Thursday, May 28, 2015

MWANASHERIA KENYA AJITOSA KUMUOA MTOTO WA OBAMA...!!!

Rais Barrack Obama wa Marekani akiwa na mtoto wake Malia. 

Mwanasheria kijana nchini ametuma ombi la kumuoa mtoto wa Rais Barack Obama anayeitwa Malia.
Mwanasheria Felix Kiprono alisema jana kwamba yupo tayari kutoa ng’ombe 50, kondoo 70 na mbuzi 30 ikiwa ni mahari ya kumposa mtoto huyo.
Alisema kuwa analazimika kufanya hivyo ili kutimiza ndoto yake ya muda mrefu ya kumuoa mtoto wa Rais Obama.
“Nimevutiwa kumchumbia Malia tangu mwaka 2008,” alisema Kiprono baada ya kuhojiwa na gazeti la The Nairobian. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

ODAMA: NAOGOPA MSAADA WA MASHARTI...!!!

Odama
Jennifer Kyaka ‘Odama

MWIGIZAJI mwenye mvuto katika filamu za Bongo, Jennifer Kyaka ‘Odama’, amesema anaogopa marafiki wa kiume kwa kuwa huwa na masharti magumu pindi wanapotoa msaada.
“Wasanii wa kiume kwangu sipendi kwa kuwa huwa na masharti kuliko marafiki wa kike ambao husaidia bila masharti ya ajabu,” alisema.
Aliongeza kwamba, marafiki wa kike anakuwa huru kuwaeleza shida na matatizo yake kuliko wa kiume ndiyo maana hiyo ni sababu yake nyingine ya kutopenda marafiki wa kiume kama anavyopenda marafiki wa kike. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS MEI 28, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03017
DSC03018
DSC03019
Nunua gari bei rahisi bofya hapa. Pia tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

"NATAKA KUWA MCHEKESHAJI" INSPEKTA HAROON

INSPECTOR.
Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’

UNALIKUMBUKA kundi la Gangwe Mobb, hapo lazima utamtaja Haruna Kaena ‘Insepkta Haroun’ na Luten Kalama, wawili hao baada ya kutengana kila mmoja akawa anafanya kazi binafsi lakini sasa Inspekta Haroun ameibuka na kudai kwamba anataka kuwa mwigizaji wa vichekesho.
Inspekta Haroun aliyetamba na wimbo wa ‘Mtoto wa Geti Kali’ aliendelea kueleza kwamba fani anazozipenda ni muziki na kuigiza vichekesho.
“Mimi msanii hivyo natakiwa niwe mbunifu, nisibweteke na kazi, fani moja na kwa sasa napenda kuwa mwigizaji wa vichekesho kwa kuwa napenda kazi hiyo na ninaiweza,” alijinadi.
Msanii huyo aliwahi kushirikishwa katika vipengele vya uigizaji katika kipindi cha vichekesho kilichokuwa kikirushwa na televisheni ya Clouds. Nunua gari bei rahisi bofya hapa.

WABUNGE WAMKAANGA MAGUFULI

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli 

Waziri wa Ujenzi, Dk John Pombe Magufuli amekuwa hapati wakati mgumu anapowasilisha bajeti ya wizara hiyo, lakini hali ilikuwa tofauti jana wakati wabunge walipoungana kueleza hofu yao katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara kutokana na madeni ya makandarasi.
Wabunge hao walidiriki kueleza kuwa kuna ufisadi katika ununuzi wa kivuko cha Bagamoyo na wengine kueleza kuwa miradi iliyotajwa kwenye hotuba ya bajeti ilishatekelezwa miaka ya 80 na 90.
Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Miundombinu kuhusu bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2015/2016 iliyosomwa na Makamu Mwenyekiti, Profesa Juma Kapuya, deni linalodaiwa na makandarasi ni kati ya Sh850 bilioni na Sh900 bilioni.
“Kamati haijaridhishwa kabisa na hali hii kwani deni hili sasa ni kubwa kuzidi hata bajeti inayotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wizara hii, jambo ambalo linafanya bajeti hii kuonekana ni kiini macho tu,” alisema Profesa Kapuya.
Kambi ya Upinzani
Katika taarifa yake, Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB) ilimshutumu Waziri Magufuli kwa kuandika hotuba ndefu ili kuwachanganya wabunge, huku hotuba hizo zikitaja hata miradi ya barabara zilizojengwa miaka ya 80 na 90.

