Wednesday, June 26, 2013

TANGAZO: NAFASI ZA MASOMO



|             ST. THOMAS INSTITUTE OF TECHNOLOGY & MANAGEMENT
                 
                              P.O. BOX 6089, Morogoro. CEL: 0713 530261, 0717-707025, 0767 530261, 0655 758980
                                                  Email: magkit2005@yahoo.com
Chuo kipo Morogoro mjini, Kilakala. Chuo Kipo katika mazingira mazuri ya kujifunzia. Studio za kisasa kwa wanafunzi wa Uandishi wa habari na Utangazaji.
LIST OF COURSES
S/N
COURSE
DURATION
1
CERTIFICATE IN BUSINESS ADMINISTRATION
1YEAR
2
 CERTIFICATE IN HOTEL MANAGEMENT
6MONTHS
3
CERTIFICATE IN HUMAN RESOURCE MANAGEMENT.
1YEAR
4
CERTIFICATE IN INFORMATION TECHNOLOGY (IT).
1YEAR
5
CERTIFICATE IN COMPUTER SCIENCE.
1YEAR
6
CERTIFICATE IN RECORD MANAGEMENT
1YEAR
7
  CERTIFICATE IN PROCUREMENT AND SUPPLY
1YEAR
8
CERTIFICATE IN NURSERY TEACHING AND KIDERGATEN
6MONTHS
9
CERTIFICATE IN ACCOUNTANCY.
1YEAR
10
CERTIFICATE IN COMMUNITY DEVELOPMENT.
1YEAR
11
CERTIFICATE IN JOURNALISM&MASS COMMUNICATION

1 YEAR
12
BASIC CERTIFICATE IN BUSINESS ADMINISTRATION
6MONTHS
13
BASIC CERTIFICATE IN HUMAN RESOURCE MANAGEMENT.
6MONTHS
14
BASIC CERTIFICATE IN INFORMATION TECHNOLOGY (IT).
6MONTHS
15
BASIC CERTIFICATE IN COMPUTER SCIENCE.
6MONTHS
16
BASIC CERTIFICATE IN RECORD MANAGEMENT
6MONTHS
17
  BASIC CERTIFICATE IN PROCUREMENT AND SUPPLY
6MONTHS
18
BASIC CERTIFICATE IN ACCOUNTANCY.
6MONTHS
19
BASIC CERTIFICATE IN COMMUNITY DEVELOPMENT.
6MONTHS

Kwa wanachuo wa Uandishi wa Habari na Utangazaji Muhula mpya utaanza Rasmi tarehe July 8 mwaka huu..

MZEE MANDELA AFANYIWA MAOMBI MAALUM


 ASKOFU mkuu wa kanisa la kianglikana mjini Cape Town, Afrika Kusini, Thabo Makgoba, amejitolea kufanya maombi kwa niaba ya rais mstaafu Nelson Mandela ambaye anaugua sana hospitalini.
Kasisi huyo anamuombea Mandela aweze kupata nafuu na amewataka wananchi kumshukuru kwa yote aliyowafanyia.
Jamaa za Nelson Mandela wamekutana nyumbani kwake huko Kunu, huku hali yake ya afya ikizidi kudorora hospitalini, Pretoria.
Afya ya Bwana Mandela ilikuwa mbaya zaidi Jumapili.
Maombi hayo yalitolewa baada ya Askofuu huyo kumtembelea Mandela hospitalini ambako kiongozi huiyo wa zamani amekuwa akilazwa kwa wiki mbili na nusu zilizopita baada ya kuugua mapafu.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa wajukuu wa rais huyo wa zamani wa Afrika kusini wanakutana nyumbani kwake kijijini katika mkoa wa Eastern Cape province, ambako viongozi wa kitamaduni wamealikwa.
Halikopta ya jeshi kadhalika zilionekana zikipaa karibu nyumbani kwa mandela. Afisi ya Rais jacob Zuma ilitangaza jumapili kuwa hali ya mzee Mandela ya afya ilikuwa mbaya sana. Chanzo: bbcswahili

Ujio wa Obama: Mashirika ya ndege yatakiwa kubadili ratiba za safari Julai Mosi

Maandalizi ya ujio wa Rais wa Marekani, Barack Obama nchini yanazidi kupamba moto huku maofisa wa usalama wa Marekani wakipiga kambi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Dar es Salaam.

