Tuesday, November 18, 2014

VIONGOZI MANYARA, KITETO WAKALIA KUTI KAVU


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  akitoa kauli ya serikali bungeni jana, kuhusu mauaji ya wakulima na wafugaji wa Wilayani Kiteto, Mkoani Arusha.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema Serikali itafanya mabadiliko ya kiutawala katika ngazi mbalimbali Wilaya ya Kiteto na Mkoa wa Manyara wiki hii ili kuimarisha uongozi kukabiliana na mauaji ya wakulima na wafugaji yaliyosababisha vifo vya watu 17 tangu Januari 12 mwaka huu hadi sasa.

Pinda alisema hayo bungeni mjini Dodoma jana wakati akitoa taarifa kuhusu vurugu zinazoendelea Kiteto kati ya wafugaji na wakulima na kusababisha mauaji.

Alisema mabadiliko ya uongozi wa kiutawala katika eneo hilo ni moja ya hatua ambazo zinachukuliwa kitaifa nyingine zikiwa ni kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya kuondoa na kuepuka na kutatua migogoro inayojitokeza kwa njia ya amani. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KANALI AHUKUMIWA KUNYONGWA, CONGO

Waaandamaji wakipinga kuuawa kwa Kanal Ndala
Mahakama ya kijeshi Mashariki mwa Jamuhuri ya Demokrasi ya Congo imemhukumu kifo Kanali Birocho Nzanzu baada ya kubainika na makosa ya kutaka kumuua afisa wa jeshi la nchi hiyo aliyekuwa mstari wa mbele kutokomeza wapiganaji wa M23.
Kanal Mamadou Ndala anayedaiwa kuuawa na njama za Kanal Birocho Nzanzu
Afisa anayedaiwa kupangiwa njama za kuuawa ni Mamadou Ndala mabaye kwa kiasi kikubwa aliamini katika vita dhidi ya kundi hilo la wapiganaji na ambaye aliuawa mwezi januari mwaka huu. Hata hivyo hukumu hiyo imetolewa kwa watuhumiwa nane ambapo kati ya hao mmoja ndiye Kanali Ndala aliyehukumiwa kifo. Mahakama imebainisha kuwa Kanali Nzanzu amekuwa akitumiwa na waasi wa ADF kutoka Uganda kuandaa maujaji. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GAVANA ATANGAZA HALI YA HATARI, MISSOURI


Machafuko Missouri

Gavana wa jimbo la Missouri nchini Marekani ametangaza hali ya hatari kabla ya kutolewa uamuzi muhimu kuhusu kumfungulia mashitaka ya jinai au la dhidi ya afisa wa polisi mzungu, ambaye alimuua kwa kumpiga risasi kijana wa Kiafrika ambaye hakuwa na silaha.
Mauaji hayo yaliyotokea katika mji wa Ferguson mwezi Agosti yalisababisha vurugu katika mitaa kwa siku kadha na kuamsha mjadala kuhusu uhusiano kati ya polisi na jamii ya watu weusi nchini Marekani.
Idara ya polisi ya Kaunti ya St. Louis ndiyo wanaosimamia maandamano yoyote. Meya wa St. Louis, Francis. Slay, amezungumzia kuhusu tahadhari wanayochukua. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...