Wednesday, January 18, 2017

WAZIRI MKUU WA ZAMANI APIGWA KOFI HADHARANI

Waziri mkuu mstaafu wa Ufaransa Manuel Valls amekashifiwa alipokuwa akihamasisha katika kampeni za chama cha kisoshalisti katika uchaguzi mkuu wa kiti cha Urais nchini Ufaransa.

Alipokuwa akihutubia katika ukanda wa Magharibi mwa mji wa Brittany alipigwa kofi na kijana mdogo alipokuwa akisalimia kwa kushikana mikono.

Mlinzi binafsi wa Bwana Valls alimkamata kijana huyo kooni kisha akamtupa chini.

Manuel Valls hajajeruhiwa katika tukio hili. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz, pia tufollow instagram @jambotz.

ALIYETABIRI KIFO CHA MUGABE AKAMATWA....!!!

Mchungaji Patrick Mugadza 

Maafisa wa polisi nchini Zimbabwe wamemkamata na kumzuilia mhubiri aliyetabiri kwamba Rais Robert Mugabe atafariki mwezi Oktoba mwaka huu.

Mchungaji Patrick Mugadza alikamatwa akiwa mahakamani mjini Harare Jumatatu ambapo alikuwa ameenda kwa kesi nyingine dhidi yake, wakili wake Gift Mtisi ameambia wanahabari.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe.

Mchungaji huyo alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kuvalia bendera ya taifa. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz pia tufollow instagram @jambotz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...