Monday, September 16, 2013

WAMALAWI WAMIMINIKA KATIKA OFISI ZA UHAMIAJI JIJINI DAR KWAAJILI YA KUJIORODHESHA UHALALI WA KUISHI TANZANIA


Raia wa Malawi wakiwa katika foleni ya kuingia kujiandikisha katika Idara ya Uhamiaji, Mkoa wa Dar es Salaam jana kuhusu zoezi linaloendelea la kuwatambua wahamiaji haramu jijini Dar es Salaam. Mamia ya wakazi hao walimiminia katika ofisi hizo leo kujiorodhesha ikiwa ni agizo la Rais Jakaya Kikwete.
Akina mama na watoto wakisubiri kujiorodhesha.
Ofisa wa Uhamiaji akiwaelekeza jambo Raia wa Malawi. Credits: Father Kidevu Blog

MSANII DR.CHENI ALAMBA DILI NONO ZA SIMU MPYA ZA PANTECH....!!!




Dr. Cheni   Muigizaji maarufu wa filamu Swahiliwood Muhsin Awadh(Dr.Cheni) ameteuliwa kuwa balozi wa simu mpya aina ya Pantech ambazo zimeanza kuingia nchini. Muigizaji huyo amesainishwa deal hilo la mwaka mmoja ambapo atakuwa katika matangazo na promotions za simu hizo. Akizungumza na Millardayo Dr. Cheni alisema "Simu inaitwa Pantech, ni simu mpya kabisa na ina operating system ya Android version mpya. Ukizingatia sasa hivi internet ndiyo kila kitu kwenye simu za mkononi, Pantech inatumia 4G na LTE kwenye connection ya internet. Kitu kingine kizuri ni kwamba simu hii ina uwezo wa kujichaji na nguvu za jua. Sasa jua letu hatutalichukia tena na pia ina camera nzuri ambayo inaitwa Spy camera yenye uwezo wa kupiga picha mbali sana"

Star huyo wa filamu za Nipende Monalisa, Jesica na Majanga aliendelea kwa kusema " Majukumu yangu hasa ni kuhakikisha simu hii watu wanatambua uwepo wake. Matangazo na promotion zinapofanyika nitakuwa na shiriki kikamilifu kabisa. Wamenipa mkataba wa mwaka mmoja kwa sasa na swali lako la thamani ya mkataba wangu naomba niweke kapuni kwasasa, ila millardayo.com itakuwa ya kwanza kujua thamani yake muda wa kuweka wazi ukifika. Ninachoweza kukwambia hivi sasa ni bei tu ya simu hizi ambayo ni Tsh 250,000 tu"

Wasanii wengi wakiwemo wa filamu siku hizi wanaanza kufaidi umaarufu wao baada ya kampuni mbalimbali kuanza kufanya nao kazi katika matangazo ya bidhaa zao kama mabalozi, wiki iliyopita Yobnesh Yusuph(Batuli), Rose Ndauka, Slim Omar na Single Mtambalike(Richie) walisainishwa mkataba wa kuwa mabalozi wa wa soko la hisa la Dar es salaam/ Dar es salaam Stock Exchange(DSE), King Majuto na JB ni baadhi ya wasanii wengine wa filamu ambao nao wana mikataba na makampuni katika kutangaza huduma na bidhaa za makampuni hayo. Katika mkutano na media........................

SUGU: "NDUNGAI ALIAMURU ASKARI WANIPIGE BUNGENI..."



NI kauli iliyotolewa na Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’
 Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amesema tukio la kupigwa ngumi na askari ndani ya Ukumbi wa Bunge lilisababishwa na  amri ya Naibu Spika, Job Ndugai na wala siyo askari.
Aidha Sugu alisema ilikuwa vigumu kuvumilia konde alilopigwa na askari wakati akitolewa nje kwenye vurugu zilizotokea bungeni hivi karibuni, ndiyo maana aliamua kulipiza kisasi kwa kutaka kumpiga ngumi na si kichwa kama anavyodai  askari.
‘Sugu’ alitoa kauli hiyo  wakati akiwahutubia wakazi wa Chunya Mjini kwenye mkutano wa hadhara ulioongozwa na Katibu Mkuu wa Chadema Taifa, Dk Willibrod Slaa ambapo viongozi hao wapo ziarani  mkoani Mbeya  wakifanya  mikutano na wananchi kwa lengo la kuwaeleza ukweli wa kilichomtokea Sugu na  wabunge wengine bungeni hivi karibuni.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU SEPTEMBA 16, 2013

DSC 0389 3dbb0
DSC 0390 e0ea2

MBOWE, LIPUMBA NA MBATIA WAMBANA JK

mbowe 23301
Mshikamano wa vyama vya upinzani katika kupinga Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa 2013 umehamia nje ya Bunge na sasa vyama hivyo vimetangaza kuanza kampeni ya kuuhamasisha umma kudai maridhiano kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba Mpya.
Jana wenyeviti wa vyama hivyo; James Mbatia (NCCR-Mageuzi), Freeman Mbowe (Chadema) na Profesa Ibrahim Lipumba (CUF) walikutana na waandishi wa habari na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kutosaini muswada huo kuwa sheria, hadi pale kutakapokuwa na maridhiano ya pande zote husika.
Walisema muungano wao ni mwanzo wa kuunganisha umma wa Watanzania kufanya uamuzi wa kunusuru walichokiita "utekaji madaraka na mamlaka ya nchi kutoka kwa wananchi" hivyo wanaitaka Serikali kurekebisha kasoro zinazojitokeza katika mchakato huo.
Akitoa tamko la pamoja kwa niaba ya viongozi wenzake, Profesa Lipumba alisema wanachopigania ni kuurejesha mchakato wa Katiba Mpya mikononi mwa umma, kwa maelezo kwamba suala hilo kwa sasa limehodhiwa na CCM.
"Rais Kikwete asisaini muswada huu, aurejeshe bungeni ufanyiwe marekebisho yenye kujenga kuaminiana na mwafaka wa kitaifa kwenye mchakato wa mabadiliko ya Katiba. Hatutakwenda kumwona ila aurejeshe bungeni,"alisema Lipumba na kuongeza:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...