Saturday, April 07, 2018

ALIEVUMBUA MADINI YA TANZANITE APEWA MILLION 100 NA RAIS MAGUFULI

Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua dini la Tanzanite mwaka 1967.  
Jumanne Mhero Ngoma mvumbuzi wa madini ya Tanzanite.

Rais Dr. John Pombe Magufuli jana amezindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite huko Mererani mkoani Arusha ambapo katika uzinduzi huo alitambua uwepo wa mvumbuzi wa kwanza wa madini ya Tanzanite ambaye hakuwahi kutambuliwa na taifa.
Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua aina hiyo ya dini la Tanzanite mwaka 1967. Jumannne Ngoma ametambuliwa na Rais Magufuli na amemzawadia shujaa huyo milioni 100 kwa ajili ya kumsaidia kujikimu na matibabu baada ya mzee huyo kupooza sehemu ya mwili.

Rais Magufuli aliwahakikisha wachimbaji wadogo kwamba atawajengea 'mazingira ili kusudi wafaidi na Tanzanite zaidi'

Tanaznite ni madini ambayo ni ya kipekee kwa Tanzania haipatikani sehemu yeyote duniani. Mauzo ya Tanzanite duniani yanafikia dola za Marekani milioni 50. Tanzanite ni jiwe yenye miaka milioni mia 6 na iligundulika Mererani, Arsuha, kaskazini mwa Tanzania, mwaka 1967. Inasemekana kuwa na upekee hata ziadi ya alhmasi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...