Saturday, June 15, 2013

HAWA NI MAJERUHI WA MLIPUKO WA BOMU MKUTANI WA CHADEMA WAKIPATIWA HUDUMA YA KWANZA KATIKA HOSPITAL YA MOUNT MERU

MADAKTARI NA WAUGUZI WAKITOA HUDUMA YA KWANZA KWA WATU WANAODAIWA KUATHIRIKA KATIKA MLUPUKO WA KITU KIN
ACHODHANIWA KUWA NI BOMU BAADA YA KUJERUHIWA WAKATI WAKIWA KATIKA MKUTANO WA CHADEMA JIJINI ARUSHA ENEO LA SOWETO.
Majeruhi. Mungu urehemu tz

JOH MAKINI ALAZWA SINZA PALESTINA, HII NDIO MESEJI YAKE

Moja ya rapper memba wa kikundi cha hip hop TZ, Joh Makini, yuko hospitali huku akiomba tumuombee na kusema yuko katika hali ya kawaida na si mbaya sana.
 

POLISI WAMTIA MBARONI MAMA ALIYEMTUPA MTOTO BAADA YA BABA WA MTOTO KUMKANA KISA ANA NYWELE ZA KIARABU



Binti mmoja aliyefahamika kwa jina la Khadija Idd anashikiliwa na jeshi la polisi mkoani Morogoro akidaiwa kumtupa barabarani mtoto wake mwenye umri wa miezi 6 baada ya mwanaume aliyezaa naye kumkataa.

Shuhuda wetu ambaye ni dereva wa bodaboda aliyefahamika kwa jina la Shabani, alisema tukio hilo lilitokea Juni 11, mwaka huu maeneo ya Mafiga karibu na Msikiti wa Mahita ambapo Khadija alichukua uamuzi huo baada ya mwanaume aliyezaa naye kumgomea mtoto kwa madai ana nywele za Kiarabu hivyo si wake.


“Huyu dada alifika kwenye kijiwe chetu akiwa amembeba mtoto mgongoni na kukodi pikipiki ili nimpeleke mjini.

“Tulipofika kwenye msitu uliopo karibu na mashamba ya SUA, aliniambia niendeshe spidi kuna mtu anamuwahi.

Nilitii amri lakini tulipofika mbele kidogo nikashangaa anamtupa yule mtoto.

RAIS OBAMA AHAIRISHA ZIARA YAKE YA KUZITEMBELEA NCHI ZA AFRICA IKIWEMO TANZANIA...!!!


WAKATI Serikali ya Tanzania ikiendelea na maandalizi ya kupokea msafara wa watu 700 waliotarajia kuingia nchini kwa ziara ya Rais wa Marekani Barack Obama, Rais huyo amesitisha safari yake.
 
Ikulu ya Marekani imetangaza kwamba msafara wa Rais Obama kuja kutembelea Bara la Afrika haitakuwepo tena,baada ya serikali ya nchi hiyo kukosa fedha itakayoweza kugaramia safari ya Rais huyo.

Taarifa iliyonaswa na kutoka katika mitandao mbalimnali  nchini Uingereza na Marekani  zinaeleza kwamba mbali na suala la bajeti ya Rais huyo kuja nchini Tanzania kuwa kubwa pia kamati ya sheria ,ulinzi na usalama wa Marekani imeshindwa kuthibitisha juu ya suala la ulinzi na Usalama wa Rais Obama katika kipindi chote atakachokuwa nchini Tanzania pamoja na baadhi ya nchi Barani Afrika.
 
Taarifa hiyo pia ilieleza kwamba msafara wa Rais Obama unahitaji maandalizi ya kutosha kwa sababu ni msafara unaohusisha watu wengi pamoja na vyombo mbalimbali vya ulinzi ikiwemo wanyama.
 
Msemaji wa Ikulu ya Marekani alisema kwamba serikali ilijaribu kuangalia uwezekano wa Rais Obama kuja Tanzania na baadaye kutembelea Senegel pamoja na Afrika Kusini ambapo alitakiwa kukaa Tanzania kwa saa mbili tu lakini gharama za ulinzi imekuwa kubwa sana.
Katika msafara wa Obama inatakiwa kuwe na ndege mbili za mwendo kasi, kwa ajili ya kulinda ndege ya Rais,iwepo ndege za askari wa majini zinazotembea kwenye meli habarini, iwepo pea maalum za magari zitakazo sushwa katika nchi zote tatu mapema kwa kutumia ndege za jeshi kwa ajili kuimarisha ulinzi kabla ya Rais kutua katika nchi hizo" alisema Mseaji wa Ikulu ya marekani Josh Earnest.

Nakala ya taarifa hiyo  pia ilimkariri msemaji huyo wa Ikulu ya Marekani akisema kwamba pia katika msafari huo ni lazima iwe na vifaa maalum vya kutolea matibabu katika kipindi chote cha ziara ya Rais, lazima pia iwe na chombo maalum kwa ajili ya waandishi mbalimbali wa habari pamoja na vyombo vingine vya usalama kwa ajili ya kutoa taarifa ya safari ya Rais ,pamoja ndege zitakazokuwa zikizunguka kuangalia hali ya usalama katika hoteli zote atakapo kuwa ana alala Rais Obama na msafara wake.
 
