Wednesday, December 13, 2017

VIGOGO WENGINE WA ACT WAHAMIA CCM

 Mwenyekiti na katibu wa Chama cha ACT Wazalendo mkoani Singida, wamejivua uanachana na vyeo vyao na kuhamia CCM.

Viongozi hao ni aliyekuwa mwenyeketi Wilfred Noel Kitundu na katibu wa mkoa wa chama hicho, Loth Robert Thomas.
Viongozi hao wamechukua uamuzi huo mbele ya mkutano mkuu wa uchaguzi CCM mkoa wa Singida uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uhazili mjini hapa juzi.

Kwa nyakati tofauti walisema changamoto ambazo upinzani walikuwa wakizipigia kelele, Rais John Magufuli ameendelea kuzitatua kwa ufanisi.

Tuesday, December 05, 2017

MBWA WA POLISI WAMUUMBUA ALIEDANGANYA KUWA KAPOLWA MIL. 20 ZA KAMPUNI

Mfanyakazi  wa kampuni ya saruji ya Simba Cement, Edward Ngassa amekamatwa na Jeshi la Polisi mkoani Dodoma kwa tuhuma za kutengeneza tukio la uongo la kuporwa Sh. milioni 20.4 na majambazi jana.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, mbwa wa polisi mwenye mafunzo ndiye aliyegundua udanganyifu huo wa Ngassa nyumbani kwake.

Kamanda Muroto alisema mtuhumiwa huyo alitengeneza tukio la uongo kwamba ameporwa fedha na majambazi katika eneo la Uhindini karibu na mgahawa wa Sunja.

Saturday, December 02, 2017

MKULIMA AFARIKI KWA KUPIGWA NA RADI AKIWA SHAMBANI USIKU

Mkazi mmoja wa kijiji cha Senga Kata ya Kamsamba wilaya ya Momba aliyetambuliwa kwa jina la Cleo Saini (23/25)amefariki baada ya kupigwa na radi alipokuwa analima kwa jembe la kukokotwa na ng'ombe mapema saa tisa usiku.

Pamoja na marehemu kufariki pia ng'ombe wawili waliokuwa wakikokota jembe wamekufa. Mtendaji wa kijiji cha Kamsamba Venance Athanas ametoa taarifa Polisi Kituo cha Kamsamba.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe Mathias Nyange amekiri kutokea kwa tukio ambapo Polisi wamekwenda eneo la tukio kwa uchunguzi zaidi wa tukio hilo.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DECEMBER 02, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

https://jambotz8.blogspot.com/

 
Subscribe katika YouTube channel ya Jambo Tz upate kuona habari na matukio mbalimbali toka duniani kote.

MBUNGE NASSARI AVAMIWA NA MAJAMBAZI USIKU WA LEO

Katika ukurasa twitter wa Mh. Joshua Nassari ameandika kuwa amevamiwa na watu waliokuwa na silaha za moto, na mara baada ya yeye pamoja na mkewe kuwagundua waliamua kukimbilia kituo cha polisi yeye ili kuokoa maisha yao.

Sunday, November 26, 2017

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU SABA KWA VYOMBO VYA UCHUNGUZI KUBAINI MMILIKI WA MAGARI YALIYOTELEKEZWA BANDARINI

Haya ndio maagizo ya Rais John Pombe Magufuli Bandarini leo baada ya kugundua uwepo wa magari zaidi ya 50 yaliyoingizwa nchini kwa kutumia jina la Ofisi ya Rais.

Saturday, November 25, 2017

TAZAMA VIDEO YA WAZIMBABWE WAKIIGIZA JINSI MUGABE ALIVYOLAZIMISHWA KIJIUZULU

Subscriber to our channel on YouTube @jambotz upate video nyingine zaidi.

PROF. LIPUMBA "SIKUTEGEMEA KAMA DR. SLAA ATATEULIWA"

Mwenyekiti wa Chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba amezungumzia uteuzi wa Dk. Wilbroad Slaa kuwa balozi akisema hakutarajia.

Rais John Magufuli juzi alimteua Dk. Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa Chadema kabla ya kukihama chama hicho wakati wa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wakati wa mchakato wa uchaguzi huo, Profesa Lipumba na Dk. Slaa ambao vyama vyao vilikuwa katika umoja uliojulikana Ukawa, walijiondoa baada ya Chadema kumpitisha Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa kuwa mgombea wake wa urais.

