Saturday, April 30, 2016

WAZIRI MKUU "TUTAUFANYIA KAZI USHAURI WA WAZIRI MKUU"

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeupokea na itaufanyia kazi ushauri wa Mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe aliyetaka Benki ya Standard ICBC ya Uingereza na kampuni dada ya Stanbic Tanzania kuchunguzwa juu ya mkopo wa hatifungani wa Sh1.2 trilioni ambao umegubikwa na ufisadi.

Zitto alitoa kauli hiyo juzi wakati akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais-Tamisemi na Utawala Bora mwaka 2016/17 na kutaka Bunge liunde kamati teule kuchunguza suala hilo na ukweli ukibainika, Serikali itakwepa kulipa deni la Sh2 trilioni ambazo Tanzania inatakiwa kulipa ikiwa ni deni na riba.

Majaliwa alitoa kauli hiyo jana mjini Dodoma baada ya kuulizwa swali na waandishi wa habari juu na hatua ambazo Serikali imezichukua kutokana na sakata hilo linalodaiwa kuwa na harufu ya ufisadi, kwamba baada ya uchunguzi kukamilika taarifa itatolewa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...