKUNA UCHAGUZI WA MEYA ARUSHA" NAPE NNAUYE

Nape Nnauye
MKURUGENZI WA Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Nape Nnauye amesema suala la uchaguzi wa Meya wa Mji wa Arusha limefikia tamati na kamwe uchaguzi huo hautafanyika tena. Nnauye alisema hayo alipozungumza na MTANZANIA jana, huku akiwataka wananchi wa Jiji la Arusha kupuuza kauli za vitisho zinazotishia kumwondoa madarakani Meya wa Jiji, Gaudence Lyimo.
Kauli ya Nnauye inafuatia kauli iliyotolewa na Mwenyekiti wa Madiwani wa Chadema Arusha Isaya Doita, aliyesema kuwa ushindi wa udiwani wa chama chao katika kata nne za mji huo ni chachu katika msimamo wa chama chao kutaka uchaguzi wa Meya wa Arusha urudiwe.

Doita akiamini kuwa Lyimo alichaguliwa kwa mizengwe, alisema ana imani muda si mrefu Jiji la Arusha litapata meya ambaye amechaguliwa kwa misingi ya sheria.

Hata hivyo, siku chache baadaye Katibu wa Chadema wa Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa alisema suala la nafasi ya umeya siyo tena ajenda ya chama hicho.

Akizungumzia suala hilo jana, Nnauye alisema CCM imezoea kusikia kauli mbalimbali za vitisho zinazotolewa Chadema na kuwataka wananchi wa Arusha kuzipuuza kauli hizo.

“Ni kazi yao vitisho nia yao ni kutaka watu wasifanye shughuli zao, lakini suala la meya yupo pale na ataendelea kuwapo kwani uchaguzi ulishafanyika na hautafanyika tena.

“Kazi iliyobaki sasa kwa wananchi wa Arusha ni kujenga mji wao kwa kufanya kazi, watu wafanye kazi zao wala hakuna sababu ya kuhofia kauli za vitisho.

“Ni upuuzi kuanza kuzungumzia kila siku suala la Arusha, waliopewa dhamana wawajibike kilichobaki ni kufanya kazi, waache kusikiliza upuuzi,” alisema Nnauye.

CHANZO MTANZANIA

KOCHA MZUNGU TAIFA STARS AFARIKI DUNIA JANA

Bert Trautmann

 
Tumempoteza: Kocha wa zamani wa Taifa Stars, Bert Trautmann amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89 jana.


Na Mahmoud Zubeiry na Chris Wheeler,
KOCHA wa zamani wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na giwji wa zamani wa klabu ya Manchester City, Mjerumani Bert Trautmann amefariki dunia leo akiwa na umri wa miaka 89.
Baada ya BIN ZUBEIRY kusoma taarifa za kifo cha kocha huyo Daily Mail, ilimpigia Nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Leodegar Chilla Tenga ambaye alifundishwa na Mjerumani huyo na akasikitisha.
Tenga, ambaye sasa ni Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), alisema kwamba Trautmann, ambaye alikuwa anasumbuliwa alikuwa mwalimu mzuri na wachezaji walimpenda sana.
Alisema kocha huyo aliyefariki asubuhi ya leo nyumbani kwake, La Losa, karibu na Valencia aliifundisha Taifa Stars kati ya mwaka 1975 na 1976.
“Alikuwa kocha mzuri, kwa sababu ni kocha aliyetokea kuwa mchezaji wa kulipwa, alikuwa anaelewa saikolojia ya wachezaji, na alikuwa mwalimu ambaye ukienda kambini unaona raha kuwa kambini.

MAAJABU:MBUZI AZALIWA NA VICHWA VIWILI TENA KWA MAUMIVU MAKALI

Kuanzia Saa 10 Alfajiri zilisikika kelele za Maumivu kutoka kwa mbuzi jike ambaye alikuwa anajifungua, Kelele zilikuwa kubwa mno kuashiria maumivu makali alikuwa anayapata kiumbe huyo, palipozidi kupambazuka ilibidi majirani waende kushuhudia kulikoni kwa mbuzi kuwa na kelele kiasi kile, na ndipo walipojionea maajabu baada ya mbuzi jike huyo kujifungua watoto watatu, wawili kati ya hao wakiwa ni wa kawaida kabisa na mmoja akiwa na vichwa viwili.

Hayo ndio yaliyojiri Alhamisi ya jana tarehe 18 July 2013 Huku katika Jimbo la Irolini Kwara, Nigeria. Hata hivyo mbuzi huyo alizaliwa na vichwa viwili alifariki saa chache baadae

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...