Monday, April 30, 2018

MBUNGE CHADEMA ALALAMIKIA VITI BUNGENI, ADAI KUFINYWA MAKALIO

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) ameomba mwongozo bungeni akitaka viti vya bungeni kukarabatiwa kwa kuwa viti hivyo ni vibovu.

“Ni lini serikali itakarabati viti hivi, hiki nilichokalia leo asubuhi kimenifinya makalio,“ alihoji Selasini.

Salasini ameyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma, wakati wa kipindi cha Maswali na majibu huku akiitaka serikali itoe majibu ni lini viti hivyo vitakarabatiwa.

Aidha Mbunge huyo baada ya kuhoji amesema kuwa kiti alichokalia leo katika bunge hilo kimemfinya makalio. Sambamba na kuomba muongozo huo Spika Ngudai amesema kuwa suala hilo limepokea na litatolewa ufafanuzi.

MAJIBU YA RAIS MAGUFULI KWA WANAOBEZA NCHI KUKOPA

Rais John Magufuli amesema Serikali itaendelea kukopa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, hata kama kuna watu wanabeza.

Amesema fedha hukopwa kwa masharti nafuu, riba ndogo na hulipwa kwa muda mrefu na kwamba fedha hizo ndizo hutumika kujenga miundombinu kama barabara ili kuchochea uchumi.

Rais alisema hayo jana mjini Iringa alipofungua barabara ya lami ya Iringa – Migoli – Fufu yenye urefu wa kilomita 189 inayounganisha mikoa ya Iringa na Dodoma. Tukio hilo lilirushwa hewani moja kwa moja na kituo cha televisheni cha TBC 1.

Barabara hiyo iliyojengwa kwa gharama ya Sh207.4 bilioni ni sehemu ya barabara kuu ya kuanzia Cape Town, Afrika Kusini hadi Cairo nchini Misri.

Imejengwa kwa ufadhili wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) kwa asilimia 65.9, Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (Jica) kwa asilimia 21.3 na Serikali ya Tanzania asilimia 12.8.

“Msiwasikilize wanaosema Serikali ina madeni makubwa wakati wao wenyewe wanapita kwenda bungeni kwenye barabarani tulizozijenga kwa kukopa,” alisema.

Magufuli alisema Serikali imekuwa ikidaiwa tangu enzi za mkoloni, lakini madeni mengine yamekuja kulipwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete.

Akizungumzia barabara hiyo, Rais alisema inalenga la kuimarisha utalii katika ukanda wa kusini.

“Watu walizoea (kwamba) ukitaka kutalii ni lazima uende Serengeti wakati Ruaha ni mbuga kubwa yenye vivutio bora, lakini haikutembelewa na watalii kwa sababu ya ukosefu wa barabara,” alisema.

“Kwa sasa itabidi wenzetu wa kaskazini wasubiri kwanza. Kwa sasa tunaendeleza maeneo yaliyochelewa kuendelezwa,” alisema.

Rais Magufuli alisema Uwanja wa Ndege wa Nduli uliopo Iringa utaimarishwa ili watalii waweze kufika maeneo ya utalii.

Rais Magufuli alisema barabara hiyo pia itawasaidia wakazi wa Iringa kusafirisha mazao kwenda sokoni bila matatizo.

“Barabara hii iwe mkombozi wa maisha yetu. Tuitunze, itasafirisha mazao, mtasafiri kwa utulivu kwenda kwenye shughuli zenu,” alisema.

Magufuli ambaye alisoma Shule ya Sekondari Mkwawa mkoani Iringa kuanzia mwaka 1978/79, alisema anakumbuka hali ya barabara ilivyokuwa tatizo wakati huo.

“Kutoka Dodoma hadi Iringa nilitumia siku mbili kwa kutumia basi la Shirika la Reli Tanzania. Tulilala njiani kwa sababu ya ubovu wa barabara,” alisema.

MCHUNGAJI KKKT ADAI KUNA UBABE KATIKA KANISA HILO

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kigogo, Richard Hananja amedai kuna ubabe katika kanisa hilo.

Hata hivyo, amesema licha ya kanisa hilo kupitia mambo mengi anaamini litaendelea kusimama imara hasa katika kipindi hiki.

