Monday, November 24, 2014

SHABIKI WA MPIRA AMNG'ATA MWENZIE KENYA

Wayne Rooney 
 
Mwanamume mmoja mjini Kisumu Magharibi mwa Kenya, alimng'ata sikio jirani yake baada ya mechi ya soka ya ligi ya uingereza iliyokuwa na matokeo yasiyo ya kuridhisha kwa mmoja wao.
Mwanamume huyo ambaye ni shabiki sugu wa klabu ya soka ya Arsenal aliamua kujiondolea hasira ya klabu yake kushindwa na Manchester United kwa kumng'ata hasimu wake wa Man U sikio lake Jumamosi usiku.
Walioshuhudia tukio hilo wanasema kuwa shabiki huyo sugu wa Arsenal hangeweza kustahimili kukejeliwa na jirani yake shabiki wa Man United baada ya klabu yake kushindwa mabao mawili kwa moja
Mwanamume huyo alifungiwa katika chumba kimoja na wakazi wa mtaa wa Railways mjini humo, ambao walitaka kumuua kwa kitendo chake. Inadaiwa hii ni mara ya pili kwa mwanamume huyo kumng'ata mwenziwe sikio kwa sababu za kisoka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...