Friday, May 30, 2014

WAMILIKI WA MAGARI WATAKIWA KURUDISHA MAGARI YAO KIWANDANI, SOMA HAPA UJUE NI GARI ZA AINA GANI

Kampuni kubwa ya kutengeza magari nchini Marekani imeagiza magari milioni 1.4 yarejeshwe kutokana na hitilafu ya usukani.
Takriban magari milioni 1.1 yaliyoundwa kwa mtindo wa kispoti yaliyokuwa yameuzwa Marekani Kaskazini yametakiwa kurejeshwa kwani huenda yana hitilafu kwenye usukani.
Vilevile magari mengine 200,000 yenye muundo wa Taurus yaliyoundwa kati ya mwaka wa 2010 na 2014 huenda yakakumbwa na tatizo ya kushika kutu kwa haraka.
Matukio kama hayo yaliyofanyika majuzi huenda yakaifanya kampuni hiyo kuvunja rekodi ya kutaka magari mengi zaidi yarejeshwe katika kipindi cha mwaka mmoja.
Urejesho huo umetokea wakati sakata ya usalama inawakumba wapinzani wakuu wa kampuni ya hiyo , General Motors (GM). GM ililaumiwa kwa kutotoa ilani za kiusalama kwamba baadhi ya magari yake hata baada ya kubaini kuwa magari hayo yanazima ghafla.
Dosari hiyo imehusishwa na vifo 13, ingawa wasanifu wa Marekani wanaamini kuwa idadi hiyo itaongezeka.
Pindi tangazo hilo lilipofanywa, kampuni za kutengeneza magari hayo pamoja na wasanifu wa Marekani wameongeza juhudi za kurejesha magari ambayo yanapatikana kuwa na dosari. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 30, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MMILIKI WAMANCHESTER UNITED, MALCOM GLAZER AFARIKI NA KUIACHA TIMU KWA WATOTO WAKE


Mmiliki wa Manchester United, Malcom Glazer amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 85, na kuacha umiliki wa klabu hiyo kwa watoto wake sita.
Familia ya bilionea huyo iliinunua Man United kwa gharama ya Euro 790 milioni Mei, 2005 licha ya pingamizi kali kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Hata hivyo, chini ya umiliki wake uliosababisha deni kubwa kwa klabu hiyo ‘’the Red Devils’’ walishinda taji la Ligi Kuu mara tano na Ligi ya Mabingwa 2008.
Watoto wa Mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuathiri umiliki wa Man United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo.
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenye hisa katika soko la hisa la NY stock Exchange. Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Bilionea huyo ambaye hakuwahi kukanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.

AUSTRALIA YAWA TIMU YA KWANZA KUWASILI BRAZIL NA REKODI YAKE YA MABAO 31-0

Australia-National-Football-Team-3 Timu ya soka ya Taifa ya Australia, maarufu kama ‘ Soccerrose’ ndiyo timu inayoshikilia rekodi ya kufunga magoli mengi katika mchezo mmoja duniani. Australia waliichapa, American Samoa magoli 31-0, April 11, 2001 katika mchezo wa kimataifa unaotambuli wa na FIFA…Soccerrose, walitua nchini, Brazil siku ya juzi  tayari kwa michuano ya kombe la dunia inayotaraji kuanza kutimua vumbi, juni 12.  Australia ipo katika kundi la pili sambamba na mabingwa watetezi, Hispania, makamu bingwa wa fainali zilizopita, Uholanzi, na Chile.

Kikosi cha kocha, Ange Postecoglou kimeshawahi kucheza michuano hiyo mara tatu na mafanikio yao makubwa ni kufika hatua ya 16 bora, mwaka 2006… Kwa mara ya kwanza, Australia, ilifuzu kwa fainali za mwaka 1974 zilizofanyika nchini Ujerumani na kuondoka patupu. 

Walipata suluhu-tasa dhidi ya Chile, kisha wakapoteza kwa waliokuwa wenyeji wa michuano, Ujerumani Mashariki, na Ujerumani Magharibi na kuondoshwa mashindanoni pasipo kufunga goli lotote. 
Ikiwategemea zaidi wachezaji wake wazoefu kama Tim Cahiil, na nahodha wa kikosi hicho, Michael Jadinak ambaye anakipiga katika kikosi cha Crystal Palece ya England ,kikosi hicho kimekuwa timu ya kwanza kuwasili, Brazil. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAIS BANDA "NITAHESHIMU MAAMUZI YA MAHAKAMA KUU"

Rais Joyce Banda wa Malawi akipungia wafuasi wake waliokusanyika huko Lilongwe wakati wa uzinduzi wa kampeni yake. Machi 29, 2014.
Rais Joyce Banda wa Malawi akipungia wafuasi wake waliokusanyika huko Lilongwe wakati wa uzinduzi wa kampeni yake.
Mahakama kuu inapanga Ijumaa kutoa maamuzi kama iwapo matokeo ya uchaguzi yatangazwe hadharani au kura zihesabiwe tena. Matokeo ya awali yamemuweka Bi. Banda nyuma ya mpinzani wake Peter Mutharika.
Bi.Banda anasema uchaguzi ulijaa ubadhirifu, ikiwemo pamoja na wizi wa kura na watu kupiga kura zaidi ya mara moja.
Ameliambia shirika la habari la reuters kwamba atakubali maamuzi ya mahakama kuu, akifahamu fika kuwa amejaribu kutetea haki za wamalawi kwa kuhakikisha kuwa kiongozi anachaguliwa kwa haki na utaratibu wa heshima. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Bi.Banda ameamuru uchaguzi mpya uitishwe katika kipindi cha siku 90 na kusema hatakuwa mgombea. Lakini mahakama kuu imebatilisha maamuzi yake pale chama kikuu cha upinzani kilipowasilisha malalamiko.
CHANZO:VOA

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...