Taarifa hiyo ilifafanua kwamba safari hiyo ndiyo safari kubwa kuliko aliyowahi kuifanya Barani Afrika ambapo alifika nchini Ghana, tangu alipochaguliwa kuwa Rais wa Marekani mwaka 2009 ambapo inakadiriwa kuwa itachukua kati ya dola za marekani 60 million sawa na tsh bilioni 96,000,000,000 na dola 100 milion sawa tsh bilioni 160,000,000,000.

LOWASSA ATANGAZA NDOTO YAKE, ISOME HAPA

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa akiwapungia mkono walimu walioshiriki katika hafla ya harambee ya kuchangia Saccos ya walimu iliyofanyika kwenye Viwanja vya Chuo cha Ushirika Moshi, jana. Picha na Dionis Nyato. 
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amesema kuwa ana ndoto kwamba siku moja sekta ya elimu itapewa kipaumbele cha kwanza nchini na kuzikomboa rasilimali za taifa la Tanzania zinazowanufaisha wageni na kuacha wananchi wakiambulia faida kidogo.Huku akimtaja Dk Martin Luther King aliyekuwa mwanaharakati wa haki za Wamarekani weusi aliyefariki kabla ya kuuona utimilifu wa ndoto yake, Lowassa alisema kuwa anamwomba Mungu asimwondoe duniani ili aweze kushiriki kuifanya ndoto hiyo kuwa kweli itakayokamilika siku si nyingi ambapo viongozi watakubali kuwa elimu bora ndiyo itakayowasaidia Watanzania kuchimba madini yao na kuyauza kwa faida duniani. 
Akizungumza wakati wa kuchangia SACCOS ya walimu ya Moshi Vijijini, Ushirika wa Stadium jana, Lowassa alisema kuwa katika ndoto yake anawaona viongozi wakikubali kwamba elimu bora ndiyo italisaidia taifa kuumiliki utalii na kunufaika nao, badala ya kuwaachia wageni wanufaike nao, huku Watanzania tukiambulia makombo.Wakati Lowassa akieleza ndoto yake hiyo, Mwenyekiti wa TLP na mbunge wa Vunjo Augustine Mrema amesema: “Biashara ya urais imenishinda namwachia Lowassa kwani mimi nimeamua kurudi kwenye biashara ya rejareja.”

MSANII WA VICHEKESHO MASELE APATA AJALI YA GARI...!!!

 


Habari za uhakika ni kuwa muigizaji wa vichekesho hapa nchini maarufukwa jina la ''Masele cha Pombe'' ni mzima wa afya na hajafariki kamabaadhi ya tetesi zilivyoanza
kuenea kwa kasi.tetesi kuwaMasele amepata ajali ya gari
maeneo ya barabara ya 14 jijini Tanga, Wasanii wenzake walipatwa na mshtuko mkubwa, ilibidi kundi zima la VITUKO SHOW litie tim Eneo la tukio na kumkuta masele mzima wa afya,Ukweli ni kwamba masele 
alimgonga mtu baada ya kumgonga mtu
alisogeza gari mbele ili apaki aongee na raia mara gafla mawe yakaanza kurushwa na watu asiowatambua! kwa kuokoa uhai

wake akawasha gari na kuwatoka raia wenye hasira kali mara akajikuta amemgonga mtu mwingine ambaye kwa bahati nzuri hakuumia, pale ndipo raia walivamia gari la masele na kulipiga mawe wakapora simu hela na baadi ya vitu vilivyokuwemo kwenye gari ilifikia hatua mtu mmoja asiejulikana alichoma kisu tairi la gari la masele na kulitoboa toboa!
 wengine walipiga mawe kioo pamoja na taa za nyuma, na kutaka
kumuua. Jeshi la police lilitia tim eneo la tukio na kumchukua masele mpaka kituo cha police Mabawa, Mpaka sasa masele yuko poa.

MREMA AKABIDHI URAIS KWA LOWASSA MWAKA 2015...!!!


Augustine Mrema (kushoto) na Edward Lowassa.
Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema amesema biashara ya kugombea urais mwaka 2015 haiwezi kamwe na ametaka ifanywe na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Mrema alisema hayo jana kabla ya harambee ya Saccos ya Walimu wa Wilaya ya Moshi Vijijini, iliyoongozwa na Lowassa katika uwanja wa Ushirika mjini hapa.
Alisema kugombea urais mwaka 2015 ni biashara kubwa kwake kwani amezoea kufanya biashara ndogo ya rejareja yaani ubunge na kumwomba Mungu mwaka huo ufike kwani atakuwa tayari kumwunga mkono Lowassa kwenye kinyang’anyiro hicho.
‘’Nasema biashara ya urais ni biashara kubwa kwangu kwa sasa na biashara hiyo namwachia Lowassa na niko tayari kumwunga mkono kwa hali na mali,’’ alisema Mrema

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI TAREHE 15.06.2013

.
.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...