Aidha, kutokana na ujio huo, Serikali imeagiza mashirika yote ya ndege kubadili ratiba zao za safari Julai Mosi, siku ambayo Rais huo atatua nchini. Jana, waandishi wetu walishuhudia pilikapilika za kuimarisha ulinzi katika uwanja huo jambo ambalo uongozi wa uwanja huo jambo wamelieleza kwamba halijawahi kutokea.
Ulinzi haujawahi kutokea Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Moses Malaki alisema jana kwamba ratiba za uwanjani hapo zitabadilika kutokana na uzito wa ugeni huo.Alisema kwa kawaida anapokuja kiongozi mkubwa wa kitaifa katika uwanja huo hakuna ndege inayoruhusiwa kutua kwa kipindi cha nusu saa. “Ni kweli hali hiyo pia itakuwapo atakapokuja Rais Obama na safari za ndege zitabadilika kulingana na ratiba ya kutua na kuondoka kwa Rais huyo,” alisema Malaki.Pia alisema ulinzi katika uwanja huo umeimarishwa kwa mwezi mmoja sasa na tangu wakati huo, maofisa wa usalama wa Marekani wamekuwa wakifika kwa nyakati mbalimbali. “Sijawahi kuona ulinzi mkali kama huu, wamekuja marais wengi hapa nchini lakini ulinzi huu ni wa kutisha, sijui kwa sababu gani?” alisema Malaki.Alisema awali, wakati maofisa hao walipoanza kuwasili nchini hawakutambua ni mgeni gani anayetarajia kufika lakini baadaye walipelekewa taarifa kuwa ni Rais Obama na baadaye walitaarifiwa kuwa angetua saa 8.40 mchana, Julai Mosi.Mkurugenzi huyo alisema Rais Obama atakuja na ndege nne, moja itakayombeba, ya pili kwa ajili ya mizigo, ya tatu itakuwa ya waandishi wa habari na maofisa wa usalama na ya mwisho ni kwa ajili ya dharura ambayo itaegeshwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

MTOTO WA MNADHIMU MKUU WA JWTZ AFUMWA KWA MGANGA WA KIENYEJI AKIROGA

 
Mama mmoja ajulilikanae kwa jina la Magreth simon Nkwera ambae ni mtoto wa kwanza wa mnadhimu mkuu wa kwanza wa JWTZ Brig Gen Simon Nkwera amekamatwa kwa Mganga wa kienyeji akijaribu kutekeleza jaribio la kuwauwa baadhi ya watoto wa mumewe na baadhi ya ndugu zake huko kibaha maili moja mkoani Pwani na hivi sasa yupo katika kituo cha polisi Maili moja akisubiri kupandishwa kizimbani.
Mtuhumiwa akiwa ndani ya chumba cha mganga na mganga wake aitwae Yahaya tayari kwa mauwaji
Mtuhumiwa huyo akiwa ndani ya gari la polisi baada ya kukamatwa
Mtuhumiwa akiwa anahojiwa na mzee wa ukoo wa shirima Afisa polisi jeshi daraja la Kwanza (woii mstaafu) Joseph Shirima mara baada ya kumkamata live kwa sangoma.
CHANZO VIJIMAMBO

NATASHA AFUNDWA: MASTAA WAKATA MAUNO MBAYA:

Baadhi ya waalikwa wakijiachia pamoja na Natasha (kushoto) wakati wa sherehe hiyo.
Na Imelda Mtema
HUKU siku za kufunga ndoa zikihesabika, mkongwe kwenye filamu za Kibongo, Suzan Lewis ‘Natasha’ amefanyiwa sherehe ya kufundwa kabla ya kwenda kwa mumewe ambayo huko mitaani inajulikana zaidi kwa jina la singo.Shughuli hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita, Tandika Maghorofani, Dar ambapo iliandaliwa na shostito wa Natasha aliyejulikana kwa jina moja la Nuru.

APEWA SOMO
Natasha aliwekwa ndani kwa muda wa saa moja akipewa somo la ndoa na watu maalumu walioandaliwa kwa ajili ya shughuli hiyo kabla ya kutoka nje kuungana na wageni waalikwa.

