Friday, May 01, 2015

SUMATRA KIINI CHA AJALI BARABARANI...!!!

Waziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta

WAZIRI wa Uchukuzi, Samuel Sitta amesema ajali za barabarani zinachangiwa na uzembe wa taasisi inayosimamia sekta ya usafiri jambo linalogharimu maisha ya watu wasio na hatia, na kuitaka taasisi hiyo kuchukua hatua na kuhakikisha nidhamu inarejea kwenye sekta hiyo.

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) ndiyo yenye dhamana ya kusimamia na udhibiti wa sekta ya usafiri katika nchi kavu na majini.

Sitta aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari wakati Kamati ya Bunge ya Miundombinu ilipokuwa ikizungumza na viongozi wa wizara hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
Sitta alisema “Hakuna kitu kinachoniuma kama ajali za barabarani ambazo nyingi zinasababishwa na uzembe, ubovu wa magari na matairi ya mtumba, halafu baya zaidi ni kwamba Mamlaka husika ya kudhibiti vyombo hivyo ipo, inaona na kuwasamehe makosa,” alisema Sitta.

Aliongeza, mamlaka husika zina wajibu wa kusimamia vyombo hivyo na kuhakikisha vile vinavyofanya makosa vinachukuliwa hatua ikiwa ni pamoja na kuvifutia leseni, kwani matukio mengi ya ajali yanatokana na uzembe na kuanzia sasa masuala ya msamaha yasiwepo.

“Hatuwezi kuendelea kuona wananchi wanakufa tu, kwa sababu ya uzembe wa madereva au wamiliki, nilizungumza na baadhi ya wamiliki wanasema hawawezi kununua matairi mapya, kwa sababu ya gharama, wanatumia matairi ya mtumba, sasa jambo hili sio sahihi, kama hawawezi kutoa huduma kwa kutumia vyombo vyenye viwango, waache, na sio kucheza na uhai wa watu,” alisisitiza Sitta.

Sitta aliongeza, wamiliki wa vyombo vya moto na madereva, wanapaswa kufuata sheria za barabarani na kuhakikisha wanazitii na kwamba vyombo hivyo vinapaswa kuwa na vipuri vyenye viwango na kuhakikisha mabasi yanayokwenda umbali zaidi ya kilometa 700, yawe na madereva wawili.

“Ipo sheria inayozungumzia umbali unaotakiwa dereva mmoja aendeshe gari, lakini pia nilizungumza na daktari kuhusu umbali unaokubalika kwa madereva kuendesha chombo cha moto, aliniambia dereva mmoja hatakiwi kuendesha gari kwa umbali wa zaidi ya kilometa 700, zaidi ya hapo inabidi wawe madereva wawili,” alisema Sitta.

Alisema hiyo inatokana na ukweli kwamba kwa umbali huo, wa kilometa 700 dereva huwa amechoka na akienda zaidi ya hapo anaweza kusababisha ajali kwa kuwa akili na mwili vimechoka hivyo hawezi kuwa makini barabarani.

Akizungumzia ubovu wa mabasi ya abiria na daladala, Sitta alisema magari yote mabovu, yanapaswa yasiwepo barabarani, kwani kuwepo kunachangia ajali kwa njia moja au nyingine. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Kuhusu mgomo, Sitta alisema nchi inaongozwa kwa sheria na kwamba sio kila kitu kinachofanywa na serikali ni masuala ya siasa, hivyo sio sahihi madereva na wamiliki wa mabasi kugoma kutoa huduma kwa abiria.

‘Huwezi kugoma kutoa huduma kwa abiria, halafu madereva wanatoa amri kwa serikali eti wanatoa siku kadhaa madai yao yatekelezwe, hii ni nchi inayoongozwa kwa sheria na sio vitisho, hawana haki ya kufanya hivyo, wanachotakiwa ni kufuata sheria,” alisema Sitta.

Alisema kama kuna madai ya stahiki za madereva na wamiliki wa vyombo hivyo, wanapaswa kupeleka madai yao sehemu husika na kwamba tatizo kubwa linaloonekana kwa watu hao ni usaliti wa wao kwa wao.

Alisema mfumo wa malalamiko upo na kwamba kama waliona uamuzi wa kushusha nauli sio sahihi, walipaswa kukata rufaa, jambo ambalo wamelifanya na kusubiri rufani yao ndani ya siku 14.

“Hii nchi inaongozwa na sheria, kama wamiliki waliona uamuzi wa kushusha nauli sio sahihi walipaswa kukata rufaa, jambo ambalo wamefanya na wasubiri uamuzi wa rufani yao ndani ya muda huo, na majibu ya rufani yanaweza kukubaliwa au kukataliwa,” alisema Sitta.

Aprili 15 mwaka huu serikali ilitangaza viwango vipya vya nauli ambavyo vilitarajiwa kuanza kutumika jana Aprili 30, mwaka huu kwa kushusha nauli za mabasi ya mikoani huku nauli za daladala zikibaki palepale. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...