Friday, October 11, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 11, 2013

DSC 0059 cbb36
DSC 0060 33282DSC 0061 02d88

ICC: MAWAKILI WA KENYATTA WATAKA KESI IFUTWE


uhurukenyatta_b6263.jpg
Mawakili wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, wameitaka mahakama ya kimataifa ya jinai kusimamisha mashtaka ya Rais huyo kabla ya kesi yake kuanza mwezi ujao.
Wanasheria hao wamesema mashahidi wa utetezi wamekuwa wakitishwa, na kwamba wanao ushahidi wa kutosha kuthibitisha ukiukwaji wa taratibu za mahakama hiyo.
Rais Kenyatta na Naibu wake William Ruto, wanatuhumiwa kuchochea wimbi la vurugu za baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007.
Takriban watu1,200 walifariki na wengine laki sita kuachwa bila makao wakati wa ghasia hizo.
Kesi dhidi ya Kenyatta inatarajiwa kuanza tarehe 12 mwezi Novemba.
Naibu Rais pia yuko mbele ya mahakama hiyo na yeye ndiye afisaa mkuu wa kwanza wa serikali kufikishwa mbele ya mahakama ya ICC.
Mawakili wa Kenyatta waliwasilisha nyaraka za kurasa 38 siku ya Alhamisi kwenye mahakama hiyo wakiitaka kesi hiyo kutupiliwa mbali.
Nyaraka hizo zilisema kuwa upande wa utetezi una ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa mahakama imekua ikiendelea kukiuka taratibu zake.
Pia zilisema kuwa kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha kuwa mashahidi wa upande wa mashitaka na mwengine mmoja walihusishwa na njama ya kutaka kuhujumu sheria.
Mawakili wa uetetzi aidha walituhumu upande wa mashitaka kwa kuwasilisha kesi ambayo ni ya kifisadi na sio ya haki dhidi ya Rais Kenyatta.
Upande wa mashitaka sasa unatarajiwa kujibu madai hayo na mahakama ya ICC huenda ikaamuru jopo la kusikilizwa kwa madai hayo kuyathibitisha.

"TUMETOKA KUFUNGONI NA HAMASA KUBWA".......... MWANANCHI

MwananchiKurudiClip_1a8e4.jpg
Hata hivyo, huu hakika sio wakati wa kumtafuta mchawi, kwa maana ya kutaka kujua nani hasa serikalini alitoa amri ya kulifungia gazeti hili kwa sababu ambazo sisi tunaona hazikuwa na chembe ya mashiko. Tulishangazwa kuona amri hiyo ya Serikali ikitolewa wakati mkuu wa nchi, Rais Jakaya Kikwete akiwa nje ya nchi, tena akiwa katika majukumu mazito ambayo dunia nzima ilikuwa ikiyafuatilia kwa shauku na umakini mkubwa.
Kulifungia gazeti wakati huo hatuoni kama ilikuwa kwa masilahi ya taifa kwa sababu hatua hiyo iliichafua taswira ya nchi yetu na bila shaka Rais Kikwete alijikuta katika wakati mgumu kila alipoulizwa kuhusu hatua hiyo iliyochukuliwa na Serikali yake.
Ni habari zipi zilizolipeleka gazeti hili kifungoni? Habari ya kwanza ilikuwa juu ya waraka kuhusu mishahara mipya ya watumishi wa Serikali ambayo tuliithibitisha pasipo kuacha shaka yoyote kutoka katika vyanzo vyetu vya habari vya kuaminika katika mamlaka za juu serikalini.

HOTUBA ZA BABA WA TAIFA SASA KUPATIKANA KIGANJANI

11_d1a97.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiki akisisitiza jambo wakati wa uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree jana. Ili kuweza kupata hotuba za maneno na picha za video unatakiwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678, pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumia www.simu.tv/nyerere mobile tv. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Push Media Mobile Freddie Manento
22_c78fe.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Push Media Mobile, Freddie Manento (katikati) akifafanua jambo kuhusiana na mpango wa kumuenzi marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kupata hotuba zake mbali mbali kwa njia ya simu ya mkononi. Kushoto ni msaidizi maalum wa mkurugenzi mtendaji wa Taasisi mwalimu Nyerere, Gallus Abedi na kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku.
33_5bf0a.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Push Media Mobile, Freddie Manento (kushoto) na Mkurugenzi wa Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku wakibadilisha mkataba mara baada ya kusainiwa katika hafla ya uzinduzi wa huduma ya kupata hotuba za Marehemu baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika kwenye hotel ya Double Tree. Huduma hiyo inamwezesha mwananchi kupata hotuba mbali mbali mbali za marehemu Baba wa Taifa kwa kutuma neno Hotuba kwenda namba 15678. Pia unaweza kupata huduma hiyo kwa kutumiawww.simu.tv/nyerere mobile tv.

BARTON : FERGUSON ALIKUWA HANA UWEZO WA KUPANGA HATA KONI


joey-barton_2698492b_331ce.jpg
Kiungo mtukutu wa Queens Park Rangers Joey Barton ameibuka tena kwenye vichwa vya vyombo vya habari baada ya kudai kocha wa zamani wa Manchester Utd Sir Alex Ferguso hakuwa na uwezo wa kufundisha,
Barton alidai nchini England mameneja wanathaminiwa sana kuliko makocha.
'Sina maana ya kutomuheshimu Sir Alex Ferguson - alikuwa meneja mkubwa lakini hakuwa na uwezo wa kufundisha,
sidhani kama alikuwa na uwezo wa kupanga hata koni. Kuna tofauti kubwa kati ya kocha na meneja'.
Barton pia amesema hakubaliani na wazo la kuundwa kwa tume ya kutafuta njia bora ya kuendeleza soka nchini England.
Akizungumza katika kilele cha mkutano wa Viongozi wa vilabu (Leaders in Sports ) uliofanyika kwenye uwanja wa Stamford Bridge , alisema: 'Timu ya taifa ya England ni mbovu na haiwezi kufanya vizuri hata kama itafuzu fainali za kombe la dunia mwakani nchini Brazil.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...