Monday, April 08, 2013

UWOYA, DIAMOND WANASWA HOTELINI!

Diamond na Uwoya, walifanya jitihada za hali ya juu kuuficha ukweli kuhusu uhusiano wao lakini ilipofika Machi 25, mwaka huu, walinaswa na kamera za Global kwenye hoteli moja yenye hadhi ya nyota tano, iliyopo Mbezi Beach, Dar es Salaam.
The Biggest IQ, Ijumaa Wikienda, linathubutu kwa kuwa lina ushahidi wa kutosha kutamka kwamba Diamond na Uwoya, walilala kwenye hoteli hiyo, chumba namba 208, waliingia saa 8:24 usiku kisha wakatoka kati ya saa 9:00 na saa 9:13 mchana.

Tigo yawekeza kuunganisha watu wa vijijini na kuboresha huduma zake.


Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mh. Charles Bishuli akihutubia wananchi wa wilaya ya Kasulu kwenye sherehe za uzinduzi wa minara. Kulia kwake  Meneja wa Kanda ya ziwa Bw Joseph Mutalemwa na  Meneja wa Tigo wa mkoa wa Kigoma Bw Gamu Kimoro.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mh. Charles Bishuli akitaka utepe kuzindua mnara ya TIGO katika kata ya Muyama wilayani Buhigwe. Kulia kwake Meneja wa kanda ya ziwa Bw. Joseph Mutalemwa.

Waziri Mkuu wa Kwanza mwanamke nchini Uingereza Baroness Thatcher afariki dunia.


Waziri mkuu wa zamani nchini Uingereza Bibi Margret Thatcher amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 87 baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi.
Thatcher aliyekuwa mwanake wa kwanza kushika wadhfa huo, alikuwa alitokea chama cha Conservative na kuongoza nchi hiyo tangu mwaka 1979 hadi 1990.
Waziri Mkuu wa sasa nchini humo Bw. David Cameron ameelezea masikitiko yake na kumuita mwana mama huyo kuwa mjasiri wa Uingereza.
Naye Malkia Elizabeth wa II wa nchi hiyo hakusita kueleza kushitushwa na habari za kifo hicho huku akisema kimemhuzunisha lakini heshima ya kiongozi huyo itabaki palepale.
Kwa mujibu wa taarifa kiongozi huyo hatazikwa kwa mazishi ya kitaifa lakini atazikwa kwa hadhi sawa na Princes Diana nay a Mama wa Malkia.
Waziri Mkuu wa Uingereza Bw.  Cameron ambaye yuko ziarani nchini Hispania kwa ajili ya mikutano, amelazimika kukatisha ratiba ya mazungumzo yake na rais wa Ufaransa Francois Hollande na kurejea nyumbani.
Lady Thatcher kama alivyokuwa akijulikana alizaliwa akiitwa Margaret Roberts na kuhudumu kama mbunge wa Finchley –London Kaskazini tangu mwaka 1959 hadi 1992.

ANGALIA TUKIO LA WACHAWI WAWILI WALIODONDOKA NA UNGO HUKO KAHAMA- SHINYANGA...

WAZEE WANAOSADIIWA KUWA NI WACHAWI WAKIWA CHINI YA ULINZI KITUO CHA POLISI,KUTOKA KUSHOTO NI MWAJUMA MPONI (70) NA KULIA NI SHIJA NKWABI (80)

Watu wawili wamenusurika kuuwawa usiku wa kuamkia juzi katika kijiji cha Mhongolo wilaya ya kahama mkoani shinyanga, baada ya kukutwa katika mazingira yanayodaiwa kuwa ya kishirikina. 

Watu hao waliojitambulisha kwa majina ya Mwajuma Mponi (70) wa Nduku, na Shija Nkwabi(80) wa Nyashimbi wilayani humo, wameanguka kijijini hapo wakitokea kijiji cha nduku wiyani humo wakielekea Nyihogo Kahama kwa shughuli za kishirikina.

Katika maelezo yao wazee hao wamedai  kuwa wameanguka baada ya kutokea ajali ya kishirikina huko angani, ambapo waligongana na wenzao ambao hawakuwafahamu walikotoka na walikokuwa wanaelekea.

Chadema kuwasha moto bungeni, ni kuhusu wanachodai 'utendaji usiofaa' wa Bunge.

Wakati Bunge la 11 la Bajeti kwa mwaka huu likianza kesho, Kamati Kuu ya Chadema imesema itatumia Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kulibana Bunge kuhusu utendaji usiofuata Kanuni za Bunge unaofanywa na Spika na wasaidizi wake.
 
Pia wabunge hao wameitaka Serikali kuweka wazi mikataba iliyoingia hivi karibuni na Serikali ya China ili wananchi waweze kufahamu kilichomo vinginevyo watatumia kambi hiyo kuwabana wahusika.


Katika kikao cha 10 kilichomalizika Februari 8, mwaka huu mjini Dodoma, Mnadhimu wa kambi hiyo, Tundu Lissu alisema kuwa wanaandaa hoja za kumng’oa Spika na Naibu wake, Job Ndugai kwa kile walichodai kukiuka kanuni mbalimbali za Bunge.

Kambi ya upinzani ilikuwa ikilalamika kuondolewa kwa hoja binafsi za baadhi ya wabunge wao ikiwemo ya Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (Maji), James Mbatia (Mitalaa ya Elimu) na Joshua Nassari, ambaye hoja yake ilihusu utendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA).

Hata hivyo, Spika wa Bunge, Anne Makinda wakati akiahirisha kikao cha 10, alisema kuwa hoja binafsi zitakuja tena katika kikao cha 11 na wenye hoja watazifufua.

Jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika alisema Kamati Kuu ilibaini kwamba matukio yaliyotokea katika kikao 10 yalitokana na meza ya spika kutofuata kanuni.

MKAPA AWATAKA VIONGOZI WAFUATE MISINGI YA NYERERE

Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa amesifia utawala wake kwa kuongoza taifa bila ya kubaguana na amesikitishwa na matukio ya udini, ambayo yanaashiria kuvuruga amani na utulivu wa Tanzania katika siku za karibuni.
Akitoa salamu zake baada ya kusimikwa kwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Desdelius Rwoma, Mkapa alisema anachojivunia ni kuheshimiwa na waumini wa
madhehebu yote.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 9 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
 
.
.
.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...