Sunday, April 08, 2018

WADAU WA USAFIRI TABORA WATAKA MADEREVA WA MAGARI YA MIZIGO KUBANWA

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora na Wadaau wa Usafiri wamependekeza uanzishwaji wa matumizi ya vitabu (log book) kwa magari ya mizigo ili kudhibiti madereva kusafiri mwendo mrefu bila kupumzika na hivyo kusababisha ajali kwa magari yao au kugongana uso kwa uso na magari mengine kutokana na uchovu.

Tamko hilo limetolewa jana wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri mara baada ya kikao cha kujitathimini kwa ajili ya kuja na majibu ya kuondoa ajali za barabarani mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema vitabu hivyo vitasaidia kuonyesha muda alitoka , mahali alitoka na kama amesafiri muda mrefu atalazimisha apumzike ili kuepusha ajali.

Alisema malori yamekuwa yakisafiri mwendo mrefu bila hata dereva wake kupumzika jambo ambalo limesababisha magari hayo yapate ajali au wakati mwingine yawe chanzo kinachosabisha ajali katika magari ya abiria.

Mwanri alisema kwa kulitambua hilo wanaona wakati umefika kwa magari ya mizigo nayo kuwa na vitabu(log book ) inayoonyesha muda alianza safari katika kituo chake cha kwanza na muda alipo baada ya kusimamishwa ili kuona kama kweli amezingatia matawaka ya kitaalamu na sharia ya kutokwenda kasi.

Alisema kitaalamu dereva anatakiwa aendeshe chombo cha moto kwa muda usiozidi saa nane lakini mara nyingi madreva wa malori wamekuwa wakiendesha magari yao hata zaidi ya muda huo jambo ambalo limekuwa kiwasababisha baadhi yao kuendesha huko wakisinzia na kupelelea gari kukosa mwelekeo.

Mwanri alisema ili kuepukana na hilo wadau wamependekeza wammiliki wa gari wa ya mizigo ya masafa marefu ni vema wawe na madereva wawili ili wasaidiane.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema hatua nyingine ambayo wameamua kuichukua ni pamoja na kuongeza askari na magari ya doria katika barabara kuu ya Igunga, Nzega kwenda Mwanza na Shinyanga.
Alisema hatua hii inalenga kupambana na madreva ambao nyakati za usiku wakwenda mwendo mkali kwa sababu ya kujua kuwa nyakati hizo tochi hazifanyi kazi.

Mwanri aliongeza kuwa Wadau wa usafiri wameiagiza Wakala wa Barabara Tanzania(TANROADS) mkoani Tabora kuhakikisha wanaziba mashimo yaliypo katika barabara kuu zote ili kuondoa uwezekano wa yenyewe kuwa chanzo cha ajali za barabarani.

Aidha alisema kuwa Wadau wamekuwabaliana kuwa ukaguzi wa madereva na magari katika barabara kuu zinazopita Mkoani Tabora utakuwa unafanyika  kila siku ili kujihakikishia kama gari linazo breki, taa zifanya kazi vizuri , matari yako vizuri na dreva ajatumia kilevi.

Alisema hatua hiyo inalenga kujihakikishia kama chombo cha usafiri na dreva wake yuko katika hali nzuri.

Hivi karibuni (4 /4/2018) kulitokea ajali ambapo basi la abiria Kampuni ya City Boy yenye namba T 983 DCE iligongana uso kwa uso lori lenye namba T .486 ARB Mitsubishi Fuso wilayani Igunga na kusababisha watu 12 kufa palepale na mmoja kufia katika Hospitali ya Rufaa Bugango.

Taarifa za awali zinaoonyesha kuwa chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa Fuso uliosababisha tairi kupasuka na gari kuhamia upande wa basi. Lori hiyo lilikuwa na viazi ambavyo lilivitoa Njombe.

Na Tiganya Vincent, Tabora

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...