Sunday, January 29, 2017

TAZAMA PICHA ZA ZOEZI LA UOKOAJI KWA WALIOFUKIWA NA KIFUSI GEITA.

Wachimbaji wote 15 waliofukiwa na kifusi katika mgodi wa RZ Geita wameokolewa asubuhi ya leo. Jambo Tz inawapa pole na kuwaombea wapone haraka ndugu wote waliokumbwa na ajali hii.

MBUNGE APENDEKEZA BIMA KWA WANYWAJI WA POMBE

Mbunge mmoja nchini Kenya amewasilisha mswada bungeni kuzishinikiza kampuni zinazouza pombe kutoa asilimia ndogo ya faida yao kuwadhamini wanywaji ambao wataathirika na pombe hiyo.

Mbunge Gideon Mwiti anataka watengenezaji wa pombe kutoa kati ya asilimia 5 na 10 ya mapato wanayopata kwa kampuni za bima ili kuwafidia watu ambao wataathirika na pombe ama hata kupata ajali kwa kuwa walevi kulingana na gazeti la Daily Nation nchini humo.

Mswada huo pia unapendekeza kwamba iwapo mtu atafariki kutokana na athari za kunywa pombe ,kampuni hizo za pombe zilazimike kufidia familia yake.

Bw Mwiti pia amezishutumu kampuni za pombe kwa kushindwa kukuza pombe zisizo na madhara kwa afya, kwa mujibu wa ripoti hiyo.

Thursday, January 26, 2017

WACHIMBAJI 14 WAFUNIKWA NA KIFUSI GEITA

Picha na maktaba.

Wachimbaji wadogo 14 kutoka mgodi wa dhahabu wa RZ uliopo Kata ya Nyarugusu mkoani Geita wamefukiwa na kifusi cha udongo baada ya kutokea maporomoko kwenye moja ya shimo walilokuwa wanachimba

Watu hao ni raia 13 Watanzania na raia mmoja wa China. Tukio hilo limetokea saa 9 usiku leo wakati wachimbaji hao wakiendelea na shughuli ya uchimbaji katika mgodi wa RZ unaomilikiwa na wachina.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Ezekiel Kyunga ametembelea eneo la tukio na kuona shughuli za uokozi zikiendelea na kuagiza nguvu ziongezwe

Tayari kampuni za madini ya dhahabu GGM, Kahama na Busolwa wameombwa kuongeza nguvu.

Wednesday, January 25, 2017

ECOWAS WABAINI KEMIKALI YA SUMU IKULU YA GAMBIA

Rais mstaafu wa Gambia Yahya Jammeh

Askari wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (Ecowas) wamegundua kemikali ya sumu kali iliyokuwa imetegwa kwenye vyumba vya Ikulu.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Ecowas kupitia gazeti la Freedom la Gambia, kemikali hiyo ilitegwa kwa lengo la kuua mtu yeyote atakayeingia ndani ya Ikulu hiyo.

Kutokana na hali hiyo, kiongozi mpya wa Gambia, Adama Barrow anatakiwa kuendelea kukaa Senegal kwa usalama wake huku uchunguzi ukiendelea kufanyika.

CUF WAMGEUKIA JENERALI MWAMNYANGE

Kikao cha kutathmini uchaguzi mdogo wa Jimbo la Dimani  cha  Chama cha  Wananchi (CUF), kimekusudia kumwandikia barua ya malalamiko Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania (JWTZ), Jenerali Davis Mwamunyange wakidai wanajeshi walishiriki kuleta hofu.

Hata hivyo, jeshi hilo limekana madai ya CUF likisema ni uzushi.

Madai hayo yalitolewa na Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alipozungumza kwa simu na mwandishi wetu kuhusu uamuzi wa kikao hicho kilichofanyika jana Unguja chini ya uenyekiti wa Katibu Mkuu, Maalim Seif Sharif Hamad na kuhudhuriwa na wajumbe 14.

Alidai kikao hicho kilichojadili mwenendo mzima wa uchaguzi kuanzia kampeni, kilifikia uamuzi wa kuandika barua ya malalamiko kwa Jenerali Mwamunyange wakidai wanajeshi walionekana wakizunguka mitaani katika jimbo, siku ya kuamkia uchaguzi na siku ya kupigakura.

FUMANIZI FEKI ZATIKISA MOSHI NA ARUSHA

(picha na maktaba) 

Utapeli wa aina yake unazidi kutikisa mikoa ya Kilimanjaro na Arusha baada ya kuibuka matukio ya kupangwa ya kufumania watu wenye heshima katika jamii kwa lengo la kujipatia fedha.