Akizungumza na Mwananchi jana, Profesa Lipumba alisema, “Imekuwa kama surprise, sikutegemea kama Dk. Slaa atateuliwa kwa sababu muda mwingi yupo Canada”.

Hata hivyo, Profesa Lipumba alisema hana shaka na uteuzi huo “Narudia, sikutegemea. Ila popote atakapopangiwa kazi Dk. Slaa atafanya kwa sababu najua ni mchapakazi,” alisema.
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema Rais Magufuli ana mamlaka kisheria ya kumteua mtu atakayemuona anafaa katika nafasi fulani.

FAMILIA YAPATA UPOFU KATIKA MAZINGIRA TATANISHI

(Picha hii haihusiani na tukio)

Mama mmoja aliyetambulika kwa jila la Doroth Otieno na watoto wake watatu wanaoishi Kisumu nchini Kenya, wamepata upofu wa ghafla bila kujua chanzo chake.

Doroth ambaye ameolewa na mkata miwa nchini Kenya, amesema hali hiyo imeleta matatizo kwenye ndoa yake na familia.

Akisimulia jinsi alivyopata upofu wake huo Doroth amesema mtoto wake wa kwanza nwenye miaka 16 na mwanafunzi wa kidato cha kwanza sekondari ya wasichana ya Nyamonye, alipata upofu ghafla baada ya kuhisi kama macho yake yana mchanga, na kisha kuwa kipofu kabisa, huku watoto wake wawili wa kiume Vicent na Benson nao wakiwa na tatizo hilo hilo.

MUGABE NA MKEWE WASUSIA SHEREHE ZA KUAPISHWA RAIS MPYA

 Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace walikosa kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mpya wa nchi hiyo Emmerson Mnangagwa baada ya wananiasa hao kukubaliana kwamba Mugabe anaweza kupumzika.

Sababu kuu ilioteolewa ni kwamba bwana Mugabe alikuwa amechoka.
Mugabe na mkewe Grace hawajaonekana hadharani tangu kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kujiuzulu kama rais kufuatia shinikizo kutoka kwa jeshi na raia.

Hatua hiyo inajiri baada ya Mugabe na mkewe kufumta kazi rais huyo mpya wakati alipokuwa makamu wa rais kwa madai kwamba alikuwa akipanga njama za kutaka kumuondoa madarakani rais Mugabe.

Saturday, November 18, 2017

WALEMAVU DAR WAANZA KUPATA NEEMA.

Hospitali ya CCBRT imeguswa na kampeni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ya kutafuta miguu bandia kwaajili ya watu wenye uhitaji kwa kuwapatia matibabu wagonjwa 35 waliokatwa miguu kutokana na ugonjwa wa kisukari.
Miguu hiyo ya kisasa ina thamani ya zaidi ya Shilling Million 157 ambapo kati ya wagonjwa 35 waliokuwa wakitembelea magongo kwa muda mrefu baada ya kukatwa miguu, 21 wameshawekewa Miguu Bandia na sasa wanaendelea na shuguli zao baada ya kuwa wazima.

Tuesday, November 14, 2017

TAZAMA VIDEO YA DR. SHIKA AKIREJEA NYUMBANI KWAKE KUTOKA KITUO CHA POLISI ALIPOKUWA AKISHIKILIWA


Dkt. Luis Shika akiwasili nyumbani akitokea Polisi.
Afafanua kwanini hakuweza kulipa 25% iliyokiwa mnadani adai tatizo ni kutokuelewana.

Monday, November 13, 2017

LULU AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA MIWILI JELA

Mahakama kuu ya Dar es salaam imemuhukumu muigizaji wa filamu, Elizabeth Michale, maarufu kama 'Lulu', kifungo cha miaka miwili baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia msanii mwenzake marehemu Steven Kanumba.

Marehemu Steven Kanumba alifariki majira ya saa nane usiku, mnamo mwaka 2012 baada ya kutokea mzozo kati yake na Elizabeth Michael ambaye inaaminika kuwa walikuwa na uhusiano wa Kimapenzi.
Kanumba, ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati na hadi Afrika Magharibi baada ya kuwashirikisha katika filamu zake baadhi ya wasanii maarufu wa kutoka Nigeria akiwemo Mercy Johnson na Noah Ramsey.

