Saturday, January 07, 2017

KLABU YA MBOWE YAZAMISHWA RASMI

nhc 
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kubomoa jengo la iliyokuwa Klabu Bilicanas na ofisi za Free Media inayomiliki gazeti la Tanzania Daima zinazomilikiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe, lililopo makutano ya barabara ya Mkwepu na Indira Gandhi lenye kitalu namba 725-726/24 na hati namba C. T No. 186018/15 and C. T No. 186018/10. 

Ubomoaji huo ulioanza jana unafanyika wakati Mbowe ameingia katika mgogoro na NHC baada ya kampuni ya udalali ya Poster and General Traders kumtolea vyombo nje mwanzoni mwa Septemba, mwaka jana kwa kudaiwa Sh bilioni 1.2 ambayo ni deni la pango ya miaka 20.

Gazeti hili lilishuhudia ubomoaji huo ukiwa katika hatua za awali na baadhi ya vijana walionekana wakianza kuondoa vioo na vigae vilivyoezekwa katika jengo hilo wakiwa chini ya usimamizi wa walinzi.

Hata hivyo, walipoulizwa watu waliokuwa wakisimamia katika eneo hilo walidai kuwa ubomoaji huo ni wa kawaida na ulipangwa kufanyika muda mrefu na endapo waandishi watahitaji maelezo wawasiliane na uogozi wa NHC.

NANA AKUFO ADDO AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA GHANA

Nana Akufo-Addo akila kiapo wakati akiapishwa 
 
Viongozi kadha wa Afrika leo wamekusanyika katika mji mkuu wa Ghana, Accra, kuhudhuria sherehe za kutawazwa rais mpya, Nana Akufo Addo.

Maelfu ya wageni walialikwa kwenye sherehe katika Medani ya Uhuru mjini Accra. Bwana Akufo Addo, aliyewahi kuwa wakili wa haki za kibinaadamu, alimshinda Rais John Dramani Mahama, katika uchaguzi wa mwezi uliopita.
Madaraka yanakabidhiwa kwa kiongozi mwengine kwa salama, jambo linaloonekana kuwa mfano mwema wa demokrasi Afrika ambako katika baadhi ya nchi, viongozi hawataki kun'gatuka.

Baada ya kuapishwa kwa rais, sasa viongozi waliohudhuria sherehe hiyo, watajadili namna ya kuhakikisha kuwa Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, anaondoka madarakani. Kiongozi huyo amekataa kustaafu ingawa alishindwa katika uchaguzi wa Mwezi Disemba.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...