Sunday, October 13, 2013

UFO SARO BADO YUKO KATIKA CHUMBA CHA UPASUAJI MHIMBILI

IMG_0031Pichani chini baadhi ya Wafanyakazi wenzake na Ufo Saro kutoka IPP pamoja waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali wakiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako Ufo Saro ambaye mpaka sasa, yuko katika chumba cha upasuaji  baada ya kupigwa risasi na mchumba wake Anteri Mushi usiku wa kuamkia leo ambapo pia alimpiga mama mzazi wa Ufo Saro Anastazia Peter Saro miaka 59 aliyefariki hapohapo  na baadae kujipiga risasi mwenyewe na kufa hapohapo, Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo huko Mbezi Luisi 1 2Wafanyakazi hao wakibadilishana mawazo hapa na pale katika hospitali ya Muhimbili leo hii 3 4Picha Kwa Hisani ya Fullshangwe Blog

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 13, 2013

DSC 0092 7ee69
DSC 0093 41bc7

SINTOFAHAMU WAIZARA YA HABARI.....!!!


makala dca7a
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amos Makalla, jana alitoa taarifa kwa umma akieleza bayana kwamba yeye ndiye aliyeliruhusu gazeti hili kuendelea kutolewa kwa njia ya mtandao (online) na Gazeti la Rai kutolewa kila siku.
Makalla alitoa ufafanuzi huo muda mfupi baada ya Idara ya Habari-Maelezo kutoa taarifa kwamba Serikali imesikitishwa na Gazeti la Mwananchi na gazeti dada la Rai, Mtanzania kukiuka masharti ya adhabu walizopewa.
Septemba 27, mwaka huu Serikali iliyafungia Mwananchi kwa siku 14 na Mtanzania siku 90.
Wakati likianza kutumikia adhabu yake, Mwananchi ambalo tayari limemaliza kuitumikia, liliendelea kutoa taarifa kwenye tovuti yake wakati Kampuni ya New Habari (2006) Ltd ambayo inamiliki Mtanzania ilianza kuchapisha kila siku gazeti la Rai ambalo awali lilikuwa likichapishwa kila wiki.
Katika ufafanuzi wake alioutoa
jana Makalla alisema: "Nimelazimika kueleza haya baada ya taarifa mpya ya Idara ya Habari-Maelezo iliyohoji uhalali wa gazeti la Mwananchi kuwa online (mtandaoni) na gazeti la Rai kutoka kila siku, badala ya mara moja kwa wiki (Alhamisi)."

IVORY COAST WAIFUMUA SENEGAL 3-1 NA KUBISHA HODI KOMBE LA DUNIA

WASHAMBULIAJI Didier Drogba, Salomon Kalou na Gervinho wote wamefunga jana Ivory Coast ikiifumua 3-1 Senegal na kuongeza matumaini ya kufuzu Fainali za Kombe la Dunia mwakani.Drogba alifunga kwa penalti dakika ya tano, kabla ya winga wa zamani wa Arsenal, Gervinho kufunga la pili dakika tisa na baadaye kipindi cha pili Salomon Kalou akafunga la tatu mjini Abidjan.
article-2456451-18B3202400000578-136_634x423_49689.jpg
Tembo wauwaji: Wachezaji wa Ivory Coast wakishangilia ushindi wao leo
Sasa Ivory Coast watahitaji sare au kufungwa si zaidi ya wastani wa bao moja katika mchezo wa marudiano moja ili kujikatia tiketi ya Brazil mwakani. Seneal yenyewe itahitaji kushinda 2-0 tu nyumbani, ili kujihakikishia kurejea Fainali za Kombe la Dunia.
article-0-18B2FA6200000578-877_634x446_38bb0.jpg
Didier Drogba ameifungia Ivory Coast leo
article-2456451-18B3209700000578-178_634x453_e3f22.jpg
Salomon Kalou na Drogba walicheza pamoja Chelsea miaka kadhaa
article-2456451-18B3D49200000578-154_634x416_2ec82.jpg
Umefanya vizuri: Gervinho akizungumza na kocha Sabri Lamouchi baada ya mechi
Bao pekee la Senegal lilifungwa na Papiss Cisse dakika tano kabla ya filimbi ya mwisho.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...