Sunday, March 03, 2013

CHADEMA WAENDELEZA WIMBI LA TIMUA TIMUA. HALI NI MBAYA SANA KUPITA MAELEZO


Chama cha Demokrasia na Maendeleo Mkoa wa Morogoro kimemfukuza uanachama ndugu Dazza na kuwarudishia uanachama wao wale wote waliokuwa wamefukuzwa uanachama na Kamati Tendaji ya wilaya. Maamuzi ya kuwarudishia uanachama wao wale waliofukuzwa na Kamati Tendaji ya Wilaya ya Morogoro Mjini ulitolewa na Baraza la Uongozi la Mkoa chini ya Mwenyekiti wake Mheshimiwa Susan Kiwanga Baada ya Baraza hilo kujiridhisha kuwa Kamati Tendaji ya Wilaya ilikiuka Katiba, Kanuni na taratibu za Chama ikiwa ni pamoja na kuwafukuza uanachama wanachama wapatao 15 pasipo kuwapa nafasi ya kusikilizwa na kujitetea.

Mmoja kati ya wahanga wa maamuzi hayo ya Kamati Tendaji ya wilaya ni Mbunge Kivuri wa CHADEMA jimbo la Morogoro mjini mheshimiwa Amani Mwaipaja ambaye pia ni mwanasheria na mmiliki wa Blog ya MWAIPAJA BLOG. wito wangu kwa CHADEMA Morogoro ni kwamba wakati wa kuendekeza siasa za chuki na majungu umepitwa na wakati. Watanxzania wa leo ni waelewa kuliko wanavyofikiri CCM. Fanyeni kazi.

KENYA WAENDELEZA UBABE WAO KILIMANJARO MARATHON 2013


Na Mroki Mroki-Father Kidevu Blog-Moshi
 
Wanariadha kutoka Nchini Kenya wameendeleza Umwambawao katika mbio za Nyika za Kilimanjaro ‘Kilimanjaro Marathon 2013’ zilizofanyika leo mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Wakenya walidhihirisha umwamba katika Mbio za Kilometa 42 baada ya Mkimbiaji wao Kipsang Kipkemoi kunyakua nafasi ya kwanza katika mbio hizo za mwaka huu upande wa wanaume na Wanawake ilinyakuliwa na Mwana dada Edna Joseph alebeba Medali ya Dhahabu.

Nafasi ya pili hadi ya tano kwa wanaume ni Julius Kilimo, Dominick Kiagor, Onesmo Maithiya Loshile Moikari ambapo upande wa wanawake ni Eunice Muchiri, Frida Too, Rosaline David na Jane Kenyara.
 
Jumla ya wakimbiaji 65000 walishiriki mbio za Kilimanjaro Marathon 2013.

TBL YATOA MSAADA WA MAGODORO 210, VYANDARUA 200 HOSPITALI MKOANI KILIMANJARO


Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), SteveKilindo (katikati), akimkabidhi Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Ibrahim Msengi msaada wa magodoro kwa ajili ya Hosptali ya Huruma ya wilayani Rombo pamoja na Kituo cha Afya cha Uru Kiaseni katika hafla iliyofanyika Mjini Moshi. Kulia kwake ni Mganga Mkuu wa mkoa huo, Dk. Mtumwa Mwako. Jumla ya magodoro 210 na vyandarua 200 vimetolewa na TBL kwa ajili ya kituo hicho na hospitali hiyo.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Ibrahim Msengi akikabidhi msaada wa magodoro kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Dk. Mtumwa Mwako baada ya kukabidhiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), mjini Moshi . Katikati ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa TBL, Steve Kilindo. Jumla ya magodoro 210 na vyandarua 200 vimlitolewa na TBL kwa ajili ya kituo Afya cha Uru Kiaseni na Hosptali ya Uhuruma .
Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL, Steve Kilindo,(katikati)wakifurahia jambo na kaimu mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dk Ibrahm Msengi (Kulia )pamoja na mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dk Mtumwa Mwako mara baada yaTBL kukabidhi msaada wa magodoro 210 na vyandarua 200 kwa kituo cha Afya cha Uru Kiaseni na hosptali ya Uhuruma .
Magodoro yaliyokabidhiwa na TBL kwa Hospitali mkoani Kilimanjaro

