Friday, May 30, 2014

MMILIKI WAMANCHESTER UNITED, MALCOM GLAZER AFARIKI NA KUIACHA TIMU KWA WATOTO WAKE


Mmiliki wa Manchester United, Malcom Glazer amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 85, na kuacha umiliki wa klabu hiyo kwa watoto wake sita.
Familia ya bilionea huyo iliinunua Man United kwa gharama ya Euro 790 milioni Mei, 2005 licha ya pingamizi kali kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo. Hata hivyo, chini ya umiliki wake uliosababisha deni kubwa kwa klabu hiyo ‘’the Red Devils’’ walishinda taji la Ligi Kuu mara tano na Ligi ya Mabingwa 2008.
Watoto wa Mmarekani huyo waliozaliwa Marekani Byan, Joel, na Avram wote wamejumuishwa katika bodi ya klabu hiyo, huku Joel na Avram wakiwa wenyekiti wenza.
Kifo cha Glazer hakitarajiwi kuathiri umiliki wa Man United, kwani familia hiyo bado inamiliki asilimia 90 za hisa za klabu hiyo.
Asilimia 10 inayosalia inamilikiwa na wenye hisa katika soko la hisa la NY stock Exchange. Glazer alikuwa pia mmiliki wa Tampa Bay Buccaneers, iliyobadili sura ya kandanda ya Marekani kwa kushinda taji la Super Bowl. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Bilionea huyo ambaye hakuwahi kukanyaga uwanjani Old Trafford kutokana na hofu ya kuwaudhi mashabiki wa timu hiyo ambao walikuwa wanamsuta kwa kupanga njama ya kuinunua klabu hiyo kwa kutumia madeni.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...