Friday, May 22, 2015

UCHAGUZI FIFA, WAWILI WAJITOA


Nembo ya shirikisho la soka Duniani FIFA
Wagombea wawili kati ya wanne waliojitokeza kuwania nafasi ya urais wa shirikisho la vyama vya soka Duniani FIFA wamejitoka katika kinyang'ang'anyiro hicho.

Nyota wa zamani wa soka huko Ureno , Luis Figo ambaye ni mmoja wa waliojitoa kuwania nafasi hiyo,amelalamikia mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi huo na kuiita kuwa ni wakinafiki.

Amesisitiza kuwa kwa mtazamo wake anaona kuwa taratibu zilizowekwa zililenga kumnufaisha mgombea mmoja tu na si kuelta usawa wa wote waliojitokeza kuwania nafasi hiyo,ambapo inaonekana kuwa ni mpango uliowekwa kumpatia nafasi ya ushindi Rais wa sasa Sepp Blatter ambaye anawania nafasi hiyo kwa kipindi cha tano.

Hata hivyo Rais wa chama cha soka huko Uholanzi , Michael van Praag , akijitoa. Huku wapinzani waliosalia ni Bw Blatter ambaye ni Jordan Prince Ali Al Hussein ambaye ni mwanachama wa kamati ya utendaji ya FIFA.

Mgombea mwingine aliyejitoa pia ni Rais wa chama cha soka cha Uholanzi Michael van Praag na hivyo kuwaacha Blatter na mtu anayedaiwa kuwa mpinzani wake wa karibu Prince Ali Al Hussein ambaye ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, May 20, 2015

MICHUANO YA COSAFA YAANZA AFRIKA KUSINI

Michuano ya COSAFA,nchini Afrika Kusini Michuano ya kumi na tano ya Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu kusini mwa Afrika,COSAFA imezikutanisha timu za ukanda huo nchini Afrika Kusini. Michuano hiyo ilianza kutimua vumbi Jumapili mei 17 na itakamilika mei 30 .

Timu 12 kati ya 14 kutoka nchi wanachama wa COSAFA tayari zipo nchini Afrika Kusini kuchuana katika mashindano hayo.

Angola na Comoro ambazo ni wanachama wa COSAFA hazikuweza kushiriki mwaka huu. Nafasi zao zimechukuliwa na Ghana iliyofikia fainali za michuano ya Caf ya mwaka huu na Tanzania kutoka ukanda wa Afrika mashariki na kati ikiwa mwanachama wa CECAFA.

Monday, May 18, 2015

NKURUNZIZA AWAFUKUZA KAZI MAWAZIRI WATATU

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza .

Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, amewafuta kazi mawaziri watatu, huku maandamano yakiendelea katika mji mkuu kufuatia jaribio la mapinduzi, juma lililopita. 

Mawaziri walioachishwa kazi ni wa Ulinzi, mashauri ya nchi za kigeni na biashara. 

Mapema hii leo, polisi walifyatua risasi hewani katika mji mkuu Bujumbura, kujaribu kuutawanya umati wa vijana uliokuwa ukifanya ghasia.

IS WAUTEKA MJI WA RAMADI


Wapiganaji wa Islamic State

Baada ya mapigano makali kwa siku kadhaa katika mji wa Ramadi nchini Iraq, hatimaye mji huo kwa sasa unashikiliwa na wapiganaji wa kundi la IS.