Kenya yatakiwa uchaguzi wa amani kudhidirisha ukomavu wa demokrasia

Wagombea wa uraisi nchini Kenya
Wakati harakati za kampeni za uchaguzi wa uraisi zinafikia ukingoni nchini Kenya, Marekani imewataka raia wa Kenya kufanya uchaguzi wa amani ili kumpata kiongozi mpya kwa amani.
Akizungumza kwa niaba ya serikali naibu msemaji wa serikali ya Marekani Patrick Ventrell ameongeza kuwa Kenya inapita katika kipindi cha muhimu na kihistoria na hivyo kuwasihi wagombea kuhakikisha wanaepuka kuwa sababisho la umwagaji damu kama uliowahi kutokea katika uchaguzi wa mwaka 2007.
Hata hivyo hali ya mvutano imeongezeka ambapo serikali ya Marekani imewataka wakenya kutumia fursa hiyo kudumisha ukomavu wa demokrasia na kutekeleza matakwa ya katiba mpya.
Msemaji huyo amesema kuwa ni matarajio ya wengi kuwa wakenya hawatajali jinsi,kabila,dini,eneo analotoka mgombea ili kuchagua bali bali watamchagua kiongozi bora kulingana na sifa stahiki.
Takribani raia elfu moja walipoteza maisha huku laki sita wakiyakimbia makazi yao katika machafuko yaliyotokea katika kipindi cha uchaguzi wa mwaka 2007.

DHARURA ZA KUOKOA ELIMU YA TANZANIA

images
MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE,
Kwa heshima kubwa, Chama cha NCCR-Mageuzi kinapenda kuwasilisha rasmi mapendekezo yake kwako yenye lengo la kuinusuru elimu ya Watanzania, kama ifuatavyo:
Utangulizi
Mheshimiwa Rais,
Sisi Chama cha NCCR-Mageuzi tumeguswa sana na hali isiyoridhisha ya ubora wa elimu katika Taifa letu la Tanzania. Hivyo tunaona ipo haja ya kuchukuliwa kwa hatua za dharura kuinusuru elimu, ili taifa lisiharibikiwe zaidi, badala yake kuwe na elimu yenye ubora wa hali ya juu na utimilifu wa malengo tuliyonayo kama taifa.
Mheshimiwa Rais,
Katika muktadha wa mapendekezo tunayoyaleta kwako, tunazingatia masuala ya kitaifa yafuatayo:-
(i) Tangu Taifa letu lipate uhuru wake mwaka 1961 (kwa Tanganyika) na mwaka 1964 (Mapinduzi ya Zanzibar) tulitambua umuhimu wa kufuta ujinga, kwa kuelimisha wananchi ili tujiletee maendeleo. Ingawa hadi sasa kazi kubwa imefanyika katika kukuza elimu hapa nchini, bado hatujafika katika hali ya kuwa na taifa ambalo karibu kila raia mwenye umri stahiki anajua kusoma na kuandika.
(ii) Katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025, tunataja pamoja na mambo mengine kwamba, ifikapo mwaka 2025 tuwe tumejenga taifa la watu walioelimika kwa upeo wa juu katika nyanja mbalimbali.
(iii) Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, ambao una malengo nane ya milenia; lengo la pili likiwa ni upatikanaji wa elimu bora kwa wote (achieving universal primary education)); na
(iv) Ifikapo mwaka 2015 (takribani miaka miwili toka sasa) tutalazimika kama taifa kupima utekelezaji wa malengo hayo ya milenia ili kuendana na viwango vya kimataifa.
Mheshimiwa Rais,
Wakati tukikabiliwa na malengo hayo ya Kitaifa, kwa muda mrefu kumekuwepo na viashiria vingi vinavyoonesha kwamba ubora wa elimu itolewayo hapa nchini katika ngazi zote hauridhishi. Viashiria hivyo ni pamoja na:-

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI TAREHE 03.03.2013 HAYA HAPA

l 001 c4e42

VAZI LA NUSU UCHI LAMTIA AIBU AUNT LULU

MSANII wa filamu asiyekaukiwa na skendo, Lulu Semagongo 'Anti Lulu' hivi karibuni alijikuta akiaibika kwenye onyesho la Bendi ya Extra Bongo baada ya kuvamia jukwaa na kuanza kucheza huku akizianika sehemu zake nyeti. 

Anti Lulu alikuwa ameongozana na mtangazaji Maimartha Jesse kwenye shoo hiyo iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Meeda, Sinza jijini Dar ambapo kila alipokuwa akicheza alikuwa akimwaga lazi kufuatia kigauni chake kifupi alichokuwa amevaa hivyo kuwafanya wanaume wakware wamkosekose kumfanyia kitu mbaya.
Katika tukio lingine, Maimartha naye alijikuta akipata aibu baada ya kunusurika kung’oa meno kufuatia viatu virefu alivyokuwa amevaa kumpiga mwereka ambapo kama siyo Lulu kumshika, tungekuwa tunazungumzia mambo mengine.
Licha kunusurika huko, Mai alionekana kutembea kwa shida sana kana kwamba alilazimishwa kuvaa viatu hivyo ambapo kuna wakati wanaume walimzomea hali iliyomfanya akose amani.

