Monday, July 08, 2013

RAIS WA ZANZIBAR DK. ALI MOHAMED SHEIN AWAASA WAISLAMU NCHINI

 

Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohamed Shein amewataka Waislamu wote nchini kuishi na Watanzania wenzao katika misingi ya kuheshimiana, kuvumiliana na kupendana, kama Uislamu ulivyofundisha.

Dk Shein aliyasema hayo jana katika ufunguzi wa msikiti wa Masjid Taqwa, uliopo Ilala Bungoni, jijini Dar es Salaam, katika hotuba ilyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Mwinyihaji MakameKatika hotuba hiyo ya ufunguzi wa msikiti huo, Dk Shein alisema kuwa ni wajibu kwa Waislamu kufanya kila jitihada katika kuilinda amani na utulivu alioubariki Mwenyezi Mungu hapa Tanzania. 

Alisema kuwa kuna kila sababu kwa Waislamu kumshukuru Mwenyezi Mungu kwamba wanaweza kufanya ibada zao katika mkusanyiko mkubwa kama huo wa ufunguzi wa msikiti bila ya hofu, woga wala bughudha ya namna yoyote.Dk Shein alipongeza jitihada zinazochukuliwa na wasimamizi wa msikiti huo katika kuimarisha na kuitunza historia yake tangu ulipoanzishwa mnamo mwaka 1927, ambapo historia hiyo inadhihirisha kuwa msikiti huo ni miongoni mwa misikiti mikongwe katika Jiji la Dar es Salaam.

MKE WA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA, MAMA ANNA MKAPA AMETENGWA...!!!

MAMA ANNA MKAPA.

MKUTANO wa wake za marais uliofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi wazito, akiwemo Rais wa zamani wa Marekani, George W. Bush na Mkewe, Laura, umeacha kitendawili kizito kuhusu mke wa Rais wa zamani, Benjamin Mkapa, Mama Anna Mkapa. Imebainika kuwa katika mkutano huo, ambao mke wa Rais Jakaya Kikwete, Salma alikuwa ni mwenyeji wao, Mama Anna Mkapa hakuhudhuria, lakini pia imeonyesha wazi kwamba hakupewa fursa kulingana na hadhi yake. 

Mkutano huo wa Kimataifa ulifanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam, Juni 2-3 mwaka huu, uliozungumzia nafasi ya wanawake kuinuka kimaendeleo, ukizihusisha taasisi zinazoendeshwa na wake wa marais, wakiwemo wale wastaafu.



HAKEEM NA FATIMA WAAGA SHINDANO LA BBA USIKU WA LEO; MWANAMZIKI WA KIBONGO ATUMBUIZA

 Ikiwa leo ni siku ya 42 ndani ya jumba la BBA,kama inavyokuwaga siku zote kila jumapili huwa ni eviction day yaan lazma mshirik hata mmoja aage mashindano
Mwanadada Fatima kutoka Malawi ndiye aliyekuwa wa kwanza kuaga mashindano ya BBA kwa usiku wa leo.Mshiriki mwenzake kutoka Malawi  Natasha hakuamini kilichotea na kuanza kulia huku Fatima akimwambia Natasha  "No drama, no drama. It's not about you, chill out "kasha akaagana na wenziwe na kutoka nje ya jumba la BBA. 
  Hakeem kutokea nchini Zimbabwe nae ameyaaga mashindano usiku wa leo huku akiwa haamini kabisa kile kilichotokea kutokana na utani aliokuwa akiwatania wenzake kwamba wanatoka leo.Na cha zaidi amemuacha mchumba wake CLEO katika wakat wa majonzi.
 .Usiku wa leo ndania ya BBA ulipambwa na msanii mahiri kutoka TANZANIA aitwaye WAKAZI aliyeimba nyimbo zake WEEKEND na TOUCH.
Live Show: Wakazi sizzles on stage

HIZI NDIYO SABABU ZA MH ZITTO KABWE KUTOSHIRIKI TAMASHA LA MATUMAINI


Kupitia account yake ya facebook Mh. Zitto Kabwe amepost hotuba hii akielezea kushindwa kwake kufika katika tamasha la siku ya matumaini.
POST YAKE AMEANZA KWA KUANDIKA HIVI.

Global Publishers leo 7.7.2013 waliandaa Tamasha la Matumaini. Bahati mbaya sana sikuweza kuwahi kutokana na safari nilizonazo. Hii ni hotuba niliyopanga kuitoa na kuwatumia waandaaji.


TAMASHA LA MATUMAINI

Leo nilikuwa niwe nanyi kwa ajili ya siku hii muhimu sana kwa nchi yetu, siku ya matumaini kama inavyoandaliwa na Kampuni ya Global Publishers. Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa ndugu yangu Erick Shigongo kwa kuandaa tamasha hili kila mwaka. Nasikitika kuwa sitaweza kufanya pambano la ngumi na ndugu Ray na pia kuchezea timu yangu ya Wabunge wa Simba dhidi ya watani zetu Yanga. Hata hivyo naamini kuwa tamasha litakuwa na mafanikio makubwa na nipo nanyi japo sipo Dar es Salaam.


Ilikuwa niwepo Dar es Salaam leo, lakini nimeshindwa kuondoka Marekani kwa sababu Spika wa Bunge Mama Anna Makinda ameniagiza kwenye safari nyingine ndefu kwenda visiwa vya Cayman na baadaye Namibia kwa shughuli za Umoja wa Wabunge wa Jumuiya ya Madola. Sikuweza kukwepa jukumu hili la kitaifa maana limekuja ghafla na mimi nipo huku jirani na maeneo hayo. Naomba radhi sana kwamba sipo nanyi leo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...