Thursday, January 01, 2015

JAMBO TZ TUNAWATAKIA KHERI YA MWAKA MPYA 2015


 Asante kwa kutembelea Blog na pia ku-like page yetu ya facebook, endelea kuwa nasi siku zote ili upate habari nzuri na za uhakika kutoka kila kona ya dunia wakati wowote kila siku.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

RAIS KIKWETE ATOA SALAMU ZA MWISHO ZA MWAKA AKIWA MADARAKANI

Rais Kikwete 

Mwaka wa uchaguzi umeingia. Usiku wa kuamkia leo, Watanzania wameupokea mwaka mpya 2015 huku tafakari kubwa ikiwa ni matukio makubwa yatakayotokea mwaka huu, ukiwamo Uchaguzi Mkuu na kura ya maoni ya Katiba Inayopendekezwa.
Mbali na uchaguzi wa rais wa awamu ya tano, wananchi wataamua ama kuipitisha au kuikataa Katiba Inayopendekezwa, mambo ambayo wasomi, wanasiasa na wanaharakati wameonya kuwa yanatakiwa kuendeshwa na kusimamiwa kwa weledi na umakini mkubwa.
Vilevile, kutokana na matukio hayo kugharimu fedha nyingi, wataalamu wa uchumi wanatabiri kuwa mwaka huu utakuwa mgumu na itakaowalazimu Watanzania kufunga mikanda zaidi.
Pia, macho na masikio ya wananchi yako kwa vyama vya upinzani ambavyo vimeungana na kuzaa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kuona kama vitasimamisha mgombea mmoja wa urais na katika nafasi za ubunge na udiwani kama vilivyokubaliana, ikiwa ni mara ya kwanza tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MUUMINI MBARONI KWA KUFANYA FUJO KANISANI

Leonard Paul
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo
POLISI mkoani Morogoro linamshikilia Jackson Mnyilemi (20), ambaye ni muumini wa Kanisa la Moravian Tarafa ya Malinyi wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro kwa tuhuma za kuhusika kufanya fujo kanisani.
Fujo hizo zilisababisha kujeruhiwa kwa waumini wawili kwa kukatwa sehemu za usoni na mikononi na kitu chenye ncha kali.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema jana kuwa tukio hilo ni la Desemba 28, 2014 majira ya saa 10 : 40 asubuhi katika kijiji cha Makelele na kuwataja waumini waliojeruhiwa kuwa ni Maria Silumbwe (47) na Aron Silumbwe (20), wote wakazi wa Kijiji hicho kilichopo Tarafa ya Malinyi wilayani Ulanga. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWAKYEMBE AFUKUZA KAZI VIGOGO 6 WA RELI

Dk Harison Mwakyembe.
 Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe ameagiza wafanyakazi sita wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), wafukuzwe kazi na polisi wawakamate na kuwalaza rumande kuanzia jana kutokana na tuhuma za wizi.
Pia, ameagiza mali za watuhumiwa hao, zichunguzwe na ikibainika ni zaidi ya kipato chao cha kawaida, zipigwe mnada na Bodi ya Wakurugenzi ikae na kuangalia hatua zaidi za kuchukua.
Dk Mwakyembe alitoa maamuzi hayo jana baada ya kuzungumza na wafanyakazi wa TRL na kuonekana kutoridhishwa na vitendo vya wizi, vinavyoendelea katika shirika hilo.
Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Stanley Makunja, Stanley Andrew, Edward Benedicto, Lucy Mtinya, B. Ruoga na Jackson Moses.
Hata hivyo, Mwakyembe alipoombwa na waandishi wa habari, kufafanua vituo vya kazi vya watuhumiwa hao, alidai kwamba wote ni wa TRL na wamewajibishwa kama wafanyakazi wa TRL. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO SIKU YA KWANZA YA MWAKA 2015

.
.
.

Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ZITTO: NITAMUUNGA MKONO MBOWE


HAKI SAWA: Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba (kulia) na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Zitto Kabwe wakiwasili kwenye Uwanja wa Mashujaa mjini Mtwara jana, ambako walihutubia mkutano wa hadhara.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Zitto Kabwe amesema atamuunga mkono Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani, Freeman Mbowe pale atakapowasilisha hoja yake bungeni kuhusu ufisadi wa zaidi ya Sh1 trilioni katika mradi wa bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar es Salaam.
Zitto aliyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashujaa mkoani hapa uliandaliwa na Chama cha Wananchi (CUF) kuwashukuru wakazi wa mkoa huo kwa kuwachagua viongozi wa chama hicho katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
“Najua bado mnalia kuhusu bomba la kupeleka gesi Dar es Salaam, machozi yenu yatafutika kwani tayari habari za ufisadi mkubwa katika ujenzi wa bomba hili zimeanza kuchomoza. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATU 20 WAFARIKI HARUSINI

Mmoja ya watoto waliojeruhiwa wakati bomu liliporushwa katika nyumba moja iliokuwa ikifanya sherehe ya harusi mkoani Helmand nchini Afghanistan.Takriban watu 20 waliaga dunia 
 
Sherehe moja ya harusi nchini Afghanistan, imeshambuliwa kwa mzinga uliorushwa na roketi na kusababisha mauaji ya watu 20 na kuwajeruhi wengine zaidi ya kumi na mbili.
Kisa hicho kilitokea wakati wa makabiliano makali kati ya walinda usalama wa Afghanistan na wapiganaji wa Taliban katika jimbo la Helmand.
Mmiliki wa jumba lilofanyiwa harusi hiyo amesema kuwa wageni walikuwa wanajikusanya nje kumkaribisha bi harusi,na kuongezea kuwa watoto wake tisa wametoweka.
Waliojeruhiwa walipelekwa katika hospitali ya Lashkar Gah,mji mkuu wa mkoa huo.
Shambulio hilo limetokea wakati wa siku ya mwisho kwa ujumbe wa wanajeshi wa Marekani na wale wa shirika la kujihami la NATO wanaoondoka nchini Afghanistan. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

PAPA AKEMEA UFISADI MWAKA MPYA

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis 
 
Papa Francis ametumia sherehe za kuupokea mwaka wa 2015 kuzungumzia tatizo la rushwa katika mji wa nyumbani wa Rome nchini Italia.
Akizungumza katika Kanisa kuu la St. Peter Basilica, papa amesema rushwa ni shumbulizi dhidi ya maskini na wasiokuwa na uwezo ambapo ametaka mabadiliko ya kiroho na kimaadili katika mji huo.
Papa ambaye ndiye Askofu wa Rome amefanya utetezi dhidi ya maskini kama nguzo muhimu katika uongozi wake wa upapa.
Maafisa wa polisi kwa sasa wanawachunguza maafisa wa Roma wanaotuhumiwa kujihusisha na kundi la Mafia na ufisadi dhidi ya fedha za umma zikiwemo zilizotengwa kwa ajili ya kituo wahamiaji. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWAKA MPYA MAAAFA CHINA WATU 35 WAFARIKI

Umati wa watu waliokanyagana na wengine kufa nchini China wakati wakiupokea mwaka mpya 2015 
 
Sherehe za kuupokea mwaka mpya 2015 zimeguka kuwa majonzi baada ya watu thelathini na watano kufa kwenye taharuki ya kukanyagana kwenye msongamano wakati wakiiupokea mwaka mpya.
Maafa hayo yametokea katika mji Shanghai ambapo maelfu ya watu walikuwa wamekusanyika ili kuupokea mwaka mpya.
Chanzo cha taharuki hiyo bado haijafamika lakini vyombo vya habari vya nchi hiyo vimenukuliwa vikisema imetokana na maelfu ya watu kuzuiwa kugombea fedha bandia zilizotupwa eneo hilo kutoka katika jengo moja. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KANO WAPOKEA MWAKA MPYA MARA YA KWANZA

