Friday, May 01, 2015

BAN KI-MOON ASIKITISHWA NA MAPIGANO YEMEN

 Ban Ki-moon
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea tahadhari yake kuhusiana na hatari ya raia kuendelea kupigana, Nchini Yemen. Anasema kuwa zaidi ya watu elfu moja mia tano wameuwawa na wengine laki tatu wametoroka makazi yao, katika kipindi cha majuma sita yaliyopita.

Mashambulizi katika majumba ya raia zikiwemo hosptali na maghala ya vifaa vya misaa ya kibinadamu yamekuwa yakiendelea.
Mapigano Yemen
Kumekuwa na taarifa watu wenye silaha wamekuwa wakiwateka raia katika mitaa ya Aden.
Shirika la Umoja wa mataifa la misaada ya chakula limesema halina jinsi zaidi ya kusitisha mipango yake ya kusambaza misaada kutoka na tatizo la mafuta.

Kwa sasa mapigano makali yanaendelea katika mipaka ya eneo la Yemen na Saudia Arabia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...