Sunday, April 08, 2018

WADAU WA USAFIRI TABORA WATAKA MADEREVA WA MAGARI YA MIZIGO KUBANWA

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora na Wadaau wa Usafiri wamependekeza uanzishwaji wa matumizi ya vitabu (log book) kwa magari ya mizigo ili kudhibiti madereva kusafiri mwendo mrefu bila kupumzika na hivyo kusababisha ajali kwa magari yao au kugongana uso kwa uso na magari mengine kutokana na uchovu.

Tamko hilo limetolewa jana wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri mara baada ya kikao cha kujitathimini kwa ajili ya kuja na majibu ya kuondoa ajali za barabarani mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema vitabu hivyo vitasaidia kuonyesha muda alitoka , mahali alitoka na kama amesafiri muda mrefu atalazimisha apumzike ili kuepusha ajali.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 08, 2018 YA DINI, MICHEZO NA HARDNEWS


TUCTA YAWALILIA WATUMISHI DARASA LA SABA YATAKA WARUDISHWE KAZINI

Baraza Kuu la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA ) jana Jumamosi Aprili 7, 2018 limetoa tamko lenye mambo saba, likiwemo la kupinga uamuzi wa Serikali kuwafuta kazi watumishi wake wenye elimu ya darasa la saba.

Akisoma tamko hilo mbele ya wajumbe wa baraza kuu la TUCTA katika mkutano wa baraza hilo uliofanyika mkoani Morogoro mwenyekiti wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya amesema uamuzi huo wa Serikali si sahihi na hivyo wametaka watumishi hao kurejeshwa kazini.

Amesema baraza limesikitishwa na uamuzi wa kuwaondoa kazini watumishi wa umma na taasisi zinazopokea ruzuku kutoka serikalini.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...