Monday, April 08, 2013

Waziri Mkuu wa Kwanza mwanamke nchini Uingereza Baroness Thatcher afariki dunia.


Waziri mkuu wa zamani nchini Uingereza Bibi Margret Thatcher amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 87 baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi.
Thatcher aliyekuwa mwanake wa kwanza kushika wadhfa huo, alikuwa alitokea chama cha Conservative na kuongoza nchi hiyo tangu mwaka 1979 hadi 1990.
Waziri Mkuu wa sasa nchini humo Bw. David Cameron ameelezea masikitiko yake na kumuita mwana mama huyo kuwa mjasiri wa Uingereza.
Naye Malkia Elizabeth wa II wa nchi hiyo hakusita kueleza kushitushwa na habari za kifo hicho huku akisema kimemhuzunisha lakini heshima ya kiongozi huyo itabaki palepale.
Kwa mujibu wa taarifa kiongozi huyo hatazikwa kwa mazishi ya kitaifa lakini atazikwa kwa hadhi sawa na Princes Diana nay a Mama wa Malkia.
Waziri Mkuu wa Uingereza Bw.  Cameron ambaye yuko ziarani nchini Hispania kwa ajili ya mikutano, amelazimika kukatisha ratiba ya mazungumzo yake na rais wa Ufaransa Francois Hollande na kurejea nyumbani.
Lady Thatcher kama alivyokuwa akijulikana alizaliwa akiitwa Margaret Roberts na kuhudumu kama mbunge wa Finchley –London Kaskazini tangu mwaka 1959 hadi 1992.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...