Wednesday, November 08, 2017

MCHUNGAJI AWANANGA WANAWAKE WANAOONGEZA MAKALIO NA MAZIWA

Huu ni ushauri wa bure kwa wote wenye tabia ya kubadili uumbaji wa Mwenyezi Mungu. Share ili wenye tabia hiyo wajifunze na kuacha.

Sunday, November 05, 2017

MAAJABU: MCHUNGAJI ATUMIA POMBE KUBATIZA WAUMINI

Mchungaji mmoja huko Afrika Kusini amekuwa akikosolewa vikali baada ya kuanza kubatiza washirika kwa kutumia vilevi ambavyo wanavipenda kitendo ambacho ni kinyume na utaratibu.

Askofu Tsietsi Makiti, (52) ambaye pia  ni Mwanzilishi wa kanisa hilo linalojulikana kama 'Gabola', amesema kuwa ameongozwa na maandiko katika Biblia ambapo Yesu alibadilisha maji kuwa divai.
"Watu wanao kunywa na kubatizwa na bia wana furaha na amani. Hii inamaanisha kuwa wanaishi katika kivuli cha Mungu, "alisema Makiti.

Kanisa hilo lenye jina 'Gabola' jina likimaanisha 'Kunywa' limesema linakubali kuwapokea waumini waliotoka makanisa mengine huku likiweka wazi kwamba idadi ya watu wameongezeka kufikia 500 ndani ya miezi miwili tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo.

Waumini pia wanaruhusiwa kunywa wakati huduma za kanisa zikiendelea. Aidha Askofu huyo ameweka wazi kwamba ana mipango ya kuanzisha matawi ya kanisa lake hilo katika miji mbali mbali.

Saturday, October 28, 2017

TAZAMA PICHA ZA MAFURIKO YALIYOATHIRI MAKAZI YA WATU DAR ES SALAAM

Mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha maeneo mengi pwani ya Tanzania imesababisha mafuriko na uharibifu mkubwa.

Katika eneo la Mji Mpya, Kawe, nyumba zimebomoka na baadhi ya maeneo hayapitiki. Nyumba zaidi ya 20 zimeharibiwa vibaya na mafuriko.

Hizi hapa ni baadhi ya picha za hali ilivyo mtaani humo.

WALIOMUINGIZA MTU MWEUSI KWENYE JENEZA AKIWA HAI WAFUNGWA

Wakulima wawili wa Afrika Kusini waliomlazimisha mtu mweusi kuingia katika jeneza akiwa hai wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela.

Theo Martins na Willem Oosthuizen walihukumiwa mnamo mwezi Agosti kwa jaribio la mauaji na utekaji nyara.

Walimtuhumu Victor Mlotshwa kwa kupita katika ardhi, wakamshambulia na kumlazimisha kuingia katika jeneza na kutishia kumchoma akiwa hai.


Kesi hiyo ilizua hisia nchini Afrika Kusini na kuangazia wasiwasi wa ubaguzi wa rangi katika jamii kadhaa za wakulima.

Friday, October 27, 2017

IDADI YA WALIOPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA MARUDIO NCHINI KENYA UTATA MTUPU

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati amesema wanakadiria kwamba idadi ya waliojitokeza kupiga kura jana kufikia wakati wa kufungwa kwa vituo saa kumi na moja jioni ni asilimia 48.

Akihutubia wanahabari, mwenyekiti huyo amesema vituo 87 kati ya vituo vyote vya kupigia kura vilifunguliwa, ambavyo ni vituo 35,564.

Kati ya vituo hivyo, fomu za matokeo kutoka kwa fomu za matokeo kutoka kwa fomu 27,124 zimepokelewa.

"Vituo 5,389 ambavyo vimetapakaa kote nchini havikufunguliwa. Baadhi vimo katika kaunti nne ambazo nilitangaza awali kwamba uchaguzi umeahirishwa," amesema.

VIDEO: RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

Rais John Magufuli amemteua aliyekuwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, huku aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Mangu akiteuliwa kuwa balozi.

Dk. Kashilillah ameteuliwa ikiwa ni takriban wiki tatu kupita tangu alipoondolewa katika wadhifa wa Katibu wa Bunge, nafasi iliyochukuliwa na Stephen Kigaigai.
Rais Magufuli Mei 28,2017 alitengua uteuzi wa IGP Mangu na kumteua Simon Sirro kushika wadhifa huo. Mangu anasubiri kupangiwa kituo cha kazi pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dk Aziz Mlima.