Makundi ya wanajeshi wa serikali wamekimbia kutoka katika eneo hilo na Islamic State wamejitangazia ushindi dhidi ya mji huo na kwamba wanaushikilia. 

Mapema msemaji wa Gavana wa jimbo hilo amesema kuwa wapiganaji hao wanayashikilia baadhi ya majengo mhimu ya serikali katika jimbo hilo. 

Hata hivyo umoja wa Mataifa umelaani hatua hiyo ya IS, ambapo pia Waziri Mkuu wa Iraq Haider al-Abadi amesema kuwa kwa sasa wanajipanga kwa kushirikiana na majeshi ya Shia ili kukabiliana na wapiganaji hao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAN CITY YAICHAPA SWANSEA 4-2

Yaya Toure mshambuliaji wa Man City

Matokeo ya Mechi mbili za ligi kuu ya England zilizochezwa hapo jana,Manchester City iliwachabanga Swansea mabao 4-2 .

Ni Wilfried Bony ambaye mnamo dakika ya 90 lililopigilia msumali wa moto kwa Swansea baada ya kufunga bao la nne.

Lakini Yaya Toure yeye alizifumania nyavu mara mbili dakika 21 na 74. , James Milner naye akifunga mnamo dakika ya 36.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Huku katika mechi ya pili Arsenal wakitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya Man united,ambapo kwa matokeo hayo sasa Arsenal wanaendelea kujiimarisha katika nafasi ya tatu. Leo West Brom watakipiga na Chelsea katika dimba la The Hawthons.

Sunday, May 17, 2015

'SI IKULU ILIYOWASAFISHA MAWAZIRI' PINDA


Waziri Mkuu Mizengo Pinda. 

Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewajibu wabunge waliokosoa kitendo cha mawaziri watano waliotajwa kwenye kashfa za Operesheni Tokomeza na akaunti ya escrow, akisema Ikulu haikuhusika kuwasafisha bali ilitangaza matokeo ya uchunguzi wa tume. 

Mtendaji huyo mkuu wa Serikali pia amesema mawaziri hao bado wanachunguzwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Jeshi la Polisi, kuhusu kuhusishwa kwao na operesheni hiyo iliyotekelezwa kwa kukiuka haki za binadamu, na sakata la escrow lililohusisha uchotwaji wa Sh306 bilioni zilizokuwa Benki Kuu.

Wakichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wiki iliyopita, baadhi ya wabunge walihoji kitendo cha Ikulu kuwasafisha mawaziri wachache na kuwaacha wengine waliojiuzulu kisiasa kutokana na wizara zao kukumbwa na kashfa na kumtaka Waziri Mkuu atoe majibu wakati akifanya majumuisho ya mjadala.

RAIA WAPYA WAKUTWA NA NYARA ZA SERIKALI...!!!

 Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi.

POLISI mkoani Katavi imewakamata raia wapya watatu waliokuwa wakimbizi kutoka Burundi kwa kujihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo.

Watu hao walikamatwa na nyara za Serikali zenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 1.2. Nyara hizo za Serikali ni vipande vitatu vya meno ya tembo vikiwa sawa na jino moja la mnyama huyo vikiwa tayari kusafirishwa kwenda mjini Tabora.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi , Dhahiri Kidavashari amewataja watuhumiwa hao kuwa ni pamoja na Frank Hamis (18) , Steven Jonas (22) na Jackson Erasto ambao karibuni wamepewa uraia wa Tanzania. 

Kidavashari alibainisha kuwa watuhumiwa hao walikutwa juzi saa 3:00 asubuhi katika chumba alichopanga mwanafunzi wa kidato cha Nne katika shule ya sekondari Katumba, Ernest John (19) katika eneo la Mnyasi kijijini Katumba wilayani Mlele. 

“Mwanafunzi huyo ana uhusiano nao wa kindugu hivyo aliwakaribisha kulala chumbani kwake alimokuwa amepanga katika nyumba ambayo ni mali ya Felix Gado iliyopo eneo la Mnyasi kijijini Katumba.

