Sunday, March 03, 2013

DHARURA ZA KUOKOA ELIMU YA TANZANIA

images
MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,
DK. JAKAYA MRISHO KIKWETE,
Kwa heshima kubwa, Chama cha NCCR-Mageuzi kinapenda kuwasilisha rasmi mapendekezo yake kwako yenye lengo la kuinusuru elimu ya Watanzania, kama ifuatavyo:
Utangulizi
Mheshimiwa Rais,
Sisi Chama cha NCCR-Mageuzi tumeguswa sana na hali isiyoridhisha ya ubora wa elimu katika Taifa letu la Tanzania. Hivyo tunaona ipo haja ya kuchukuliwa kwa hatua za dharura kuinusuru elimu, ili taifa lisiharibikiwe zaidi, badala yake kuwe na elimu yenye ubora wa hali ya juu na utimilifu wa malengo tuliyonayo kama taifa.
Mheshimiwa Rais,
Katika muktadha wa mapendekezo tunayoyaleta kwako, tunazingatia masuala ya kitaifa yafuatayo:-
(i) Tangu Taifa letu lipate uhuru wake mwaka 1961 (kwa Tanganyika) na mwaka 1964 (Mapinduzi ya Zanzibar) tulitambua umuhimu wa kufuta ujinga, kwa kuelimisha wananchi ili tujiletee maendeleo. Ingawa hadi sasa kazi kubwa imefanyika katika kukuza elimu hapa nchini, bado hatujafika katika hali ya kuwa na taifa ambalo karibu kila raia mwenye umri stahiki anajua kusoma na kuandika.
(ii) Katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025, tunataja pamoja na mambo mengine kwamba, ifikapo mwaka 2025 tuwe tumejenga taifa la watu walioelimika kwa upeo wa juu katika nyanja mbalimbali.
(iii) Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, ambao una malengo nane ya milenia; lengo la pili likiwa ni upatikanaji wa elimu bora kwa wote (achieving universal primary education)); na
(iv) Ifikapo mwaka 2015 (takribani miaka miwili toka sasa) tutalazimika kama taifa kupima utekelezaji wa malengo hayo ya milenia ili kuendana na viwango vya kimataifa.
Mheshimiwa Rais,
Wakati tukikabiliwa na malengo hayo ya Kitaifa, kwa muda mrefu kumekuwepo na viashiria vingi vinavyoonesha kwamba ubora wa elimu itolewayo hapa nchini katika ngazi zote hauridhishi. Viashiria hivyo ni pamoja na:-

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...