Wednesday, June 14, 2017

USHAHIDI WA KESI YA WEMA WAKWAMA KUTOLEWA

Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayomkabili Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi Julai 10.

Wema ambaye ni mshindi wa taji la urembo, maarufu Miss Tanzania kwa mwaka 2006 na msanii wa filamu, anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kutumia na kupatikana na bangi.

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa alisema kesi ilipangwa leo (Jumatano) kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka lakini Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayeisikiliza kesi hiyo yupo likizo.

Kutokana na hilo, aliomba iahirishwe hadi Julai 10 ombi lililokubaliwa na mahakama. Wema na wenzake Angelina Msigwa na Matrida Abbas wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na dawa za kulevya na kutumia dawa hizo.

Inadaiwa Februari 4, katika makazi ya Wema, Kunduchi Ununio, walikamatwa wakiwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08. Wema pia anadaiwa Februari Mosi katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam alitumia bangi.

MAGUFULI AFANYA MAZUNGUMZO NA ACACIA, WAKUBALI KULIPA FEDHA WANAZODAIWA NA PIA KUSAIDIA UJENZI WA MTAMBO WA KUCHENJULIA DHAHABU NCHINI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiagana Mhe. Ian Myles balozi wa Canada Nchini pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton alipofoika ikulu kwa mazungumzo juni 14,2017.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na  Mwenyekiti wa Barrick  Gold Corporation  Profesa John L. Thornton baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es salaam  Juni 14, 2017. wakiwa na  Waziri wa Sheria na Katiba Profesa Palamagamba Kabudi na Balozi wa Canada nchini Mhe. Ian Myles.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu ni kwamba, Prof. John L. Thornton ambaye amesafiri kwa ndege binafsi kutoka nchini Canada hadi Tanzania amekutana na Mhe. Rais Magufuli leo Juni 14, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam na mazungumzo yao yamehudhuriwa na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...