Sunday, October 08, 2017

KIM JONG-UN AMPANDISHA CHEO DADA YAKE

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, amempandisha cheo dada yake mdogo, na kumpa madaraka zaidi katika chama tawala cha wafanyakazi.

Kim Yo-jong, anayeaminika kuwa na umri wa zaidi ya miaka 26 amekuwa mjumbe katika kamati kuu ya chama, ambalo ni baraza kuu la uamuzi linalojulikana kama politburo.

Bi Kim Yo-jong alipewa kwanza wadhifa wa kuwa afisa wa wa cheo cha juu wa chama, miaka mitatu iliyopita.

Familia ya Kim, imeongoza Korea Kaskazini, tangu nchi hiyo ilipoundwa, mwaka wa 1948.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 08, 2017 YA MICHEZO, DINI NA HARDNEWS





POLISI YADAI PANYA NDIO WALIOKULA MADAWA YA KULEVYA YALIYOKAMATWA

Police katika mji wa Mumbai nchini India wanawalaumu panya kwa kutoweka kwa kilo 34 za dawa za kulevya kwa jina Ketamine.

Wanasema wanawatuhumu panya hao kwamba ndio wa kulaumiwa baada ya kupata mabagi hayo yalitobolewa kwa chini.

Uchunguzi wa miaka mitatu umekamilika kwamba iwapo ingekuwa binadamu wangechukua mabagi yote.

Dawa hizo zilizohifadhiwa katika ghala moja la serikali zilikuwa miongoni mwa kilo 200 za mihadarati zilizopatikana na walanguzi wa mihadarati 2011.

Hii sio mara ya kwanza kwa maafisa wa polisi nchini India kuwalaumu panya kwa kutoweka kwa mihadarati iliokamatwa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...