Sunday, June 16, 2013

BINTI ACHOMWA MOTO HADI KUFA BAADA YA KUOMBA AOLEWE NA NDUGU YAKE...!!!


Msichana wa miaka 19 amechomwa moto hadi kufa na mama yake kupigwa baada ya kuwaomba wazee wa kijiji kuruhusiwa kuolewa na mvulana mmoja kutoka kijijini hapo na ukoo mmoja, polisi wa India wamethibitisha.
Anju Yadav, kutoka kijiji cha Karahkol, wilayani Deoria katika jimbo la Uttar Pradesh, alichomwa moto nyumbani kwake wakati mama yake, Gyanwati Devi, mwenye miaka 48, alipokuwa upande mwingine wa kijiji hicho akiiomba halmashauri ya kijiji kumruhusu Anju aolewe na rafiki yake wa kiume aliyekuwa na mahusiano naye kwa miaka miwili, Ranjit Yadav, mwenye miaka 21.
Lakini halmashauri ya kijiji hicho, sambamba na baba wa mvulana huyo, Jai Hind Yadav, mwenye miaka 52, walitupilia mbali maombi hayo wakisisitiza ilikuwa kinyume cha utamaduni.

Badala yake, baba wa mvulana huyo alikimbilia kwenye nyumba ya familia na kumchoma moto msichana huyo, ilidaiwa.
Jamii ya India inafahamika mno kwa mfumo wake wa ukoo ulioingiliana, ambao unaweza kuzuia watu kutoka jamii tofauti kuoana na katika baadhi ya matukio kuafikiana na jambo kama hilo.

OMMY DIMPOZ AANZA SAFARI YA KWENDA NYUMBANI KWA AKINA MANGWEA KUOMBA MSAMAHA

 
Kutokana na kauli aliyotoa msanii Ommy Dimpoz ya SITAKUFA KIJINGA NA KIMASIKI KAMA KAMA ALIVYOKUFA NGWAIR, hii ndio kauli aliyotoa baada ya mashabiki na Wanamuziki wenzake kumaind kwa kile alichokisemahttps://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKiN6BrFwokEV_2Z_ENfiFrWaNHdg_4ahM2D2NktQGeixKbh3-1ZjbVuKvlJtAk_l3af9FSyxVZYQkdxlXT1WMaz8T3v94BhpaRuUlze-iL1pPiQyA46yUL0_lSrcBCqYLWDnMLuwMKZw/s1600/dimpoz.jpg
NANUKUHU:
"Samahani tena sana sitawacha kuomba msamaha, nimekubali makosa na hivi sasa naelekea nyumbani kwao kuomba msamaha kwa familia na nitue kwa vituo vya radio kuomba msamaha kwa wabongo na wote niliowaudhi. Samahani sana na nakubali mimi si mtu bila nyinyi na sikuongea kuhusu legend Ngwair kwa ila mbaya. One love". mwisho wa kunukuu

KIM KARDASHIAN AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE...!!!

NI siku ya furaha kwa Kanye West! Kim Kardashian amejifungua mtoto wa kike Jumamosi asubuhi katika hospitali ya Cedars-Sinai Medical Center, Los Angeles, mtandao wa OMG umethibitisha.

Inasemekana Kardashian, 32, alikuwa na West pembeni mwake wakati wa kujifungua, kumkaribisha duniani binti yao mwezi mmoja kabla ya muda uliotarajiwa. Tarehe halisi ya kujifungua ilitazamiwa kuwa Julai 11.

"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye kupata mtoto mapema," chanzo cha hospitali kimeileza Us Weekly. “Inafurahisha, wote katika hali nzuri!"

Kanye West, 36, na Kim - wote wawili wakiwa ndo mara ya kwanza kuwa wazazi, wamekuwa wapenzi tangu Aprili 2012. Desemba 30, 2012, West alitangaza kwamba mpenzi wake alikuwa na mimba wakati wa tamasha lake Atlantic City.

"Simamisha muziki na wote mpige kelele kwa mama kijacho," alisema West jukwaani akionyesha kidole kwa Kim ambaye alikuwa mmoja wa  watazamaji.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 16, 2013

.
.

HABARI YA KINA KUHUSU MLIPUKO WA BOMU ARUSHA


Mkutano wa Chadema wa kumaliza kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani mjini Arusha, jana ulivunjika baada ya bomu kulipuka na kuua watu wanne na wengine kujeruhiwa.Bomu hilo lililipuka jana saa 11:50 dakika chache kabla ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe kumaliza kuhutubia mkutano huo uliofanyika katika Viwanja vya Soweto mjini Arusha na kuhudhuriwa na mamia ya wananchi.Hilo ni tukio la pili la bomu kulipuka katika mkusanyiko wa watu, Mei 5 mwaka huu bomu lililipuka katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi, Parokia ya Olasit mjini Arusha na kuua watu watatu na wengine kujeruhiwa.


Mama akikimbizwa hospitali kupata matibabu.

 Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru Frida Mokiti alisema katika hospitali yake kuna maiti moja ya mtoto na majeruhi 11.Habari zingine zilisema katika hospitali ya Misheni ya Selian kuna maiti za watu wawili, waliokufa kutokana na shambulio hilo na majeruhi ambao idadi yao haijafahamika.Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema katika tukio hilo watu wawili wamepoteza maisha, mwanamke na mwanamume na kwamba idadi ya majeruhi bado haijafahamika kwa kuwa wametawanywa katika hospitali mbalimbali mkoani humo.

HILI NDILO CHIMBUKO LA JINA LA ANACONDA ANALOTUMIA JAYDEE

 Huyu naye alikuwepo ili kuonyesha uhalisia wa jina la Anaconda ambalo sasa anatumia msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini Jay Dee, ambapo jina hilo limetokana na vuguvugu ambalo linaendelea hivi sasa ambalo hilo vuguvugu ndilo limechangia shoo ya mwanamuziki huyo kujaa huku mashabiki wakionyesha hali ya kumshinda mtu anyemkandamiza msanii huyo

CHADEMA YAKANA TUHUMA ZA KUUA WATU.

Singo Kigaila.

Huku kukiwa na madai kuwa Chadema inahusika na matukio ya kula njama za utekaji na kuteka, kupiga na kuua watu, chama hicho kimekuja juu na kukanusha madai hayo.

Pamoja na kukanusha, kimemwomba Rais Jakaya Kikwete aunde tume huru ya kimahakama kuchunguza matukio yaliyotokea ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wote watakaobainika kuhusika.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mafunzo na Oganaizesheni wa chama hicho, Singo Kigaila, alisema walishamwomba Rais aunde Tume lakini akadai ombi hilo halijatekelezwa hadi sasa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...