Tuesday, March 07, 2017

YA MH. LISSU KAMA FILAMU VILE

Mambo yanayomtokea kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) ni kama mchezo wa kuigiza.

Jana, Lissu alianza siku kwa furaha baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu kumuona hana kesi ya kujibu, lakini dakika chache baadaye polisi walimkamata tena, kumhoji na kumuachia kwa dhamana.

Licha ya kashikashi hizo mahakamani na kituo cha polisi, Lissu ameonyesha kuwa na sakata jingine katika uchaguzi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) baada ya kudai kuwa kuna mkakati unasukwa na baadhi ya mawakili wenzake kutaka kumkwamisha asigombee urais wa chama hicho.

 Baada ya kuachiwa huru, Lissu alikamatwa na polisi akiwa Mahakama ya Kisutu na kupelekwa Kituo Kikuu cha Polisi, lakini haikueleweka sababu za kukamatwa kwake.

Lissu alikutana na polisi hao saa 4:00  asubuhi na akaambiwa kuwa anahitajika kituoni, mbunge huyo aliomba aendeshe gari lake mwenyewe ambalo alikuwa nalo Kisutu.
Wakili wake, Fredrick Kihwelo alisema: “Polisi walikubaliana naye na kuingia kwenye gari lake na kuelekea kituoni hapo na walipofika walikaa muda kisha wakaelezwa kuwa, anadaiwa kutoa matamshi yanayoweza kusababisha matatizo ya kidini.”

Alisema Lissu alidaiwa kutoa matamshi hayo akiwa mkoani Dodoma, hivyo baada ya mahojiano aliachiwa kwa dhamana na kutakiwa kuripoti kituoni hapo Machi 13.

Chanzo: Mwananchi.

VIGOGO WA ‘UNGA’ WAHOJIWA

Kazi ya kuchunguza majina 97 yaliyokabidhiwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa Kamishna wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, imeanza kufanyiwa kazi kwa vigogo watano waliotajwa kuhojiwa.

Februari 13, Makonda alimkabidhi Kamishna Mkuu wa Mamlaka hiyo, Rogers Sianga orodha ya majina 97 ikiwa ni awamu ya tatu ya watuhumiwa wa biashara ya dawa za kulevya.

Kamishna wa Intelijensia wa Mamlaka hiyo, Fredrick Kibula alisema jana kuwa wanawahoji na wanafanya uchunguzi dhidi ya watuhumiwa hao kabla ya kuwafikisha mahakamani.

“Tuna watu muhimu watano wanaotoka katika orodha ile ya mkuu wa mkoa. Tunao kwa ajili ya uchunguzi zaidi na muda ukifika tutawatajia mtawafahamu,” alisema Kamishna Kibula na kuongeza:

“Hatukamati ovyoovyo ni lazima tujiridhishe bila shaka kwamba wahusika wana sifa ya kukamatwa. Pia hatutangazi ingawa tunafanya operesheni za kiuchunguzi ambazo zinafanyika mara kwa mara.”

MAGUFULI AAGIZA TANESCO KUWAKATIA UMEME WASIOLIPA BILI

Rais wa Tanzania John Magufuli jana aliiagiza kampuni ya ugavi wa umeme nchini humo (TANESCO) kuwakatia umeme wateja wote wenye madeni makubwa kwa kampuni hiyo, ikiwemo serikali ya Zanzibar.

Akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi kwenye kituo kipya cha TANESCO mkoani Mtwara, rais Magufuli alisema kuwa tasisi zote za umma zinapaswa kulipa madeni la sivyo zitakatiwa umeme.

Alisema kuwa serikali ya Zanzibar pekee, kupitia shirika la umeme za Zanzibar (ZECO), ina deni la TANESCO kiasi cha shilingi bilioni 121 za Tanzania.

"Msiogope mnapaswa kukata huduma hii kwa taasisi yoyote ambayo hailipi bili zake. Nataka kumwambia waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kwamba umeme unapaswa kukatwa hata Ikulu. Nikilala gizani, halafu maafisa wa Ikulu ambao hawajalipa watawajibika na sio wewe. Una hakikisho langu kwa hili.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...