Mchungaji Hananja amesema hayo Aprili 29, 2018 alipozungumza na Mwananchi kuhusu baraza la maaskofu wa KKKT ‘kuwatenga’ maaskofu watatu kwa kutosoma waraka wa ujumbe wa Pasaka kwenye dayosisi zao.

SERENGETI BOYS MABINGWA WA CECAFA

Timu ya Tanzania ya vijana wasiozidi umri wa miaka 17 Serengeti Boys ndio mabingwa wa Kombe la Vijana la mataifa ya Afrika Mashariki na Kati Cecafa wa mwaka 2018.

Serengeti Boys walitwaa ubingwa baada ya kuwalaza Somalia mabao 2-0 katika mechi ya fainali iliyochezewa mjini Bujumbura, Burundi. Mabao ya Serengeti yalitiwa kimiani na Edson Jeremiah na Japhary Mtoo.

Ushindi huo ndio wa kwanza tangu kuanzishwa kwa michuano hiyo mwaka 2007 na unatarajiwa kuwatia moyo vijana hao wanapijiandaa kushindi michuano ya Kombe la Vijana Mabingwa Afrika mwaka 2019.

Sunday, April 29, 2018

SERIKALI YAINGILIA KATI MATIBABU YA MZEE MAJUTO, SASA KUPELEKWA INDIA, WADAU NAO WAJITOKEZA

Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) jana Aprili 28, 2018 amemtembelea msanii nguli wa filamu Bw. Amri Athumani (Mzee Majuto) ambaye alikuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Tumaini, Dar es Salaam. 

Dkt. Mwakyembe akizungumza katika tukio hilo amesema Serikali imeamua kumpeleka Mzee Majuto nchini India kwa ajili kupata matibabu zaidi. 


"Kwa kuanzia tumeamua kumuhamishia Mzee Majuto katika hospitali ya Muhimbili ili kukamilisha maandalizi muhimu ya kiafya kabla ya safari ya kuelekea India", alisema Dkt. Mwakyembe.

Thursday, April 26, 2018

NENO LA MIZENGO PINDA KUHUSU WATU WAOFANYA VURUGU NCHINI

Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Kayanza Peter Pinda.
Hii ilikua Juni 20, 2013, akizungumza katika Kipindi cha Maswali ya Papo kwa Hapo kwa Waziri Mkuu, bungeni Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa Kilwa Kaskazini Murtaza Mangungu .

Mh. Pinda alisema “Ukifanya fujo umeambiwa usifanye hiki ukaamua wewe kukaidi utapigwa tu maana hakuna namna nyingine maana wote lazima tukubaliane nchi hii tunaiendesha kwa misingi ya kisheria sasa kama wewe umekaidi hutaki unaona kwamba ni imara zaidi, wewe ndio jeuri zaidi watakupiga tu na mimi nasema muwapige tu, kwa sababu hakuna namna nyingine maana tumechoka sasa”.

HISTORIA YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR


Mkataba wa Muungano ulitiwa saini na Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume, Aprili 22, 1964, Zanzibar.
Ulithibitishwa na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi Aprili 26, 1964, na Aprili 27, 1964 viongozi hao walikutana katika ukumbi wa Karimjee, jijini Dar es Dalaam kubadilishana hati za Muungano.


Sheria za Muungano ilitamka kwamba, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar zililazimika, kuwa dola ya Jamhuri kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jina ambalo lilibadilishwa Oktoba 28, 1964 na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupitia sheria ya Jamhuri ya Muungano, sheria namba 61, ya mwaka 1964.

Wednesday, April 25, 2018

ALICHOSEMA KAMANDA WA POLISI DODOMA KUHUSU MAANDAMANO YA KESHO

Bofya hapo chini upate kusikiliza kauli ya kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Gilles Muroto kuhusu maandamano ya kesho. Usisahau ku-subscribe, kulike na kucomment.

Thursday, April 19, 2018

BABU SEYA NA WANAE WATINGA BUNGENI LEO

Mwanamuziki nguli wa dansi, Nguza Viking ‘Babu Seya’ na watoto wake ambao ni Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ na Francis Nguza, leo Aprili 19, 2018 wametembelea Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Dodoma baada ya kualikwa na Mbunge wa Viti Maalum CCM, Mariam Ditopile.

