Wednesday, June 19, 2013

LUNDENGA AMTIMUA MREMBO JUKWAANI BAADA YA KUTINGA NA KIVAZI CHA NUSU UCHI...!!!


MWENYEKITI wa Kamati ya Mashindano ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga Jumamosi iliyopita alimtimua mshiriki wa shindano la Redd’s Miss Morogoro 2013, Saphina Chumba (20) jukwaani wakati shindano hilo lilipokuwa likiendelea.
Tukio hilo lilitokea Jumamosi iliyopita katika Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Nashera mjini hapa wakati mrembo huyo alipokuwa akiwania kuvaa taji la mkoa huo.

Kisa cha mrembo huyo aliyevalia namba 5 kutimuliwa ni kukiuka maadili na kanuni za mashindano hayo kwa kuvaa nusu utupu mbele ya mgeni rasmi ambaye alikuwa Mbunge wa Kilosa, Mustapha Mkulo na mbele ya Kamati nzima ya Miss Tanzania.
Baada ya kuona jinsi alivyovaa, Lundenga na kamati yake walikubaliana kumtimua mshiriki huyo kwa kumwita Jaji Mkuu wa shindano, Alex Niktasi na kumtaka amuondoe haraka.
Mbali na Chumba, pia jaji alimtimu mrembo mwingine aliyevalia namba 8, Neema Joel (20) kutokana na kushiriki shindano  hilo mara mbili mwaka huu, inadaiwa mara ya kwanza alishiriki mkoani Arusha.
Lundenga alipohojiwa na waandishi wa habari alisema kamati yake inataka kuendeleza nidhamu tangu ngazi ya chini, hivyo hawawezi kuruhusu utovu wa nidhamu.

CCM YAOMBWA IRUHUSU WATU KUJITANGAZA URAIS.

VUGUVUGU la Uchaguzi Mkuu wa 2015 linazidi kupamba moto ambapo juzi aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye, ameomba CCM itoe ruhusa mapema kwa wanaowania urais kuanza kutangaza nia lakini bila kukampeni.

Sumaye ambaye alipata kugombea urais mwaka 2005, alionya kuwa kama CCM haitaruhusu wagombea kutangaza nia leo, yanayofanyika chini chini ni mabaya zaidi.

Akizungumza katika kipindi cha dakika 45 juzi, Sumaye mbali na kuitaka CCM kuruhusu wanachama wake kuan

za kutangaza nia ya kugombea mapema, pia alielezea athari za muundo wa Serikali tatu uliopendekezwa na Rasimu ya Katiba mpya na mfumo mpya wa kusoma Bajeti ya Serikali bungeni.


Urais 2015

MDADA ACHEZEA KICHAPO KWA KUFANYA UKAHABA JIRANI NA MSIKITI...!!!

 Richard Bukos na Issa Mnally

KHAAA! Operesheni Fichua Maovu ‘OFM’ iliyo chini ya Global Publishes, ipo mzigoni na hivi karibuni imenasa tukio la aina yake ambapo mke wa mtu amechezea kichapo ‘hevi’ akidaiwa kufanya ukahaba jirani na msikiti, Risasi Mchanganyiko lina kisa kamili.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu majira ya usiku jirani na msikiti huo uliopo nyuma ya Corner Bar, Kijitonyama jijini Dar ambapo mwanamke huyo na wenzake walikamatwa na baadhi ya vijana waumini wa Kiislamu waliokerwa na kitendo cha wao kutoa huduma haramu ya ngono maeneo hayo.


WENZAKE WATOKA NDUKI
Baada ya wenzake kufanikiwa kutoka nduki mithili ya mwanariadha Usai Bolt wa Jamaika, mwanamke huyo alishuhudiwa akila bakora kisha akapelekwa katika Kituo cha Polisi Kijitonyama, Dar akaunganishwa na wengine waliokamatwa usiku huo.
Ilielezwa kuwa wanawake hao wamekuwa wakiuza miili kwa wanaume karibu na msikiti huo na pembezoni mwa baa hiyo.
Ilisemekana kuwa kumekuwa na kawaida ya wanawake hao kusimama maeneo ya nyumba hiyo ya ibada na kufanya biashara hiyo huku wakichafua mazingira kwa kutupa ovyo kondomu na kujisaidia maeneo hayo. 


NGUO YA NDANI YAMVUKA
Wakati mwanamke huyo akicharazwa bakora, nguo ya ndani ilimvuka huku akipiga kelele kuwa hatarudia kufanya hivyo na kama akirudia basi akatwe kichwa.

BAADA YA KUZUSHIWA KIFO, HIKI NDICHO ALICHOSEMA MSANII SAIDA KAROLI

 
Baada ya taarifa kuzushwa kuwa Mwanamuziki wa asili, Saida Karoli amefariki katika ajali ya meli habari za uhakika ni kuwa Saida Karoli wala hayuko mahala popote jirani na Ziwa Victoria. 
Baada ya kuweko Dar es Salaam wiki iliyopita, Saida na kundi lake walikodishwa na kuelekea Makongorosi Chunya mahala aliko mpaka asubuhi hii.
Saida Karoli anasema "sina mpango wowote wa kufa hivi karibuni".
MUNGU AMUONGEZEE SIKU NYINGI ZENYE FARAJA KATIKA MAISHA YAKE

MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 19, 2013

.
.

HOFU YATANDA MKOANI SHINYANGA JUU YA MAUAJI YA WATOTO

( Picha na maktaba )

Na Steve Kanyeph
Wakazi wa manispaa ya Shinyanga wamegubikwa na hali ya hofu na wasiwasi kufuatia matukio ya mara kwa mara ya kuuawa kwa watoto wa kike wanaofanyiwa ukatili na unyanyasaji na kisha kuuawa ama kutelekezwa wakiwa hawajitambui.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakazi hao walisema vitendo vya unyanyasaji kwa watoto wa kike wenye umri wa kuanzia miaka tisa hadi kumi na nne katika manispaa ya Shinyanga kwa zaidi za miezi minne sasa vimekithiri hali ambayo inatishia amani kwa wakazi hao.

Akizungumza na Jambo Tz jana mkazi wa eneo la Ngokolo katika Manispaa ya Shinyanga bi Dafrossa Pius ambaye ni mjasiliamali, siku moja baada za tukio la kuuawa kikatili kwa binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kumi na mbili hadi kumi na tatu, kisha mwili wake kufungwa kama mzigo kwenye boksi na kutupwa kwenye ghuba la takataka katika eneo hilo la ngokolo mitumbani,alisema ni ukatili usiovumilika hata kidogo “ukatili kama huu kwa watoto wa kike wasio na hatia haupaswi kuvumiliwa wala kufumbiwa macho``

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...