Monday, November 24, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MDAHALO WA JAJI WARIOBA KESHO DAR

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.PICHA|MAKTABA 
Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imeandaa mdahalo maalumu wa Katiba utakaofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City ambao mzungumzaji mkuu atakuwa Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Joseph Butiku alisema jana kwamba mdahalo huo wa amani ni kwa ajili ya Watanzania wenye mapenzi mema na utakuwa wa wazi, ikiwa ni sehemu ya kuziba pengo la mdahalo wa Katiba uliovunjika Novemba 2 ambao ulifanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl.
Ulivunjika baada ya kutokea vurugu zinazodaiwa kuanzishwa na kikundi cha watu kwa lengo la kuvuruga uwasilishwaji wa ujumbe wa Katiba, huku Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda akitajwa kinara wa vurugu hizo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BUNDUKI BANDI YAMLETEA MAAFA

Kijana Tamir Rice alipigwa risasi mbili baada ya kupatikana na kilichobainika kuwa bunduki bandi. 
 
Wakili anayewakilisha familia ya kijana mweusi mwenye umri wa miaka kumi na mbili aliyepigwa risasi na polisi katika mji wa Cleveland nchini Marekani, amesema familia yake itafanya uchunguzi wake sambamba na ule unaofanywa na Polisi kubaini kilichotokea.
Kijana huyo kwa jina Tamir Rice mwenye umri wa miaka 12 alikuwa amebeba kile kilichoonekana kuwa bunduki bandia. Polisi wanadai kuwa kijana huyo alikataa kutii amri alipoambaiwa asalimu amri.
Kifaa walichokuwa nacho polisi ndicho kilibaini kuwa bunduki hiyo ilikuwa bandia.
Inaarifiwa kijana huyo alipigwa risasi mara mbili baada ya kuitoa bunduki yake kiunoni mwake lakini hakujaribu hata wakati mmoja kuielekeza kwa poliso wala kujribu kuifyatua.
Wakili wa familia hiyo amesema kuwa ikiwa watapata kuwa haki za kijana huyo zilikiukwa, familia yake itachukua hatua za kisheria dhidi ya polisi.
Mwanasiasa mmoja anapendekeza sheria ambayo itahakikisha kuwa bunduki bandia zinakuwa na rangi unayong'aa zaidi ili ziweze kutambulika haraka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MFANYAKAZI KATILI MATATANI UGANDA

Mfanyakazi wa nyumbani Tumuhirwe akimchapa mtoto wa mwajiri wake 

Polisi wamebadilisha mashtaka ya mfanyikazi wa nyumbani aliyenaswa kwa kamera akimpiga na kumtendea unyama mtoto wa mwaka mmoja na nusu, kutoka kwa kosa la kutesa na sasa anakabiliwa na kosa la jaribio la mauaji.
Video hiyo iliwaudhi watu wengi sana kwenye mitandao ya kijamii ila babake mtoto huyo alisema walisambaza video hiyo ili kuwatahadharisha wazazi wenegine.
Mfanyakazi huyo wa nyumbani Jolly Tumuhirwe, alikuwa amezuiliwa katika gereza la Luzira na mahakama ya Nakawa kwa kosa la kutesa chini ya kifungo cha 41 kwenye katiba kinachoongelea dhidi ya mateso.
Mwanamke huyo sasa anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 8 Disemba.
Hata hivyo, msemaji wa polisi Bwana Fred Enanga, amesema "shtaka dhidi ya mwanamke huyo lilibadilishwa baada ya kupitiwa mwendesha mkuu wa mashitaka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ROGDERS AKUBALI LAWAMA KIPIGO CHA LIVERPOOL


Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers 
 
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amesema anapokea lawama zote kufuatia kipigo cha timu yake ya Liverpool ilichokipata kutoka kwa Cyristal Palace.
Liverpool ambayo msimu uliopita ilishika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi ya England jana ilipata kipigo cha mbwa mwizi cha mabao 3 -1 kutoka kwa Crystal Palace.
Rodger amesema amekubali kwamba ulikuwa ni wakati mgumu na analazimika kufanya juhudi kubwa ili kutafuta ufumbuzi wa tatizo ndani ya Liverpool.
Amesema wamesikitishwa na kiwango cha timu pamoja na matokeo mabovu na kwamba kama meneja wa ni lazima achukue lawama. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SHABIKI WA MPIRA AMNG'ATA MWENZIE KENYA

Wayne Rooney 
 
Mwanamume mmoja mjini Kisumu Magharibi mwa Kenya, alimng'ata sikio jirani yake baada ya mechi ya soka ya ligi ya uingereza iliyokuwa na matokeo yasiyo ya kuridhisha kwa mmoja wao.
Mwanamume huyo ambaye ni shabiki sugu wa klabu ya soka ya Arsenal aliamua kujiondolea hasira ya klabu yake kushindwa na Manchester United kwa kumng'ata hasimu wake wa Man U sikio lake Jumamosi usiku.
Walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwa shabiki huyo sugu wa Arsenal hangeweza kustahimili kukejeliwa na jirani yake shabiki wa Man United baada ya klabu yake kushindwa mabao mawili kwa moja
Mwanamume huyo alifungiwa katika chumba kimoja na wakazi wa mtaa wa Railways mjini humo, ambao walitaka kumuua kwa kitendo chake. Inadaiwa hii ni mara ya pili kwa mwanamume huyo kumng'ata mwenziwe sikio kwa sababu za kisoka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...