Babu Seya na familia yake, walishangiliwa na Bunge zima baada ya kutambulishwa na Spika wa Bunge, Job Ndugai, baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika bungeni humo.

Wanamuziki hao walikuwa ni miongoni mwa wafungwa 8,157 waliosamehewa na Rais John Magufuli siku ya maadhimisho ya sherehe za uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 2017 zilizofanyika mjini Dodoma.

MSUKUMA 'LEMA SASA HIVI KIDOGO AMEKUWA BINADAMU'

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Msukuma, amemuomba Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi, kupeleka bungeni muswada  kubadilisha sheria ili makosa ambayo hayastahili mtu kufungwa apewe adhabu ndogo ili kuondoa msongamano katika magereza.

Pia mbunge huyo aliwataka baadhi ya wabunge waache kupiga kelele bungeni juu ya matukio ya watu kupotea na kutekwa, badala yake waviache vyombo vya sheria na vya usalama vifanye kazi yake.

Hayo ameyasema Bungeni wakati akichangia hoja katika Wizara ya Katiba na Sheria jana, Aprili 18, 2018.

PICHA ZA HARUSI YA ALIKIBA ILIYOFANYIKA MOMBASA



 Baada ya ukimya na usiri wa muda mrefu kuhusu mahusiano yake ya kimapenzi hatimae leo April 19, 2018 Ali kiba amefunga ndoa katika msikiti wa Ummul Kulthum Mombasa nchini Kenya akiwa ameozeshwa na sheikh Mohammed Kagera.


Alikiba  amemuoa Amina Khalef Ahmed mkazi wa Mombasa ambapo ndipo sherehe za harusi hiyo zinafanyika hii leo huku sherehe nyingine kubwa ikitarajiwa kufanyika April 29, 2018 jijini Dar es Salaam.

Sunday, April 08, 2018

WADAU WA USAFIRI TABORA WATAKA MADEREVA WA MAGARI YA MIZIGO KUBANWA

Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora na Wadaau wa Usafiri wamependekeza uanzishwaji wa matumizi ya vitabu (log book) kwa magari ya mizigo ili kudhibiti madereva kusafiri mwendo mrefu bila kupumzika na hivyo kusababisha ajali kwa magari yao au kugongana uso kwa uso na magari mengine kutokana na uchovu.

Tamko hilo limetolewa jana wilayani Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri mara baada ya kikao cha kujitathimini kwa ajili ya kuja na majibu ya kuondoa ajali za barabarani mkoani humo.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema vitabu hivyo vitasaidia kuonyesha muda alitoka , mahali alitoka na kama amesafiri muda mrefu atalazimisha apumzike ili kuepusha ajali.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRIL 08, 2018 YA DINI, MICHEZO NA HARDNEWS


TUCTA YAWALILIA WATUMISHI DARASA LA SABA YATAKA WARUDISHWE KAZINI

Baraza Kuu la Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA ) jana Jumamosi Aprili 7, 2018 limetoa tamko lenye mambo saba, likiwemo la kupinga uamuzi wa Serikali kuwafuta kazi watumishi wake wenye elimu ya darasa la saba.

Akisoma tamko hilo mbele ya wajumbe wa baraza kuu la TUCTA katika mkutano wa baraza hilo uliofanyika mkoani Morogoro mwenyekiti wa TUCTA, Tumaini Nyamhokya amesema uamuzi huo wa Serikali si sahihi na hivyo wametaka watumishi hao kurejeshwa kazini.

Amesema baraza limesikitishwa na uamuzi wa kuwaondoa kazini watumishi wa umma na taasisi zinazopokea ruzuku kutoka serikalini.