 
Mwaka mpya 2015 ulivyopokelewa Hong Kong
 
Mwaka mpya wa 2015 umepokewa kwa kishindo katika maeneo mbali mbali duniani na barani Afrika.
Nchini Nigeria kumekuwa shamra shamra ambapo kwa mara ya kwanza mafataki yalirushwa katika eneo la kaskazini mwa nchi hiyo lenye waislamu wengi.
Shamra shamra hizo zimefanyika katika kituo cha michezo katika mji wa Kano ambapo waliohudhuria ni wale waliopata mwaliko pekee.
Habari zinasema kumekuwa na mwitikio mkubwa ambapo umati wa watu ulihudhuria shamra shamra hizo jambo lililowapa wakati mgumu maafisa usalama kuudhibiti umati huo.
Waandaji wa shamra shamra hizo za maonyesho ya kulipua mafataki hayo wanasema wanataka jimbo la Kano kuungana na miji mingine mikubwa duniani kusherehekea siku kuu ya Mwaka Mpya.
Ulinzi mkali uliimarishwa kwa tahadhari ya shambulio lolote kutoka kundi la wapiganaji wa kiislamu la Boko Haram.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Na BBC

RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND LEO, MAN U, ARSENAL, CHELSEA MZIGONI

Chelsea+v+Manchester+United+Premier+League+SSB1R4Q96Y8l
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
EnglandPremier League
15:45 Stoke City ? – ? Manchester United
18:00 Aston Villa ? – ? Crystal Palace
18:00 Hull City ? – ? Everton
18:00 Liverpool ? – ? Leicester City
18:00 Manchester City ? – ? Sunderland
18:00 Newcastle United ? – ? Burnley
18:00 Queens Park Rangers ? – ? Swansea City
18:00 Southampton ? – ? Arsenal
18:00 West Ham United ? – ? West Bromwich Albion
20:30 Tottenham Hotspur ? – ? Chelsea 

KOMBE LA MAPINDUZI KUANZA KUTIMUA VUMBI LEO

MICHUANO ya Kombe la Mapinduzi inaanza kutimua vumbi leo Visiwani Zanzibar ambapo Simba itacheza na Mtibwa Sugar, na mabingwa watetezi, Azam watacheza na KCCA ya Uganda Ijumaa kwenye Uwanja wa Amaan.
Mashindano hayo ni maalumu kwa ajili ya kuadhimisha siku ya Mapinduzi ya Zanzibar yanashirikisha timu mbalimbali kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambazo ni KCCA, Sports Club Villa zote kutoka Uganda, El Merreikh ya Sudan, Ulinzi ya Kenya, Azam, Simba na Yanga zote kutoka Tanzania Bara na Shaba, JKU, Mtendeni, Mafunzo na KMKM kutoka Zanzibar.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa waandaaji wa mashindano hayo ambao ni Chama cha Soka cha Zanzibar (ZFA) zilisema kwamba baadhi ya timu zimeshawasili kwa ajili ya mashindano hayo.
Michuano ya mwaka huu inatarajia kuwa na ushindani mkali kutokana na kushirikisha timu nyingi kubwa na zinazofahamiana kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WILFIED BONY AWINDWA NA MAN CITY

24457D2A00000578-0-image-a-54_1420058218252
Wilfried Bony anawindwa na Manchester City 
 
Manchester City wameanza mazungumzo ya kumsajili mshambuliaji wa Swansea City, Wilfried Bony kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 25.
Mwenyekiti wa Swansea,  Huw Jenkins  alisema jana kuwa klabu yake haijapokea ofa yoyote mpaka sasa, lakini City wameshafungua mazungumzo ili kumnasa Muivory Coast huyo ambaye pia anawaniwa na Real Madrid.
Mazungumzo yalifanyika na washauri wa Bony jana usiku.
Wiki ijayo Bony ataenda Abu Dhabi ambapo Ivory Coast imeweka kambi ya kujiandaa na michuano ya mataifa ya Afrika mwaka huu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...