Monday, October 23, 2017

USHAHIDI ALIOUTOA LULU MAHAKAMANI KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

Msanii wa filamu, Elizabeth Michael (22) amejitetea katika kesi ya kuuwa bila kukusudia katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Katika utetezi wake, Lulu amesema anakumbuka siku ya tukio ilikuwa Ijumaa ya April 6, 2012 ambapo aliahidiana na rafiki zake kwamba wangetoka usiku.

Amesema kuwa asubuhi ya siku hiyo alienda kuonana na rafiki zake maeneo ya Mikocheni, ambapo pia alikuwa akiwasiliana na Kanumba.

"Marehemu alikuwa ni msanii mwenzangu lakini pia nilikuwa naye na mahusiano naye ya kimapenzi,".

Lulu alisema kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi kumuona akitoka, hivyo hadi siku ya tukio hakutaka kumwambia kwamba atatoka na rafiki zake.

Sunday, October 08, 2017

KIM JONG-UN AMPANDISHA CHEO DADA YAKE

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, amempandisha cheo dada yake mdogo, na kumpa madaraka zaidi katika chama tawala cha wafanyakazi.

Kim Yo-jong, anayeaminika kuwa na umri wa zaidi ya miaka 26 amekuwa mjumbe katika kamati kuu ya chama, ambalo ni baraza kuu la uamuzi linalojulikana kama politburo.

Bi Kim Yo-jong alipewa kwanza wadhifa wa kuwa afisa wa wa cheo cha juu wa chama, miaka mitatu iliyopita.

Familia ya Kim, imeongoza Korea Kaskazini, tangu nchi hiyo ilipoundwa, mwaka wa 1948.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 08, 2017 YA MICHEZO, DINI NA HARDNEWS





POLISI YADAI PANYA NDIO WALIOKULA MADAWA YA KULEVYA YALIYOKAMATWA

Police katika mji wa Mumbai nchini India wanawalaumu panya kwa kutoweka kwa kilo 34 za dawa za kulevya kwa jina Ketamine.

Wanasema wanawatuhumu panya hao kwamba ndio wa kulaumiwa baada ya kupata mabagi hayo yalitobolewa kwa chini.

Uchunguzi wa miaka mitatu umekamilika kwamba iwapo ingekuwa binadamu wangechukua mabagi yote.

Dawa hizo zilizohifadhiwa katika ghala moja la serikali zilikuwa miongoni mwa kilo 200 za mihadarati zilizopatikana na walanguzi wa mihadarati 2011.

Hii sio mara ya kwanza kwa maafisa wa polisi nchini India kuwalaumu panya kwa kutoweka kwa mihadarati iliokamatwa.

Saturday, October 07, 2017

RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI





'KUNA UWEZEKANO WA KUFANYIKA MAPINDUZI NCHINI ZIMBABWE' GRACE MUGABE

Mke wa rais Robert Mugabe, Grace Mugabe ameonya kwamba kuna uwezekano wa kufanyika kwa mapinduzi huku kukiwa kuna wasiwasi mkubwa nchini humo kuhusu harakati za kumrithi rais Mugabe.

Anasema kuwa washirika wa makamu wa rais Emmerson Mnangangwa wanatishia maisha ya wale ambao hawamuungi mkono kumrithi rais Robert Mugabe mwenye umri wa miaka 93.

Bi Mugabe yeye binafsi na bwana Mnangagwa wako kifua mbele na uadui wao umekigawanya chama tawala cha Zanu PF .

Mgogoro huo unajiri baada ya bwana Mgangagwa kudai kwamba aliwekewa sumu katika chakula chake mwezi Agosti.

Wafuasi wake wamesema kuwa wapinzani wake ndani ya Zanu PF ndio wakulaumiwa, ijapokuwa bwana Mnangagwa amejitenga na madai kama hayo.

Alikiambia chombo cha habari cha taifa hilo anasalia kuwa mtiifu kwa rais Mugabe.

Bi Grace Mugabe aliyekasirika alimshutumu bwana Mnangagwa katika hafla moja mjini Harare.

''Tunatishiwa usiku na mchana kwamba iwapo mtu fulani hatokuwa rais , tutauawa'', alisema.