Saturday, April 07, 2018

MAGUFULI APIGA MARUFUKU ASKARI NA VIONGOZI KUFYEKA NA KUCHOMA MASHAMBA YA BANGI

Rais Magufuli amepiga marufuku askari wa jeshi la polisi, na viongozi wote wa serikali wakiwemo mawaziri, wakuu wa mikoa na makatibu wakuu kujishughulisha na kazi ya uchomaji na uteketezaji wa mashamba ya bangi na badala yake ameiagiza polisi kuwatumia wanakijiji kufanya kazi hiyo.
Hi
Ametoa agizo hilo leo wakati akihutubia wananchi katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha baada ya uzinduzi wa nyumba za askari na kushuhudia maonesho ya utayari ya jeshi hilo katika kukabiliana na uhalifu.
“Kama bangi imelimwa karibu na kijiji, shika kijiji kizima, kuanzia wazee, wamama mpaka watoto ndiyo wakafyeke hilo shamba, maaskari wangu hawakuajiriwa kufyeka mashamba ya bangi.… Usiwatume maaskari wako kufyeka bangi, mwisho wataumwa nyoka mule, mmevaa sare nzuri halafu mnafyeka bangi, mnaaibisha jeshi”, alisema Rais Magufuli

Rais amesema wanaolima bangi wakikamatwa ndio wanaotakiwa kuzifyeka.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 07, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS




ALIEVUMBUA MADINI YA TANZANITE APEWA MILLION 100 NA RAIS MAGUFULI

Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua dini la Tanzanite mwaka 1967.  
Jumanne Mhero Ngoma mvumbuzi wa madini ya Tanzanite.

Rais Dr. John Pombe Magufuli jana amezindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite huko Mererani mkoani Arusha ambapo katika uzinduzi huo alitambua uwepo wa mvumbuzi wa kwanza wa madini ya Tanzanite ambaye hakuwahi kutambuliwa na taifa.
Bwana Jumanne Mhero Ngoma alivumbua aina hiyo ya dini la Tanzanite mwaka 1967. Jumannne Ngoma ametambuliwa na Rais Magufuli na amemzawadia shujaa huyo milioni 100 kwa ajili ya kumsaidia kujikimu na matibabu baada ya mzee huyo kupooza sehemu ya mwili.

Rais Magufuli aliwahakikisha wachimbaji wadogo kwamba atawajengea 'mazingira ili kusudi wafaidi na Tanzanite zaidi'

Tanaznite ni madini ambayo ni ya kipekee kwa Tanzania haipatikani sehemu yeyote duniani. Mauzo ya Tanzanite duniani yanafikia dola za Marekani milioni 50. Tanzanite ni jiwe yenye miaka milioni mia 6 na iligundulika Mererani, Arsuha, kaskazini mwa Tanzania, mwaka 1967. Inasemekana kuwa na upekee hata ziadi ya alhmasi.

MAAJABU: JAMAA ATOLEWA MSWAKI TUMBONI

Mswaki 
Madaktari katika Hospitali Kuu ya Mkoa ya Pwani (CPGH) mjini Mombasa, Kenya wamefanikiwa kuutoa mswaki ambao ulikuwa umekwama tumboni mwa mwanamume mmoja kwa siku sita.

David Charo alikuwa akipiga mswaki alipoumeza kimakosa Jumapili wiki iliyopita apokuwa anajiandaa kwenda kazini Bamba, Kilifi. Kufikia jana, alikuwa ameanza kupata matatizo ya kupumua.
 Davis Charo 
Awali, madaktari walikuwa wamedokeza kwamba angehitaji kufanyiwa upasuaji kuutoa. Lakini Ijumaa asubuhi, madaktari wakiondozwa na Ramadhan Omar wamefanikiwa kuutoa mswaki huo bila kumfanyia upasuaji wa kawaida.

Badala yake, wamemfanyia upasuaji wa kutumia matundu madogo. Jumapili, Charo alipokuwa alipoumeza mswaki huo kimakosa, awali ulikwama ndani ya koo kabla ya kutumbukia ndani tumboni.

MARAIS WALIOPANDISHWA KIZIMBANI NA KUHUKUMIWA KIFUNGO WIKI HII

  Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma
Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma
 
Wiki hii tumeshuhudia baadhi ya marais wastaafu wa nchi mbalimbali wakifikishwa mahakamani kusomewa mashtaka na wengine kuhukumiwa vifungo gerezani. Miongoni mwa marais hao ni:-

Rais wa zamani wa Afrika kusini Jacob Zuma amefika mahakamani kujibu mashtaka ya ulaji wa rushwa yanayohusishwa na mkataba wa ununuzi wa silaha miaka ya tisini.

