Tuesday, August 27, 2013

HII NDILO JENEZA LENYE KIYOYOZI NDANI, WACHA LILE LA MSUYA LINALOFUNGULIWA KWA RIMOTI

Hili ni sanduku ya aliyekua Mfalme wa Roma(self-appointed Roma king),Florin Cioaba aliyefariki wiki moja iliyopita kwa mshtuko wa moyo huko Uturuki. Sanduku lake lilikua na Kiyoyozi kama lionekanavyo pichani.
Hivi karibuni watanzania tulishangazwa pale tulipoona sanduku la Billionea wa Arusha ambalo lilikua likifunguliwa kwa 'Remote Control'. Nadhani sanduku hili pia litawashangaza wengi.


MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 27, 2013

DSC 0048 a976f
DSC 0049 e302d
DSC 0050 81f49
DSC 0051 86967

EAC KUJITOSA MZOZO WA TANZANIA, RWANDA

sezi_cbe2f.jpg
Wakati Tanzania ikisema kuwa iko tayari kukaa meza moja na jirani yake Rwanda kumaliza hali ya uhasama iliyoanza kujitokeza katika siku za hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, Dk Richard Sezibera amesema jitihada za kidipolomasia zinafanyika kutatua tofauti hizo za kimawazo.

Bila kutaja taasisi wala wanaohusika katika jitihada hizo za kidiplomasia, Dk Sezibera aliwaambia waandishi wa habari jijini Arusha jana kuwa jitihada hizo zinafanyika kimya kimya bila kushirikisha vyombo vya habari "Migongano na tofauti za kimtazamo miongoni mwa viongozi wakuu wa nchi wanachama wa EAC ni jambo lisilo la afya kwa Jumuiya na linastahili kushughulikiwa kidiplomasia," alisema Dk Sezibera.


Akizungumza kwa tahadhari kubwa kukwepa kuingia kwa undani kuhusu suala hilo, Katibu Mkuu huyo alisema inafaa kila linalowezekana lifanyike kutatua mgongano wowote unaotokea kati ya viongozi wakuu.
Mjini Dar es Salaam, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe naye alisema katika mahojiano kuwa iwapo Rwanda itaomba kukutana na Tanzania kwa ajili ya kumaliza mzozo huo Serikali itakuwa tayari kutoa ushirikiano.

TAARIFA KAMILI KUHUSU BOMU KATIKA KANISA LA KKKT DAR ES SALAAM


POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, imebaini kuwa chombo kilichodhaniwa kuwa bomu katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kijitonyama hakikuwa bomu, bali ni kifaa cha Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) cha kuchunguza anga.
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleman Kova alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, baada ya kufanya uchunguzi kwa kushirikiana TMA.
"Baada ya kupata taarifa, polisi walifika eneo la tukio na kukuta kifaa kilicho katika umbo la kasha kikining'inia kwenye transfoma karibu na Kanisa kikiwa kinawaka taa.

“Katika kasha hilo kulikuwa na maandishi ya kalamu ya wino yaliyosomeka TMA na Airport," alisema Kamanda Kova.
Alisema baada ya uchunguzi wa awali, polisi walibaini kuwa kifaa hicho si bomu na kuondoka nacho kwa uchunguzi zaidi. Mtabiri Mwandimizi wa hali ya hewa kutoka TMA, Augustino Kanemba, alisema kifaa hicho kinaitwa Radio Sound na hutumiwa na Mamlaka hiyo kufanya utafiti wa hali ya anga za juu.

DADA YAKE FREEMAN MBOWE AIKIMBIA CHADEMA NA KUJIUNGA CCM, ADAI CHADEMA HAINA JIPYA



DADA wa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Grace Mbowe, amejiunga na Chama Cha Mapinduzi ( CCM) akitokea Chadema, kwa kile alichodai haoni jambo jipya katika chama hicho.

Grace amesema amehama kutokana na kuwepo propaganda zisizotekelezeka. Hata hivyo, amesisitiza kwamba kuwepo kwake katika Chadema, siyo kwa sababu ya familia.

Alikabidhi kadi hiyo jana kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Hai. Alisema itikadi za kisiasa, zisihusishe masuala ya kifamilia, kwani upendo wao uko pale pale.

Alisema kilichomfanya kujiunga na chama hicho ni utashi wake. Alidai CHADEMA wanafanya propaganda za 



kuwadanganya wananchi.

Alisema itikadi za chama, haziwezi kuingilia masuala ya kifamilia, hivyo kwake siyo ajabu kuondoka CHADEMA, kwani kila mtu ana utashi wake wa kisiasa.

MAN U, CHELSEA HAKUNA MBABE



Beiki wa Chelsea, Ashley Cole (kushoto) akikwaana na Wyne Rooney wa Manchester United.
Mshambuliaji wa Manchester United, Wyne Rooney (kushoto)  akijaribu kupiga shuti langoni mwa Chelsea.
Mourihno na Moyes wakisalimiana kabla ya mechi hiyo.

MANCHESTER UNITED VS CHELSEA 0-0 FULL HIGHLIGHTS

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...