GIZA NENE MAKADA URAIS CCM

Katibu mwenezi CCM Nape Nnauye.

Hali bado ni tete kwa makada sita waliofungiwa na CCM kujihusisha na masuala ya uchaguzi baada ya chama hicho tawala kueleza kuwa mchakato wa kuwachunguza haujakamilika na adhabu yao inaweza kuendelea hata baada ya vikao vya juu vitakavyofanyika mwishoni mwa wiki.

CCM pia imebadili tarehe za vikao vya Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ambavyo awali vilipangwa kufanyika Mei 20, 21 na 22 na badala yake sasa vitafanyika Mei 22,23 na 24.

Akizungumza na waandishi wa habari jana kwenye ofisi za chama hicho jijini, Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hafahamu lini adhabu ya viongozi hao itakwisha kwani bado mchakato wa kuwachunguza haujafika mwisho.

Wednesday, May 13, 2015

RAIS NKURUNZIZA APINDULIWA...!!!

Meja Jenerali Godefroid Niyombareh amewaambia waandishi wa habari mjini Bujumubura, kuwa kumeundwa kamati maalum ya kuiokoa Burundi
Raia wa Bujumbura wakishanilia tangazo la generali Niyombareh

Meja Generali Niyombareh amesema wamechukua hatua hiyo baada ya watu wa Burundi kukataa kwa kinywa kipana awamu ya tatu ya urais wa Nkurunziza.
Jenerali huyo aliyetimuliwa na Nkurunziza mwezi februari anasema kuwa Nkurunziza alishindwa kuheshimu mwafaka wa amani mbali na sheria za kimataifa.

Polisi wameamrishwa kuondoka mabarabarani

Jenerali Niyombareh alikuwa ameandamana na viongozi wengine wa jeshi la Burundi.
Tayari wanajeshi wameshika doria nje ya makao makuu ya runinga ya taifa.
 
Maafisa wa polisi wamekuwa wakipambana na waandamanaji wanaopinga hatua ya Rais Nkurunzinza kuwania awamu ya tatu

JACQUELINE WOLPER: ANAETOKA NA NAY WA MITEGO AMESHAJULIKANA

Jacqueline Wolper

Muigizaji wa filamu zabkibongo, Jacqueline Wolper amewaweka njiapanda mashabiki wake kwa kaul yake kuwa msichana aliye katika uhusiano wa kimapenzi na msanii wa bongo flava Emmanuel Elibariki 'Nay wa Mitego' amekwishafahamika tofauti na alivyokuwa akihisiwa yeye.

 "Watu hawana dogo, ukiwa na ukaribu na mtu unaambiwa ni mpenzi wako, Nay hakuwahi kuwa mpenzi wangu kwa kuwa ni zaidi ya rafiki kwangu, ila watu wasio waelewa ndiyo waliokuwa wakivumisha kuwa tuna uhusiano kwa maslahi yao, lakini sasa ukweli umejulikana kama mnavyoona na mnavyosikia Nay ni wa nani" alieleza Jacqueline bila kuweka wazi ni nani anatoka na mwana hip hop huyo.

 Wolper aliongeza kuwa taarifa hizo ziliposanbaa alipata tabu ambapo alitumia muda mwingi kutolea maelezo kwa watu wake wa karibu.




BARCELONA YATINGA FAINALI

Messi, Suarez na Neymar wakishangilia bao

Miamba ya soka Hispania, Barcelona wamefanikiwa kutinga fainali baada ya kuibwaga Bayern Munich kwa jumla ya mabao 5-3 waliyokusanya katika mikondo yote miwili waliyokutana katika hatua ya nusu fainali.
 Katika mchezo wa usiku wa kuamkia leo ambao ulipigwa katika dimba la Allinza Arena, Bayern walipaswa kushinda bao nne bila ili wapate tiketi ya kusonga mbele.
 Lakini mpaka kipyenga kinapulizwa the Bavarian 3,Barcelona wakajipatia mabao mawili.
 Leo usiku kutakuwa na mchezo kati ya Real Madrid dhidi ya Juventus katika dimba la Banabeu.