Baada ya Zuma (75) kufika mbele ya Mahakama Kuu kwa dakika 15 huko Durban, kesi hiyo iliahirishwa hadi tarehe 8 mwezi Juni.

Ameshtakiwa kwa makosa kumi na sita ya ulaji wa rushwa, ufisadi, ulaghai na ulanguzi wa fedha, aliyoyaepuka wakati wa utawala wake na kurejeshwa tena mwaka 2016. Bw Zuma alitolewa madarakani kwa nguvu mwezi Februari mwaka huu.
  Rais wa zamani wa Korea Kusini Park Geuin Hye 
Rais wa zamani wa Korea Kusini Park Geuin Hye  

Aliyekuwa rais wa Korea Kusini, Park Geuin Hye, amehukumiwa kifungo cha miaka 24 jela, baada ya kupatikana na hatia ya ufisadi, iliyomuondoa madarakani.

Friday, April 06, 2018

MAKAMU WA RAIS ASIKITISHWA NA UHARIBUFU WA MAZINGIRA UNGUJA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu amesikitishwa sana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika machimbo ya mchanga Donge.

Makamu wa Rais ambaye yupo kwenye ziara Visiwani Unguja na jana alikuwa na ziara katika mkoa wa Kaskazini Unguja. Makamu wa Rais amesema hatua za haraka zichukuliwe ili kuokoa mazingira yasiendelee kuharibiwa.

Makamu wa Rais pia amewataka Viongozi wote wa CCM kuhakikisha kuwa Chama kinajitegemea kwenye maeneo yao, Makamu wa Rais aliyasema hayo mara baada ya kukagua shughuli za kiuchumi za CCM katika ufukwe wa Nungwi ikiwa sehemu ya ziara yake aliyoifanya kwenye mkoa wa Kaskazini Unguja.

Makamu wa Rais pia alifungua ofisi mbili za CCM moja ikiwa ya jimbo la Donge na nyingine ikiwa Ofisi ya CCM mkoa wa Kaskazini ambapo inahistoria ya kipekee kutokana na kuwekwa jiwe la msingi mwaka 1986 na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

MBUNGE WA CHADEMA AISHAURI SERIKALI KUFUTA VYAMA VYA UPINZANI, MWIGULU AMJIBU

Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Cecilia Pareso.

Mbunge wa Viti Maalum Chadema, Cecilia Pareso amesema kama serikali ina lengo la kuwabana na kuwanyima haki wapinzani, basi ni bora mfumo wa vyama vingi ukafutwa ili ifahamike kwamba nchi ni ya chama kimoja.

Pareso ameyasema hayo jana Aprili 5, Bungeni Mjini Dodoma wakati akichangia katika Mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Ofisi ya Waziri Mkuu mwaka 2018/19 huku akidai kwamba vyama vya upinzani vimekuwa vikionewa ikiwemo viongozi wake kukamatwa mara kwa mara na kufunguliwa mashtaka huku wengine wakifungwa jela. 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt. Mwigulu Nchemba.

Amesema vyama hivyo vimekuwa ni adui mwingine kwa kuwa kwa sasa vinapigwa vita na Serikali iliyopo madarakani, kuzuiwa kufanya shughuli za siasa majukwaani.

Pia alidai chaguzi ndogo zilizofanyika hivi karibuni, zilikuwa ni kati ya Chadema na Jeshi la Polisi na kudai kwamba wabunge na madiwani walinunuliwa, wakahama vyama vyao, hivyo kukalazimika kufanyika chaguzi nyingine ndogo alizodai zimegharimu zaidi ya Sh bilioni 6.

UKUTA WA MADINI YA TANZANITE KUZINDULIWA LEO

 Rais wa jamuhuri ya muungao wa Tanzania Dr. John Magufuli, leo anatarajia kuzindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite, iliopo eneo la Mererani, mkoani Arusha.

