Saturday, June 15, 2013

MSANII WA VICHEKESHO MASELE APATA AJALI YA GARI...!!!

 


Habari za uhakika ni kuwa muigizaji wa vichekesho hapa nchini maarufukwa jina la ''Masele cha Pombe'' ni mzima wa afya na hajafariki kamabaadhi ya tetesi zilivyoanza
kuenea kwa kasi.tetesi kuwaMasele amepata ajali ya gari
maeneo ya barabara ya 14 jijini Tanga, Wasanii wenzake walipatwa na mshtuko mkubwa, ilibidi kundi zima la VITUKO SHOW litie tim Eneo la tukio na kumkuta masele mzima wa afya,Ukweli ni kwamba masele 
alimgonga mtu baada ya kumgonga mtu
alisogeza gari mbele ili apaki aongee na raia mara gafla mawe yakaanza kurushwa na watu asiowatambua! kwa kuokoa uhai

wake akawasha gari na kuwatoka raia wenye hasira kali mara akajikuta amemgonga mtu mwingine ambaye kwa bahati nzuri hakuumia, pale ndipo raia walivamia gari la masele na kulipiga mawe wakapora simu hela na baadi ya vitu vilivyokuwemo kwenye gari ilifikia hatua mtu mmoja asiejulikana alichoma kisu tairi la gari la masele na kulitoboa toboa!
 wengine walipiga mawe kioo pamoja na taa za nyuma, na kutaka
kumuua. Jeshi la police lilitia tim eneo la tukio na kumchukua masele mpaka kituo cha police Mabawa, Mpaka sasa masele yuko poa.
.
































 Taa iliovunjwa hio



 Mwene No Disc

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...