NGASSA ASAINI KUCHEZA AFRIKA KUSINI

Mrisho Ngassa

 Mshambuliaji hodari wa timu ya Yanga, Mrisho Ngassa amemwaga wino wa kuichezea timu ya Free State Stars ya ligi kuu Afrika Kusini kwa miaka minne.

 Ngassa ameripotiwa kufurahia mkataba huo mnono na kuanza maisha yake mapya baada ya kucheza nyumbani kwa miaka kadhaa.

"Nataka kuitumia fursa hii kutangaza soka la Tanzania na nitajituma ili kufanya vizuri zaidi" alisema mchezaji huyo.

Katika mitandao mbalimbali ya kijamii Ngassa ameonekana akiwa na kocha wa timu hiyo mara baada ya kusaini mkataba.


Friday, May 01, 2015

UKAWA WAKUNA VICHWA SAA 48

 
Mwenyekiti  mwenza wa Ukawa, Freeman Mbowe akizungumza wakati wa mkutano na waandishi  wa habari, Dar es Salaam jana. Wengine ni wenyeviti wenza, James Mbati,  Profesa Ibrahim Lipumba na  Dk Emmanuel Makaidi.

Saa 48 zilizotumika kikaoni kutafuta muafaka wa majimbo yenye utata ndani ya umoja wa vyama vya upinzani vilivyo chini ya Ukawa, zimekatika bila mafanikio na  mvutano unaonekana kubakia kwenye majimbo 12 kati ya 239 waliyopanga kugawana.

Vyama hivyo vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi vimekubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia kiti cha urais hadi udiwani, lakini kazi ya kugawana majimbo imekuwa ikivisumbua na ilitarajiwa kuwa ingemalizika juzi baada ya viongozi kukutana kwa siku mbili kuanzia Jumanne.
Lakini habari kutoka ndani ya kikao hicho kilichofanyika jijini Dar es Salaam zinaeleza kuwa wajumbe walishindwa kufikia muafaka kwenye majimbo 12.

Hata hivyo, viongozi hao wa vyama hivyo walikataa kutaja majimbo hayo yaliyosalia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 01, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC02005
DSC02006
DSC02007 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SUMATRA KIINI CHA AJALI BARABARANI...!!!

Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta

WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema ajali za barabarani zinachangiwa na uzembe wa taasisi inayosimamia sekta ya usafiri jambo linalogharimu maisha ya watu wasio na hatia, na kuitaka taasisi hiyo kuchukua hatua na kuhakikisha nidhamu inarejea kwenye sekta hiyo.

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ndiyo yenye dhamana ya kusimamia na udhibiti wa sekta ya usafiri katika nchi kavu na majini.

Sitta aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari wakati Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipokuwa ikizungumza na viongozi wa wizara hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BAN KI-MOON ASIKITISHWA NA MAPIGANO YEMEN

 Ban Ki-moon
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea tahadhari yake kuhusiana na hatari ya raia kuendelea kupigana, Nchini Yemen. Anasema kuwa zaidi ya watu elfu moja mia tano wameuwawa na wengine laki tatu wametoroka makazi yao, katika kipindi cha majuma sita yaliyopita.

Mashambulizi katika majumba ya raia zikiwemo hosptali na maghala ya vifaa vya misaa ya kibinadamu yamekuwa yakiendelea.
Mapigano Yemen
Kumekuwa na taarifa watu wenye silaha wamekuwa wakiwateka raia katika mitaa ya Aden.
Shirika la Umoja wa mataifa la misaada ya chakula limesema halina jinsi zaidi ya kusitisha mipango yake ya kusambaza misaada kutoka na tatizo la mafuta.