Alipotoka nje, alikutana na waalikwa ambapo kati yao ni mastaa mbalimbali Bongo kisha wakaungana kwenye zoezi zima la kucheza ngoma.
KIASILI ZAIDI
Waalikwa walipata nafasi ya kupakwa urembo mbalimbali wa kiasili usoni na kuifanya hafla hiyo iwe ya kipekee kutokana na vivutio hivyo.
Baada ya yote hayo kukamilika, msafara wa kuelekea nyumbani kwa Natasha, Yombo ulianza huku ngoma zikiendelea kupigwa na mastaa mbalimbali wakikata mauno ndani ya gari.

Akizungumzia shughuli hiyo, Natasha alisema: “Nashukuru sana jamani kwa kupita hatua hii ya kwanza kuelekea kwenye ndoa yangu. Siwezi kuacha kumshukuru zaidi rafiki yangu Nuru kwa kunifanikishia.”

SERIKALI YATOA TAMKO KUHUSU KAULI YA WAZIRI MKUU...YADAI POLISI WANARUHUSIWA KUPIGA NA KUUA KISHERIA

Serikali imetoa tamko bungeni kuhusu mauaji ya raia mikononi mwa polisi ikieleza kuwa sheria ya kanuni ya adhabu inaruhusu kutumia nguvu za kadiri hata kiasi cha kusababisha madhara au kifo. 
Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kunukuliwa bungeni akiwataka polisi kuwashughulikia kwa kuwapiga watu wote wanaokaidi kutii sheria.
“…Nasema wapigwe tu, maana tumechoka sasa,” alisema Pinda alipojibu maswali ya papo hapo Alhamisi iliyopita.
Akisoma tamko hilo bungeni jana, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima alisema kuwa kifungu cha 18(B) na 18(C) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinatoa uwezo kisheria wa kutumia nguvu za kadiri hata ikibidi kiasi cha kusababisha madhara au kifo katika mazingira ya kisheria.
Aliyataja mazingira hayo kuwa ni pamoja na kuokoa uhai wa mtu mwingine, kuzuia madhara makubwa ya mwili yasitokee kwake au kwa mtu mwingine na kumzuia mtu anayetenda tendo ovu la kubaka au kunajisi mtoto au kufanya vitendo kinyume na maumbile.
Pia kumzuia mtu anayevunja nyumba usiku au unyang’anyi wa kutumia silaha au kuchoma nyumba moto au kufanya kitendo chochote kinachohatarisha uhai wa mtu au mali.
Alieleza kuwa Kifungu cha 18 na 18(A) cha Sheria ya Adhabu Sura namba16 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2002, kinampa haki mtu yeyote akiwemo askari kujilinda, kumlinda mtu mwingine, kulinda mali yake au mali ya mtu mwingine ikiwemo ya Serikali na taasisi zake, ambayo iko chini ya uangalizi wake kisheria.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 26, 2013

.
.

RAIS WA MAREKANI BARAK OBAMA KUANZA ZIARA BARANI AFRIKA LEO

 
Rais Barack Obama anafanya ziara ya pili barani Afrika kuanzia leo Jumatano. Atazuru Senegal, Afrika Kusini na Tanzania.
Rais wa  Marekani Barack Obama  Jumatano anaanza ziara ya wiki moja nzima katika nchi tatu za Afrika kwa lengo la kuhamasisha demokrasia na uwekezaji wa Marekani barani humo.

Rais Obama  atakwenda Senegal leo Jumatano ambako atakutana na rais Macky Sall na  kesho Alhamis atatembelea nyumba ya kihistoria ya watumwa  wa Afrika walioletwa Marekani katika kisiwa cha Goree.
Ijumaa bwana Obama atakwenda Afrika Kusini ambako atakutana na rais Jacob Zuma na kutembelea kisiwa  cha Robben ambacho rais wa zamani Nelson Mandela alifungwa jela.

Maafisa wa Afrika Kusini walisema ziara ya bwana Obama itaendelea licha ya kuwepo na hofu kote nchi  humo kuhusu  kudhoofika kwa  afya ya bwana Mandela. Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini mwenye miaka 94 yuko katika hali mahtuti na amelazwa katika  hospitali moja mjini  Pretoria.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...