Saturday, November 25, 2017

MUGABE NA MKEWE WASUSIA SHEREHE ZA KUAPISHWA RAIS MPYA

 Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace walikosa kuhudhuria sherehe ya kuapishwa kwa rais mpya wa nchi hiyo Emmerson Mnangagwa baada ya wananiasa hao kukubaliana kwamba Mugabe anaweza kupumzika.

Sababu kuu ilioteolewa ni kwamba bwana Mugabe alikuwa amechoka.
Mugabe na mkewe Grace hawajaonekana hadharani tangu kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kujiuzulu kama rais kufuatia shinikizo kutoka kwa jeshi na raia.

Hatua hiyo inajiri baada ya Mugabe na mkewe kufumta kazi rais huyo mpya wakati alipokuwa makamu wa rais kwa madai kwamba alikuwa akipanga njama za kutaka kumuondoa madarakani rais Mugabe.

Aliyekuwa makamu wake wa rais Emmerson Mnangagwa amewataka raia wa Zimabwe kusalia watulivu na kuweka amani na kutolilipiza kisasi.

Umati mkuwa wa takriban raia 60,000 wa Zimbabwe wakiwemo viuongozi wa kimataifa na wanadiplomasia walihudhuria sherehe ya kumuapisha Mnangagwa katika uwanja wa michezo wa mj9ini harare.

Upinzani umemtaka rais mpya kukabiliana na ufisadi wakati rais Mugabe alipolazimishwa kuondoka madarakani siku ya Jumanne baada ya jeshi kuchukua mamlaka kulikuwa na sherehe matika maeneo tofauti ya taifa hilo.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...