Monday, April 08, 2013

Tigo yawekeza kuunganisha watu wa vijijini na kuboresha huduma zake.


Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mh. Charles Bishuli akihutubia wananchi wa wilaya ya Kasulu kwenye sherehe za uzinduzi wa minara. Kulia kwake  Meneja wa Kanda ya ziwa Bw Joseph Mutalemwa na  Meneja wa Tigo wa mkoa wa Kigoma Bw Gamu Kimoro.
Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mh. Charles Bishuli akitaka utepe kuzindua mnara ya TIGO katika kata ya Muyama wilayani Buhigwe. Kulia kwake Meneja wa kanda ya ziwa Bw. Joseph Mutalemwa.

Mkuu wa wilaya Buhigwe Mh Charles Bishuli akikabidhi vitabu 1,000 vya sayansi kutoka  kampuni ya simu za mkononi TIGO,  kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Nyaminkunga Bw Hamisi Bunoge.
Tigo Tanzania leo wametangaza mipango yao ya kuwekeza katika upanuzi wa mtandao wake ili kuongeza kiwango cha ubora na upatikanaji wa mtandao huo nchini kote. Upanuzi huo pia utakwenda sambamba na kujenga miundombinu mipya ya mawasiliano hasa katika maeneo ya vijijini, kuleta mawasiliano kwa maelfu ya watu. Minara mipya ya mawasiliano itajengwa nchi nzima ambapo mradi huo utaanzia katika maeneo kama Mwanza, Tabora, Kigoma, Mara na Kagera.
Kwa kuanzia mkoa wa Kigoma Tigo imeboresha mtandao kwaku zindua minara mitatu (3) katika Tarafa ya Mwandiga wilaya ya Kigoma vijijini,Kata ya Muyama wiliaya mpya ya Buhigwe na Kazuramimba wilaya ya Uvinza.
 Akizindua Minara hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mh. Issa Mashibya ,Mkuu wa Wilaya ya Buhigwe Mh.Charles Gishuli alisema Uzinduzi wa minara hii mipya wa mawasiliano hapa leo hii itatuwezesha kutumia mtandao wa Tigo kwa kutoa mawasiliano yenye ubora wa hali ya juu hivyo kufurahia zaidi mawasiliano ya simu zetu za mkononi. Matumaini na imani yangu kuwa, hii ni mojawapo ya mambo mengi mazuri kutoka Tigo na ninatarajia mambo mengine makubwa na mazuri zaidi kuja kupitia mtandao huu kwa siku zijazo.
Akitangaza mradi huo, kwa niaba ya Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania, Meneja wa Kanda ya Ziwa Bw. Joseph Mutalemwa alisema “Tigo Tanzania imeendelea kukua kwa kasi mwaka hadi mwaka. Bidhaa zetu za kipekee na huduma pamoja na kuongezeka kwa wateja ni ushahidi wa wazi kabisa wa kukua kwetu. Uzinduzi wa minara hii mipya utawezesha kuwapatia wateja wetu bidhaa bora za kipekee zilizobuniwa katika ubora wa hali ya juu ili wateja wetu waweze kunufaika na huduma na bidhaa zenye kiwango cha hali ya juu kabisa kwa hatua mpya. Hii ndio dhamira yetu ambayo imetufanya tuendelee kuwa kampuni inayoongoza ya mtandao wa simu za mkononi Tanzania.”
Kwa kanda ya Ziwa Tigo ina mpango wa kuboresha minara 141 hadi kufikia mwezi septemba ambapo tayari minara 17 imeshawaka, kati ya hii 17, mitatu (3)  ndiyo iliyozinduliwa Kigoma na lengo kubwa nikuwasha minara 24 kwa mkoa  wa Kigoma.
Tukiwa tayari na mtandao imara wa mawasiliano katika mikoa mingi ya Tanzania bara na Zanzibar, upanuzi huu wa mtandao wetu unalenga kuhakikisha kuwa mtandao wetu unapatikana katika mikoa mingi zaidi nchini. Itaboresha ubora wa mtandao katika maeneo ambayo tayari yana mtandao wa Tigo kuhakikisha mawasiliano yanaboreka zaidi na huduma za Intaneti zinapatikana vizuri zaidi na wakati huo huo kuhakikisha kuwa tunapeleka huduma za mtandao wa Tigo nje kidogo ya Tanzania, kuwawezesha wateja wapya kuungana na wenzao ulimwenguni na kuwa sehemu ya jamii kubwa ya mtandao wa mawasiliano ya simu.
“Tukiwa tunajiamini katika utoaji wa huduma bora za mawasiliano ya simu na nia ya kuendelea kusonga mbele zaidi kwa siku zijazo, tumeona umuhimu wa kupanua na kuboresha mtandao wetu. Uzinduzi wa minara hii mipya utatuwezesha kupanua huduma zetu za mawasiliano katika maeneo haya mapya, kwa wateja tulionao na tutakaokuwa nao kama tunavyodhamiria”
Pia katika kufanikisha uzinduzi huo kampuni  ya Tigo ilitoa vitabu 1000 vya sayansi katika shule ya msingi ya Nyaminkunga Tarafa ya Muyama Wilaya ya Buhigwe kama sehemu ya mchango wao kwenye sekta ya elimu, akipokea vitabu hivyo mwalimu mkuu wa shule hiyo bw.Hamisi Bunoge ameishukuru sana kampuni ya simu za mkononi  ya Tigo kwa mchango huo kwa kutambua umuhimu wa elimu katika nchi yetu ya Tanzania
Katika ripoti ya hivi karibuni ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ya robo mwaka ya mawasiliano ya mwezi Septemba 2012, idadi ya wateja wa Tigo iliongezeka kwa 20%  kati ya mwezi Juni mwishoni 2012 na Septemba 30, 2012 ikiwa na wateja 630,000 walioripotiwa. Tukiwa na mikakati hii ya upanuzi, tunatarajia kukua zaidi kwa mwaka huu 2013.
“SMILE, YOU ARE WITH TIGO”.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...