MAREKANI YAIONDOLEA VIKWAZO SUDAN

Marekani imeiondolea vikwazo Sudan ikisema taifa hilo la Afrika lilikuwa limeanza kuangazia maswala kuhusu kukabiliana na ugaidi pamoja na ukiukeaji wa haki za kibinaadamu dhidi ya raia wanaoishi katika jimbo la Darfur.

Uamuzi wa kuiondolea vikwazo na kusitisha vikwazo vya kiuchumi wa taifa hilo unajiri baada ya utawala wa Trump mwezi uliopita kuliondoa taifa hilo katika mataifa ambayo raia wake wamewekwa vikwazo vya kusafiri.

Sudan ndio taifa la pekee ambalo liliondolewa katika orodha hiyo. Lakini uamuzi huo unaviacha vikwazo vingine kuendelea kwa sasa ikiwemo vile dhidi ya watu binafsi walio na agizo la kukamtwa kufuatia unyanyasaji uliofanyika katika eneo la Darfur.

Friday, September 29, 2017

OFISI YA BUNGE YAKANUSHA MBOWE KUNYANG'ANYWA GARI

Ofisi ya Bunge imekanusha kumnyang’anya gari mbunge Freeman Mbowe na kuwa linatafutiwa kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi ili Mbowe akalitumie Nairobi.

GAZETI LA MWANANCHI LATAKIWA KUOMBA RADHI

Serikali ya mapinduzi Zanzibar imewaagiza Wahariri wa Gazeti la Mwananchi kuomba radhi Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) ndani ya saa 24 kuanzia saa 9:00 Alasiri ya jana Septemba 28, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa naNaibu Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Zanzibar, Dk. Juma Mohammed Salum ambapo amesema iwapo wahusika hawatafanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya gazeti hilo la Mwananchi.

Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali kudai gazeti hilo la Mwananchi linalochapishwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited Septemba 27, 2017 kuchapisha makala katika Ukurasa wake wa 16 yenye kichwa cha habari kisemacho “Siri ya nini Zabuni ya Mafuta Zanzibar”?

Salum amefafanua kuwa makala hiyo licha ya kujenga picha kwamba hakuna uwazi katika Zabuni ya uletaji Mafuta Zanzibar,msingi na maudhuhi ya Makala yenyewe kwa ujumla ni upotoshaji wa makusudi kwa nia ya kuipaka matope Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Taarifa hiyo pia licha ya kuwataka wahariri wa gazeti hilo kuomba radhi pia imefafanua ukweli wa mambo yalivyo kwa sasa ambapo Serikali, kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) tayari imeanzisha mfumo mpya wa uletaji Mafuta Zanzibar tangu Septemba Mosi, 2017.

Saturday, September 09, 2017

WATOTO WALIOPO TUMBONI WAKUTWA NA MATATIZO YA MOYO

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Naiz Majani.
 
JUMLA ya wajawazito 35 wamefamyiwa  uchunguzi wa kipimo cha magonjwa ya moyo kwa watoto wachanga waliopo tumboni mwa mama zao (FETAL ECHOCARDIOGRAPHY) ili kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la.

Majibu ya kipimo hicho yalionyesha kuwa kati ya hao watoto watano walikutwa na matatizo ya moyo jambo ambalo litawawezesha   kupata matibabu mapema pindi watakapozaliwa.

Hayo yamesemwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani wakati akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.

Dkt. Naiz alisema kipimo hicho hakina madhara yoyote kwa mama na mtoto na kina  uwezo wa kugundua endapo mtoto ameathirika na ugonjwa wa moyo na hivyo kumuandaa mama mjamzito kwaajili ya uzazi salama.

“Mojawapo ya dalili za mama mjamzito ambazo zinaweza pelekea kupata mtoto mwenye  tatizo la ugonjwa wa moyo ni pamoja na ugonjwa wa kisukari,shinikizo la damu,matumizi ya dawa za muda mrefu,mimba ya mapacha, kuwepo na mtu mwenye tatizo la moyo katika familia na mimba pandikizi”.

“Ninawaomba kina mama wajawazito wenye moja ya dalili nilizozitaja waje tuwafanyie kipimo hiki  kipindi  ambacho mimba zao zitakuwa na umri wa kati ya miezi minne hadi saba hii itawasaidia  kugundua afya za watoto wao na kuepuka na  vifo vya mara  baada ya kuzaliwa vinavyotokea kipindi cha mwezi mmoja hadi  mwaka”, alisema Dkt. Naiz.

Alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa kinamama wajawazito juu ya kipimo hicho kwa kufikiria kuwa kinamadhara  jambo ambalo siyo kweli kwani kipimo hicho hakina  madhara yoyote kiafya.

Taasisi ya Moyo  Jakaya Kikwete (JKCI) ilianza kutoa huduma hiyo tangu mwezi wa tatu mwaka huu ili kupunguza  vifo vya watoto vinavyotokana na  magonjwa ya moyo mara baada ya mtoto kuzaliwa.
Na Sweetbert Hudson.

Wednesday, September 06, 2017

WANAFUNZI 917,072 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA LEO

Baraza la Taifa la Mitihani nchini (NECTA) limesema maandalizi ya kuanza mtihani wa Taifa wa darasa la saba utakaofanyika leo jumatano Septemba 6 na kesho alhamisi ya Septemba 7 yamekamilika.

Akizungumza na wanahabari kuhusu maandalizi hayo, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde. Tayari mitihani imesafirishwa katika maeneo yote nchini na kinachosubiriwa kwa sasa ni kuanza kwa mtihani.

“Leo na kesho katika shule zetu 16,583 za msingi nchini kutakuwa ana mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, watahiniwa ni 917,072 wataufanya wavulana wakiwa 432,744 sawa na asilimia 47.19%, wasichana ni 484,328 sawa na asilimia 52.81%, mwaka jana watahiniwa walikuwa 795,761.

EMIRATES TANZANIA YAPATA BOSI MPYA

Uongozi wa shirika la ndege la kimataifa la Emirates umemteua Bwana Rashed Alfajeer kuwa meneja mkuu mpya wa shirika hilo nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa shirika hilo nchini Tanzania inasema, Bwana Alfajeer, kutoka katika nchi za Falme za Kiarabu, atakuwa na jukumu la kusimamia shughuli zote za Emirates za kibiashara, wateja na mizigo kwenye soko.

"Nina furaha kwa kuchaguliwa kuwa meneja mpya wa Emirates nchini Tanzania na ninatarajia kufanya kazi na timu ya ndani, pamoja na washirika wetu wa biashara katika kuendeleza biashara zaidi ya Emirates kwenye soko," alisema Alfajeer.

"Mtazamo wangu utakuwa kuendelea kuwapa wateja wetu wa Tanzania huduma bora kulingana na thamani ya pesa, tunapowaunganisha kwenye maeneo zaidi ya 150 ulimwenguni kote," aliongeza.

Bwana Alfajeer alijiunga na Emirates mwaka 2013 kama sehemu ya mpango wa Emirates kama msimamizi wa Taifa wa Uendeshaji wa Biashara. Tangu wakati huo, amefanya kazi za biashara nchini Sri Lanka kabla ya kuchukua nafasi ya Meneja wa Wilaya huko Dammam, Saudi Arabia mwaka 2015.

Emirates hufanya safiri mara moja kwa siku kati ya Dar es Salaam na Dubai na ndege kubwa aina ya Boeing 777.

HASHIM RUNGWE ASHIKILIWA NA POLISI

Aliyekuwa mgombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Hashim Rungwe anashikiliwa na polisi kwa siku nne sasa.

Rungwe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Chaumma anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. Mwanasiasa huyo anashikiliwa akituhumiwa kughushi nyaraka.

Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema jana Septemba 5 kuwa, Rungwe anashikiliwa kituoni hapo kwa siku nne.

Hata hivyo, Kamanda Mambosasa hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo akisema hana taarifa za kutosha.

JAJI MARAGA AMJIBU UHURU KENYATTA

JAJI Mkuu David Maraga amejibu shutuma kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine wa Chama cha Jubilee, kufuatia uamuzi wa  Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais.

Viongozi wa Jubilee wamemkosoa Maraga wakidai anatumiwa na upinzani kutoa maamuzi yanayoupendelea muungano wa NASA, na wameapa  kuupitia uamuzi huo wa mahakama wakati uchaguzi utakapomalizika.

“Mimi si mwanasiasa na ninafanya kazi kwa kuzingatia misingi ya kiapo cha utii nilichoapa kuwatumikia Wakenya. Siungi mkono Jubilee wala NASA au  mtu yeyote,” alisema Jaji Maraga katika taarifa yake fupi jana.

