Wednesday, April 04, 2018

TAZAMA MUONEKANO MPYA WA MBOWE BAADA YA KUKAA MAHABUSU KWA SIKU SABA



Baada ya kukaa mahabusu kwa siku saba na kusherehekea sikuu ya Pasaka wakiwa gerezani, Mwenyekiti wa Chadema Taifa  Mhe. Freeman Mbowe pamoja na vigogo wengine sita wa chama hicho leo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaachia kwa dhamana, baada ya kukamilisha masharti.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRIL 04, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS





KIKWETE AINGILIA KATI AFYA YA MZEE MAJUTO, HII HAPA AHADI YAKE

LICHA ya kufanyiwa upasuaji wa tezi dume bado hali ya staa wa filamu za Kibongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ ni tete ambapo Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’, amejitosa baada ya kumuona alivyodhoofu kwa sasa.

JK na Mzee Majuto walikutana uso kwa uso wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambako kulikuwa na shughuli ya utoaji tuzo za filamu zilizojulikana kwa jina la Tuzo za Kimataifa za Sinema Zetu ambapo walionekana wakiteta kwa dakika kadhaa kabla ya kila mmoja akaenda kukaa kwenye siti yake.

Mzee Majuto alionekana akiwa amedhoofu kwani aliingia ukumbini akitembea kwa msaada wa fimbo huku akionekana kutokuwa mchangamfu kama ilivyo kawaida yake, hali iliyowahuzunisha mashabiki wake waliokuwa ukumbini hapo.

AGNES MASOGANGE AKWEPA KWENDA JELA BAADA YA KULIPA FAINI

Msanii wa kupamba video za muziki (Video Queen), Agnes Gerald ‘Masogange’ amekwepa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kulipa faini ya Sh. milioni 1.5.

Msanii maarufu nchini, Agnes Gerald maarufu Masogange alikutwa na hatia ya kutumia dawa za kulevya na kuhukumiwa kwenda jela au kulipa faini.

 Hakimu wa Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Wilbard Mashauri, ametoa hukumu hiyo leo Aprili 3 na kuieleza mahakama kuwa Masogange katika kosa la kwanza amekutwa na hatia ya kutumia dawa za kulevya aina ya heroin na kosa la pili kutumia dawa za kulevya aina ya Oxazepam.

“Hivyo katika kosa la kwanza, mahakama inamhukumu kwenda jela miaka miwili au kulipa faini ya Sh1 milioni na kwa kosa la pili, amehukumiwa kwenda jela miezi 12 au kulipa faini ya Sh 500, 000,” amesema Hakimu Mashauri.

Februari 17 mwaka jana, aliyekuwa Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwaeleza wanahabari kuwa Masogange amepelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serikali kupimwa iwapo anatumia dawa hizo za kulevya.

NUKUU SITA (6) MAARUFU ZA WINNIE MANDELA ENZI ZA UHAI WAKE

Winnie Madikizela-Mandela, ex-wife of former South African President Nelson Mandela, arrives at the Union Buildings in Pretoria 27 April 2004 for the inauguration of President Tahbo Mbeki second and final term as the country celebrated the 10th anniversary of the end of apartheid. 
Winnie Madikizela-Mandela enzi za uhai wake.
 
Mwanasiasa na mwanaharakati aliyepigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela alifariki dunia Jumatatu akiwa na miaka 81.

Alikuwa mke wa zamani wa rais wa kwanza mweusi Afrika Kusini Nelson Mandela lakini alikuwa na msimamo mkali zaidi kumshinda hata Bw Mandela mwenyewe. Winnie alifahamika sana na wengi kama Mama wa Taifa.
Winnie Mandela, former wife of former South African President Nelson Mandela attends the opening of the 53rd National Conference of the African National Congress (ANC) on December 16, 2012 in Bloemfontein.
Winnie alikuwa nembo kuu ya vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, na ingawa sifa zake ziliingia doa miaka ya baadaye, lakini bado alitambuliwa kama mtetezi wa wanyonge.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...