Tuesday, July 21, 2015

UCHAGUZI UMEEANZA NCHINI BURUNDI


Uchaguzi wa urais umeanza Burundi

Baada ya ghasia na maandamano ya miezi kadhaa, hatimaye raia nchini Burundi sasa wamefika katika vituo vya kupiga kura ili kumchagua rais wao. Watu wawili wameuwawa usiku wa kuamkia leo katika mji mkuu Bujumbura.

Foleni zimeonekana katika vituo vya kupigia kura

KESI YA RAIS WA ZAMANI WA CHAD YAAHIRISHWA HADI SEPTEMBA

Rais wa zamani wa Chad arejeshwa kortini 

Kesi ya kihistoria dhidi ya Kiongozi wa zamani wa Chad Hissene Habre iliyokuwa imerejeshwa mahakamani leo nchini Senegal sasa imeahirishwa hadi mwezi Septemba.

Mahakama imetoa muda huo kwa wakili wapya wa kiongozi huyo wa zamani wa kimla kujiandaa kwa kesi inayomkabili ya makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu, ukatili na uhalifu wa kivita.

Bwana Habre ambaye amekataa kuitambua mahakama hiyo alikataa kuzungumza mahakamani huku akiwashauri wakili wake wasimwakilishe mahakamani.

KITIMTIM MICHUANO YA KLABU BINGWA ULAYA

Michuano ya Klabu Bingwa Ulaya inaendelea tena hii leo kwa timu zile zinacheza round ya kwanza ambapo Dila Gori ya Geogia itakuwa na kibarua kigumu itakapoumana vikali na Partizan Belgrade ya Serbia.

Huku FC Pyunik ya Armenia ikikutana uso kwa uso na Molde ya Norway.

Milsami ya Boldova itapimana nguvu na Ludo Bulgaria.

Mechi nyingine za Klabu Bingwa barani Ulaya hapa chini Dila Gori v Partizan Belgrade 13:30

FC Pyunik v Molde 15:00

Milsami Orhei v Ludo Razgd 16:00

HJK Helsinki v FK Ventspils 17:00

Maccabi Tel Aviv v Hibernians FC 18:30

Lincoln Red Imps v FC Midtjylland 19:00

Vardar v Apoel Nic 19:00

Zalgiris v Malmö FF 19:10

Crusaders FC v Skenderbeu Korce 19:45

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...