TFF YAIKOMALIA SERIKALI

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesema ipo haja kwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara kufikiria upya uamuzi wake wa kutengua usajili wa Katiba ya TFF ya mwaka 2012 na kutaka itumike ya mwaka 2006, kwani hautekelezeki.

Akizungumza na waandishi wa habari leo mchana, mara baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji, Rais wa TFF, Leodegar Tenga amesema ni muhimu jambo hilo likaangaliwa upya kwa sababu athari zake ni mbaya, na pengine Dk. Mukangara hakushauriwa vizuri kabla ya kufanya uamuzi huo.

“Kamati ya Utendaji ya TFF haitaki kubishana na Mheshimiwa Waziri hata kidogo, ila tunaamini wakati anatamka haya hakufahamu madhara yake, athari zake na ugumu wa utekelezaji wake. Kwa waliomshauri hili, wamemshauri vibaya,” amesema Rais Tenga.

Amesema rai ya TFF kwa Waziri ni kuwaita ili wamweleze ni kitu gani wafanye kunusuru mpira wa miguu wa Tanzania, kwani wanaamini jambo hili litakwisha baada ya kumwelimisha hasa kutokana na ukweli kuwa kabla ya kufanya uamuzi huo hakuwasikiliza.

Katika mkutano huo, Rais Tenga alianza kwa kusema kuwa TFF inaiheshimu sana Serikali, hivyo inaheshimu maagizo yaliyotolewa na Waziri, lakini akaongeza kuwa TFF ina wajibu wa kutoa ufafanuzi juu ya maagizo hayo.

Amesema lengo la kuelezea historia ya TFF ilikotoka ni kubaini migongano ya maagizo hayo na taratibu za TFF ambazo kwa bahati mbaya zinasigana na maagizo hayo.

Rais Tenga amesema TFF ni chombo cha wanachama, ambapo wanachama wake ni vyama vya mikoa, vyama shiriki na klabu za Ligi Kuu, na ina taratibu za kufanya uamuzi kwa mujibu wa Katiba yake na za wanachama wake ambazo zimeidhinishwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema si TFF pekee, bali vyama vya nchi zote ambavyo vimeunganishwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), zinaheshimu na kufuata maagizo na miongozi ya shirikisho hilo la kimataifa la mpira wa miguu.

Rais Tenga amesema TFF haitakiwi kuingiliwa katika uongozi na uendeshaji wake, kwani jambo hilo likitokea rungu la FIFA litaiangukia TFF, na madhara yake ni makubwa. Miongozo ya FIFA inasisitiza uhuru wa wanachama wake katika uendeshaji shughuli za mpira wa miguu, na iko kwenye Katiba ya TFF.

“Sheria za nchi ndizo zilizozaa Katiba ya TFF. TFF ni chama kamili kinatakiwa kufanya uamuzi wake ili mradi uzingatie madhumuni ya kuanzishwa kwake. Leo TFF ikiacha mpira wa miguu na kuanza kujishughulisha na gofu, hapo Msajili ana haki ya kuingilia,” amesema Rais Tenga.

SIMBA NDANI YA ANGOLA TAYARI KUPAMBANA NA LIBOLO


Baadhi ya wachezaji wa Simba wakiwa wamepozi nje ya Hotel Ritz na mchambuzi wa soka Edo Kumwembe huko Angola tayari kwa kupambana na Libolo siku ya leo katika mechi ya pili ya Mabingwa wa Afrika.

Tume ya Wajumbe 15 iliyoundwa na Waziri Mkuu ya kuchunguza Matokeo CSEE 2012 hii hapa.


