Monday, November 24, 2014

BUNDUKI BANDI YAMLETEA MAAFA

Kijana Tamir Rice alipigwa risasi mbili baada ya kupatikana na kilichobainika kuwa bunduki bandi. 
 
Wakili anayewakilisha familia ya kijana mweusi mwenye umri wa miaka kumi na mbili aliyepigwa risasi na polisi katika mji wa Cleveland nchini Marekani, amesema familia yake itafanya uchunguzi wake sambamba na ule unaofanywa na Polisi kubaini kilichotokea.
Kijana huyo kwa jina Tamir Rice mwenye umri wa miaka 12 alikuwa amebeba kile kilichoonekana kuwa bunduki bandia. Polisi wanadai kuwa kijana huyo alikataa kutii amri alipoambaiwa asalimu amri.
Kifaa walichokuwa nacho polisi ndicho kilibaini kuwa bunduki hiyo ilikuwa bandia.
Inaarifiwa kijana huyo alipigwa risasi mara mbili baada ya kuitoa bunduki yake kiunoni mwake lakini hakujaribu hata wakati mmoja kuielekeza kwa poliso wala kujribu kuifyatua.
Wakili wa familia hiyo amesema kuwa ikiwa watapata kuwa haki za kijana huyo zilikiukwa, familia yake itachukua hatua za kisheria dhidi ya polisi.
Mwanasiasa mmoja anapendekeza sheria ambayo itahakikisha kuwa bunduki bandia zinakuwa na rangi unayong'aa zaidi ili ziweze kutambulika haraka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...