Saturday, April 07, 2018

MAGUFULI APIGA MARUFUKU ASKARI NA VIONGOZI KUFYEKA NA KUCHOMA MASHAMBA YA BANGI

Rais Magufuli amepiga marufuku askari wa jeshi la polisi, na viongozi wote wa serikali wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa na makatibu wakuu kujishughulisha na kazi ya uchomaji na uteketezaji wa mashamba ya bangi na badala yake ameiagiza polisi kuwatumia wanakijiji kufanya kazi hiyo.
Hi
Ametoa agizo hilo leo wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha baada ya uzinduzi wa nyumba za askari na kushuhudia maonesho ya utayari ya jeshi hilo katika kukabiliana na uhalifu.
“Kama bangi imelimwa karibu na kijiji, shika kijiji kizima, kuanzia wazee, wamama mpaka watoto ndiyo wakafyeke hilo shamba, maaskari wangu hawakuajiriwa kufyeka mashamba ya bangi.… Usiwatume maaskari wako kufyeka bangi, mwisho wataumwa nyoka mule, mmevaa sare nzuri halafu mnafyeka bangi, mnaaibisha jeshi”, alisema Rais Magufuli

Rais amesema wanaolima bangi wakikamatwa ndio wanaotakiwa kuzifyeka.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 07, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS




ALIEVUMBUA MADINI YA TANZANITE APEWA MILLION 100 NA RAIS MAGUFULI

Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua dini la Tanzanite mwaka 1967.  
Jumanne Mhero Ngoma mvumbuzi wa madini ya Tanzanite.

Rais Dr. John Pombe Magufuli jana amezindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite huko Mererani mkoani Arusha ambapo katika uzinduzi huo alitambua uwepo wa mvumbuzi wa kwanza wa madini ya Tanzanite ambaye hakuwahi kutambuliwa na taifa.
Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua aina hiyo ya dini la Tanzanite mwaka 1967. Jumannne Ngoma ametambuliwa na Rais Magufuli na amemzawadia shujaa huyo milioni 100 kwa ajili ya kumsaidia kujikimu na matibabu baada ya mzee huyo kupooza sehemu ya mwili.

Rais Magufuli aliwahakikisha wachimbaji wadogo kwamba atawajengea 'mazingira ili kusudi wafaidi na Tanzanite zaidi'

Tanaznite ni madini ambayo ni ya kipekee kwa Tanzania haipatikani sehemu yeyote duniani. Mauzo ya Tanzanite duniani yanafikia dola za Marekani milioni 50. Tanzanite ni jiwe yenye miaka milioni mia 6 na iligundulika Mererani, Arsuha, kaskazini mwa Tanzania, mwaka 1967. Inasemekana kuwa na upekee hata ziadi ya alhmasi.

MAAJABU: JAMAA ATOLEWA MSWAKI TUMBONI

Mswaki 
Madaktari katika Hospitali Kuu ya Mkoa ya Pwani (CPGH) mjini Mombasa, Kenya wamefanikiwa kuutoa mswaki ambao ulikuwa umekwama tumboni mwa mwanamume mmoja kwa siku sita.

David Charo alikuwa akipiga mswaki alipoumeza kimakosa Jumapili wiki iliyopita apokuwa anajiandaa kwenda kazini Bamba, Kilifi. Kufikia jana, alikuwa ameanza kupata matatizo ya kupumua.
 Davis Charo 
Awali, madaktari walikuwa wamedokeza kwamba angehitaji kufanyiwa upasuaji kuutoa. Lakini Ijumaa asubuhi, madaktari wakiondozwa na Ramadhan Omar wamefanikiwa kuutoa mswaki huo bila kumfanyia upasuaji wa kawaida.

Badala yake, wamemfanyia upasuaji wa kutumia matundu madogo. Jumapili, Charo alipokuwa alipoumeza mswaki huo kimakosa, awali ulikwama ndani ya koo kabla ya kutumbukia ndani tumboni.

MARAIS WALIOPANDISHWA KIZIMBANI NA KUHUKUMIWA KIFUNGO WIKI HII

  Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma
Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma
 
Wiki hii tumeshuhudia baadhi ya marais wastaafu wa nchi mbalimbali wakifikishwa mahakamani kusomewa mashtaka na wengine kuhukumiwa vifungo gerezani. Miongoni mwa marais hao ni:-

Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma amefika mahakamani kujibu mashtaka ya ulaji wa rushwa yanayohusishwa na mkataba wa ununuzi wa silaha miaka ya tisini.

Baada ya Zuma (75) kufika mbele ya Mahakama Kuu kwa dakika 15 huko Durban, kesi hiyo iliahirishwa hadi tarehe 8 mwezi Juni.

Ameshtakiwa kwa makosa kumi na sita ya ulaji wa rushwa, ufisadi, ulaghai na ulanguzi wa fedha, aliyoyaepuka wakati wa utawala wake na kurejeshwa tena mwaka 2016. Bw Zuma alitolewa madarakani kwa nguvu mwezi Februari mwaka huu.
  Rais wa zamani wa Korea Kusini Park Geuin Hye 
Rais wa zamani wa Korea Kusini Park Geuin Hye  

Aliyekuwa rais wa Korea Kusini, Park Geuin Hye, amehukumiwa kifungo cha miaka 24 jela, baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi, iliyomuondoa madarakani.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...