Rais Kenyatta mwishoni mwa wiki iliyopita alimkosoa Maraga akimwita ‘mkora’, kwamba ‘alipindua’ matakwa ya mamilioni ya Wakenya waliomchagua.

Kufuatia vitisho hivyo, ambavyo vimelaaniwa vikali na wanaharakati na katika mitandao ya jamii, Maraga ambaye ni mzee wa Kanisa la Sabato (SDA),  alisisitiza kuwa anamwogopa Mungu pekee.

“Ninafuata katiba yetu. Nendeni mkaendeshe uchaguzi na iwapo mtu anapinga, lete shauri ukiwa na ushahidi mzuri na nitalifanyia kazi ipasavyo.  Kumbuka namhofia Mungu pekee,” alisema Maraga ambaye anaongoza mfumo wa mahakama

Friday, August 18, 2017

MAPACHA WALIOSHIKANA WAFARIKI MUHIMBILI

Pacha walioshikana ambao walikuwa wamelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili mjini Dar es Salaam wamefariki kwa mujibu wa msemaji wa hospitali hiyo.

Pacha hao waliokuwa wakifanyiwa vipimo ili kuwaanda kwa upasuaji walifariki siku ya Jumanne kulingana na bi Neema Mwangomo. Watoto hao walizaliwa wilayani Kilosa katika eneo la Morogoro. Familia yao ilitoka katika kijiji cha Chaumbele.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Bi Mwangomo alisema kuwa wataalam watatoa maelezo katika wakati ufaao.

Pacha hao walioshikana chini ya kifua na tumboni walikuwa wakitumia ini moja na mishipa ya moyo lakini kila mmoja alikuwa na tumbo lake.

Awali daktari wa watoto Dkt Zaituni Bokhary alitumai kwamba pacha hao wanaweza kutenganishwa watakapofikisha umri wa miaka sita.

MUGABE: 'WALIOWAUA WAZUNGU HAWATASHITAKIWA'

Rais Robert Mugabe, ameuambia umati wakati wa sherehe za siku ya mashujaa jijini Harare Jumatatu wiki hii kuwa watu waliowaua wakulima wa kizungu wakati wa mabadiliko ya sheria ya ardhi nchini Zimbabwe hawatashtakiwa.

“Ndiyo, tuna wale waliouawa wakati wakipinga ukoloni. Hatuwezi kuwashtaki wale waliowaua wazungu. Je, tutawashtaki vipi?” alisema Mugabe.

Wakati wa ukoloni, ardhi nzuri ilitengwa kwa wazungu, lakini mwaka 2000, Mugabe aliongoza kutwaliwa kwa ardhi hiyo kutoka kwa wakulima 4,000 wa kizungu.

Rais Mugabe awali alikiri kuwa mifumo ya ardhi ya nchi hiyo ilishindwa na mwaka 2015 alisema: “Nafikiri mashamba tuliyowapa watu wetu ni makubwa, hawawezi kuyasimamia.”

Kutwaliwa ghafla mashamba kutoka kwa wakulima wazungu, inaonekana kuwa sababu kuu ya kuporomoka kwa uchumi wa Zimbabwe tangu mwaka 2000.

DANGOTE: 'NIKIINUNUA ARSENAL NITAMFUKUZA WENGER'

Mfanyabiashara tajiri raia wa Nigeria Aliko Dangote, ambaye anaorodheshwa kuwa mtu tajiri zaidi Afrika, amesema kuwa atamfuta kazi meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ikiwa atafaulu kuinunua klabu hiyo ya Uingereza, kwa mujibu wa shirika la Bloomberg.

Wakati wa mahojiano na shirika hilo, Dangote alisema kuwa atajaribu kuinunua klabu hiyo, wakati ujenzi wa kiwanda chake cha kusafisha mafuta cha gharama ya dola bilioni 11 mjini Lagos utakapokamilika.

Bw. Dangote anasema amekuwa shabiki wa Arsenal tangu mwaka 1980.

Wenger ni mmoja wa mameneja wa kandanda wanaosifika sana barani Ulaya na hivi majuzi, alisaini mkataba wa miaka miwili na kuendelea kuwa na klabu hiyo kwa zaidi ya miongo miwili.

Kuna maoni tofauti kutoka kwa wafuasi wake, wengine wakisema kuwa klabu hiyo inahitaji meneja mpya ili kiweze kurejea hadhi yake.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...