Thursday, April 05, 2018

BASI LA CITY BOYS LAGONGANA NA FUSO, 12 WAFARIKI, 46 WAJERUHIWA!

Basi la Kampuni ya City Boys lenye namba za usajili T983 DCE Scania limepata ajali ya kugongana na lori aina ya Fuso lenye namba za usajili T486 ARB katika eneo la Makomero Tarafa na Wilaya Igunga Mkoa wa Tabora usiku wa kuamkia leo na kusababisha vifo vya watu 12 na wengine 46 kujeruhiwa.

Kaimu Mkuu wa Usalama Barabarani wa Mkoa wa Tabora, Insp Hardson, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa chanzo cha ajali hiyo ni tairi la kulia la Fuso lilitumbukia kwenye mashimo mawili na kusababisha tairi kupasuka na rimu kupinda hivyo likakosa mwelekeo na kuligonga basi la City Boy uso kwa uso.

Insp Hardson amesema miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya igunga huku baadhi ya majeruhi wakipelekwa Hospitali ya Nkinga na wengine Bugando Mwanza kwa ajili ya matibabu.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...