Saturday, October 28, 2017

TAZAMA PICHA ZA MAFURIKO YALIYOATHIRI MAKAZI YA WATU DAR ES SALAAM

Mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha maeneo mengi pwani ya Tanzania imesababisha mafuriko na uharibifu mkubwa.

Katika eneo la Mji Mpya, Kawe, nyumba zimebomoka na baadhi ya maeneo hayapitiki. Nyumba zaidi ya 20 zimeharibiwa vibaya na mafuriko.

Hizi hapa ni baadhi ya picha za hali ilivyo mtaani humo.

WALIOMUINGIZA MTU MWEUSI KWENYE JENEZA AKIWA HAI WAFUNGWA

Wakulima wawili wa Afrika Kusini waliomlazimisha mtu mweusi kuingia katika jeneza akiwa hai wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela.

Theo Martins na Willem Oosthuizen walihukumiwa mnamo mwezi Agosti kwa jaribio la mauaji na utekaji nyara.

Walimtuhumu Victor Mlotshwa kwa kupita katika ardhi, wakamshambulia na kumlazimisha kuingia katika jeneza na kutishia kumchoma akiwa hai.


Kesi hiyo ilizua hisia nchini Afrika Kusini na kuangazia wasiwasi wa ubaguzi wa rangi katika jamii kadhaa za wakulima.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...