Waziri Mkuu, Mizengo Pinda jana Jumamosi, Machi 2, 2013 amezindua Tume maalum aliyoiunda ili ifanye uchunguzi wa matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyotangazwa Februari 18, mwaka huu na kuwataka wajumbe wa Tume hiyo watafute kiini cha mserereko wa kushuka kwa ufaulu kuanzia mwaka 2010 hadi 2012.
Waziri Mkuu amezungumza na wajumbe wa Tume hiyo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni, jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk  Shukuru Kawambwa. 
Amesema kwa  mujibu wa hadidu za rejea, wajumbe wa tume hiyo watatakiwa kuangalia ni sababu zipi zimechangia kuwepo kwa matokeo hayo mabaya, mserereko wa kushuka umekuwa ukiongezeka kwa sababu gani, usimamizi katika Halmashauri ukoje, ukaguzi wa elimu na uhamishiwaji wa sekta ya elimu kwenye Wizara ya TAMISEMi umechangiaje kushuka kwa kiwango cha ufaulu.
Vilevile, watatakiwa kuangalia mitaala na mihutasari ikoje, kuangalia uwiano uliopo kwenye mitihani inayotungwa ikiwa ni pamoja na uhakiki wa mitihani hiyo; kuangalia mazingira ya kufundishia, mfumo wa upimaji, usimamizi na uendeshaji, na kutokuwepo kwa chakula shuleni kunachangiaje kushuka kwa utendaji mbaya wa wanafunzi katika masomo yao.
Tume hiyo yenye wajumbe 15, imepewa muda wa wiki sita kuanzia Machi mosi iwe imekamilisha kazi hiyo na kuwasilisha taarifa yao kwa Waziri Mkuu. 
Tume itaongozwa na Prof. Sifuni Mchome wa Tume ya Vyuo Vikuu, na Makamu wake atakuwa Bi. Bernadetha Mushashu (Mbunge wa Viti Maalum – Kagera).
Wajumbe ni Bw. James Mbatia (Mbunge wa kuteuliwa), Bw. Abdul J. Marombwa (Mbunge wa Kibiti), Prof. Mwajabu Possi (Chuo Kikuu – UDSM), Bibi Honoratha Chitanda (CWT), Bibi Daina Matemu (TAHOSSA) na Bw. Mahmoud Mringo (TAMONGSCO).
Wangine ni Bw. Rakhesh Rajani (TWAWEZA), Bw. Peter Maduki (CSSC), Mwl. Nurdin Mohamed (BAKWATA), Bw. Suleiman Hemed Khamis (Baraza la Wawakilishi, Zanzibar), Bw. Abdalla Hemed Mohamed (Chuo Kikuu – SUZA), Bw. Mabrouk Jabu Makame (Baraza la Elimu Zanzibar na Bw. Kizito Lawa (Taasisi ya Kukuza Mitaala).

Mkutano wa CUF Jimbo la Kwamtipura mjini Zanzibar


Mwakilishi wa Mji Mkongwe ambae pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CUF Ismail Jusa Ladu wakushoto akiwa na Mkurugenzi wa Habari,Uwenezi na Mawasiliano ya Umma wa CUF Salum Abdallah Bimani wakisikiliza kwa makini risala ya vijana wa jimbo la Kwamtipura katika mkutano wa hazara uliofanyika katika kiwanja cha mpira kwamtipura.
Wananchi wa Jimbo la Kwamtipura wakisikiliza kwa makini hutuba ya Mwakilishi wa Mji Mkongwe ambae pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CUF Ismail Jusa Ladu hayupo pichani katika Mkutano wa hazara uliofanyika huko ktk kiwanja cha mpira kwamtipira
Mwakilishi wa Mji Mkongwe ambae pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Taifa la CUF Ismail Jusa Ladu akihutubia wananchi wa Jimbo la Kwamtipura katika Mkutano wa hazara uliofanyika ktk kiwanja cha mpira kwamtipira.(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar). 

Makamu wa Rais Dkt. Bilal Kufungua Miradi ya Maendeleo ya Ujenzi Mkoani Mara.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal atakuwa Mgeni Rasmi katika sherehe za uzinduzi wa  Miradi ya  Maendeleo inayotekelezwa na Wizara ya Ujenzi kuanzia tarehe  04/03/2013 mkoani Mara.
Pamoja na shughuli nyingine, siku ya  Jumatatu tarehe 04 Machi 2013 akiwa mkoani humo, Mhe. Makamu wa Rais  ataweka  jiwe la msingi kwa ajili ya  ukarabati wa barabara ya kutoka mpakani mwa Mkoa wa Simiyu na Mara hadi  Musoma yenye urefu wa kilomita 85.5.  Barabara ambayo ujenzi wake utawekewa jiwe la msingi ni sehemu ya Barabara ya Mwanza – Nyanguge – Makutano – Musoma ambayo ni kiungo muhimu  na nchi jirani za Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.  Hivyo kukamilika kwake ni fursa nyingine nzuri ya kuibua uchumi wa nchi yetu na ukanda huu.
Jumanne ya tarehe 5 Machi 2013 asubuhi Mhe. Makamu wa Rais atazindua Kivuko cha Musoma kinachotoa huduma kati ya Musoma na Kinesi.  Siku hiyo hiyo mchana Makamu wa Rais ataweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa Nyumba za Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) zilizoko eneo la Old Customs katika barabara ya Lake Side, Musoma.
Uzinduzi wa miradi hii ni utekelezaji wa azma ya Serikali ya Awamu ya nne ya kuboresha miundombinu muhimu ya usafiri na makazi kwa wananchi wake. Aidha, uzinduzi  wa Kivuko cha Musoma (MV Musoma) kinachotoa huduma kati ya Manispaa ya Musoma na Kinesi Wilayani Rorya ni utekelezaji wa ahadi za Mheshimiwa Rais baada ya kupokea ombi la Kivuko kutoka kwa wakazi wa Musoma na vitongoji vyake.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...