Ukuta huo wenye urefu wa kilomita 24.5 na urefu wa mita tatu kwenda juu, umejengwa kufuatia agizo lililotolewa na Rais John Magufuli, kama jitihada za kudhibiti na kuzuia utoroshwaji wa madini hayo, ambayo yanapatikana nchini Tanzania pekee.
Mwezi Februari mwaka huu, wakuu wa vyombo vya usalama, walitembelea eneo hilo, kuukagua ukuta huo uliojengwa kwa gharama za Kitanzania isiyozidi bilioni 6. 

Walisisitiza kuwa lengo la kujengwa kwake ni kuzuia uhalifu na si kuwazuia wachimbaji wakubwa na wadogo kupata riziki zao.

Wakitoa taarifa kwa viongozi wa ulinzi, wataalamu waliojenga ukuta huo, walisema licha ya kufanikisha ujenzi huo, changamoto mbalimbali walikutana nazo ikiwemo hatari inayoukabili ukuta huo, kutokana na wachimbaji kulipua baruti, karibu na ukuta, hivyo kusababisha hatari za kuharibika haraka. Ugumu wengine walioupata ni uchimbaji katika maeneo yenye miamba.

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRIL 06, 2018 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS



SALMAN KHAN AHUKUMIWA KUFUNGWA JELA KWA KOSA LA UWINDAJI HARAMU

Mahakama nchini India imemuhukumu nyota muigizaji wa sinema za Bollywood Salman Khan, kifungo cha miaka mitano jela kwa kuua aina mojawapo ya swala ambao ni adimu kupatikana duniani mwaka 1988.

Mahakama hiyo iliyoko Jodhpur imemtoza faini ya rupia 10,000 ($154; £109) kwa kosa hilo.
Amepelekwa korokoroni na anatarajiwa kusalia huko kwa muda.

Khan aliwaua swala wawili kwa jina blackbucks, ambao hulindwa na kuhifadhiwa, Magharibi mwa jimbo la Rajasthan alipokuwa akiigiza filamu yake.

Thursday, April 05, 2018

CHADEMA WATAJA MAJINA 25 YA WAFUASI WAKE WANAOSHIKILIWA NA POLISI BILA KUPELEKWA MAHAKAMANI

Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimetoa orodha ya majina ya watu 25, wakiwemo viongozi, wanachama na wafuasi wa wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda ya Dar es Salaam na kuwaagiza wanasheria wake kuchukua hatua zaidi za kisheria kwa kuwasilisha maombi ya ‘Habeas Corpus’, Mahakama Kuu, iwapo jeshi hilo halitawaachia au kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao kama taratibu zinavyotaka.

Chama hicho kimesema kimefikia uamuzi huo, kutokana na tabia ya Jeshi la Polisi kuendeleza utaratibu unaovunja haki na sheria kwa kuwakamata watu na kuwashikilia mahabusu za Polisi kinyume na matakwa ya taratibu za nchi.

Kati ya watu hao 25 wanaoshikiliwa na Polisi, mmoja ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, John Heche, ambaye pia ni Mbunge wa Tarime Vijiji huku watu wengine 24 wakiwemo viongozi, wanachama na wafuasi wa CHADEMA waliikamatwa juzi wakiwa maeneo ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakifuatilia hatma ya dhamana ya viongozi wakuu wa chama mahakamani hapo.

BASI LA CITY BOYS LAGONGANA NA FUSO, 12 WAFARIKI, 46 WAJERUHIWA!

Basi la Kampuni ya City Boys lenye namba za usajili T983 DCE Scania limepata ajali ya kugongana na lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T486 ARB katika eneo la Makomero Tarafa na Wilaya Igunga Mkoa wa Tabora usiku wa kuamkia leo na kusababisha vifo vya watu 12 na wengine 46 kujeruhiwa.

Kaimu Mkuu wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Tabora, Insp Hardson, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni tairi la kulia la Fuso lilitumbukia kwenye mashimo mawili na kusababisha tairi kupasuka na rimu kupinda hivyo likakosa mwelekeo na kuligonga basi la City Boy uso kwa uso.

Insp Hardson amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya igunga huku baadhi ya majeruhi wakipelekwa Hospitali ya Nkinga na wengine Bugando Mwanza kwa ajili ya matibabu.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...