Kwa sasa mapigano makali yanaendelea katika mipaka ya eneo la Yemen na Saudia Arabia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAANDAMANO MAPYA BALTIMORE MAREKANI


Kumetokea maandamano mapya nchini Marekani katika mji wa Baltimore kufuatia kifo cha kijana mweusi Freddie Gray aliyekufa kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi. Mamia ya watu wameandamana katika mitaa, wakionyesha ujasiri licha ya hali mbaya ya hewa iliyokuwepo.

Matokeo ya mwanzo ya uchunguzi wa polisi wa jinsi kijana wa miaka ishirini na mitano mwenye asili ya weusi alivyouawa bado hayajawekwa hadharani.

Maandamano Baltimore
 
Mtetezi wa haki za binadamu, Mchungaji Al Sharpton, ameitisha mkutano mjini Baltimore ili kuimarisha uhusiano baina ya polisi na wanajamii. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

YANGA INA MATUMAINI YA USHINDI

 
Kocha mkuu wa Yanga Hans Pluijm.
 
Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm amesema wana ari ya kushinda mechi yao ya mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Etoile du Sahel licha ya kuwaacha wachezaji wake tegemezi katika msafara wao wa Tunisia.

Yanga imeondoka Dar es Salaam Jumatano usiku huku wachezaji wake tegemezi, wakiwemo Hassan Dilunga, Salum Telela na Danny Mrwanda, aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini Vietnam wakiachwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kifamilia. “Yanga imesajili zaidi ya wachezaji 20, wote ni muhimu katika timu”.

“Ni kweli niliwahitaji katika mechi yetu ngumu dhidi ya Etoile, lakini sababu mbalimbali zimepelekea kuachwa kwao”, amesema Pluijm. Yanga itacheza na wenyeji wao, Etoile du Sahel katika mechi ya marudiano ya raundi ya 16 bora ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Katika mechi iliyochezwa wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, Yanga ililazimishwa sare ya 1-1 hivyo kuwa na kibarua kigumu cha kushinda ugenini huku wenyeji wao wakililia sare ili kucheza hatua inayofuata. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TAZAMA PICHA ZA YANGA WAKIWA KATIKA MAZOEZI NCHINI TUNIS

IMG-20150501-WA0002
Katika mazoezi ya jana usiku kocha mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amewaambia vijana wake kujiamini na kucheza soka la kushambulia ili kufunga magoli ya mapema  na kuwachanganya Etoile du Sahel katika mechi ya leo usiku kuanzia majira ya saa 3:00 usiku kwa saa za Tanzania.
Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro naye kama kawaida yupo Tunisia kufuatilia mambo yanavyokwenda. Yanga wanahitaji ushindi au sare ya angalau magoli 2-2 ili kusonga mbele moja kwa moja kwasababu mechi ya kwanza jijini Dar es salaam timu hizi zilitoka sare ya 1-1.
Maelekezo ya hapa na pale kabla ya kuanza mazoezi.
Mrisho Ngassa (kushoto) na Simon Msuva (kulia) wanatarajia kuongoza safu ya ushambuliaji leo
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BEN DAVIES APASULIWA BEGA

 
timu ya Wales 
 
Beki wa kulia wa Tottenham Ben Davies ameenguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Wales baada ya kufanyiwa upasuji wa bega. Mlinzi huyu aliumia wakati wa mchezo wa ligi kati ya timu yake na Southampton uliofanyika wiki iliyopita.

Davies hatojumuika na wenzake katika mchezo wa kuwania kuzufu kwa michuno ya ulaya ya mwaka2016. Ambapo Wales watakua na mchezo dhidi ya Ubelgiji , tayari kocha wa timu hiyo Chriss Coleman amemuita kikosini beki wa Swansea City's Neil Taylor kuziba pengo hilo.

Hii inasababisha mchezaji huyu kukosa michezo iliyobaki ya ligi ya England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...