Siku za karibuni kumekuwa na mlolongo wa matukio hayo, yakiwalenga viongozi wa kiroho, wanandoa na vigogo wenye nyadhifa serikalini.

Uchunguzi ulibaini utekelezaji wa matukio hayo huambatana na vitisho kwa walengwa, ikiwamo kuwapiga picha na baadaye kutakiwa kutoa fedha kati ya Sh milioni 5 na Sh milioni 15 ili tukio hilo lisichapishwe kwenye vyombo vya habari.

Wake au waume za watu, viongozi wa dini na watendaji serikalini ndiyo walengwa wakuu wa matukio hayo, kwa kuwa ndiyo wenye hofu ya kuvunjiwa heshima kwenye jamii.

Chanzo: Mwananchi.

IVORY COAST YATUPWA NJE YA AFCON

Wachezaji wa Morocco wakishangilia.

Bingwa mtetezi wa michuano ya kombe la mataifa ya afrika tembo wa Africa Ivory Coast, wametupwa nje ya michuano ya mwaka huu baada ya kuchapwa kwa bao 1-0 na Simba wa Atlas Moroco

Goli pekee liliowaondoa miamba hao wa soka wa Afrika mashindanoni lilifungwa na Rachid Alioui katika dakika ya 64 ya mchezo.

Nayo timu ya Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo ilitambia Togo kwa kuichapa kwa mabao 3-1 na hivyo kufuzu hatua ya robo fainali wakiwa vinara kwa kundi C kwa alama 7 huku Moroco wakiwa nafasi ya pili kwa alama 6.

Moroco na Jamuhuri ya kidemocrasia ya Congo wanafuzu katika kundi hilo la huku Ivory Coast na Togo zikitupwa nje ya michuano hiyo.

Tuesday, January 24, 2017

MAALIM SEIF "NIMESHAMALIZANA NA JECHA"

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad 
  
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamada mesema ameshamalizana na mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha na haoni umuhimu wa kuzungumzia wala kumjibu, kwa sababu atampa sifa asizostahili.

Akihojiwa katika kipindi cha Funguka cha kituo cha televisheni cha Azam TV juzi, Jecha alisema hakumshirikisha Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein katika kufuta matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2015 visiwani humo.

Jecha alifuta matokeo hayo Oktoba 28, 2015, siku ambayo alitakiwa atangaze mshindi wa uchaguzi wa rais, huku ZEC ikiwa imeshatangaza matokeo ya majimbo 31 na mengine tisa yaliyosalia yakiwa yameshahakikiwa.

Alitangaza uchaguzi mpya Machi 20, 2016 ambao ulisusiwa na CUF na Dk Shein kuibuka mshindi.

DC AMSWEKA NDANI DIWANI WA CHADEMA

 
Mkuu wa Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu, Joseph Chilongani amemweka rumande Diwani wa Bukundi, Joseph Masibuka (CHADEMA ) kwa tuhuma za kubomoa nyumba 20 za wananchi kwa madai ya kujengwa katika eneo lake.

Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Simiyu, Jonathan Shanna alisema jana kuwa wanachunguza madai hayo kubaini kama kuna kosa ili hatua za kisheria zichukuliwe.

Shanna aliwapongeza wananchi kutojichukulia sheria mkononi wakati wa ubomoaji wa nyumba hizo wilayani hapa.

Kubomolewa kwa nyumba hizo na kampuni ya udalali, kumesababisha zaidi ya kaya 100 kukosa makazi.

Hata hivyo, Chilangoni aliwataka wananchi kurejea kwenye makazi yao na kwamba gharama za ujenzi zitafanywa na diwani huyo.

Baadhi ya wakazi hao walisema nyumba za nyasi na magodoro yalichomwa moto wakati wa ubomoaji.

Saturday, January 21, 2017

BABU WA LOLIONDO KURUDI UPYA NA KIKOMBE....!!!

Mchungaji Ambilikile Mwasapile

Mchungaji Ambilikile Mwasapile bado yupo na shughuli zake za kutoa kikombe cha dawa anayodai inatibu magonjwa  yote yanayomkabili binadamu.

Hata hivyo, baada ya ukimya wa muda mrefu babu ameibuka na kuitaka kwa mara nyingine Serikali kuboresha miundombinu ya Loliondo kwa kuwa kuna mambo makubwa yanakuja kutokana na maono anayoonyeshwa.

Akizungumza nyumbani kwake katika Kijiji cha Samunge, Tarafa ya Sale jana, Mchungaji Mwasapile alisema watu waliokuwa wanakwenda kwa wingi miaka iliyopita wamepungua sana na sababu ni kuwa idadi kubwa ya walipokea uponyaji wakati huo.

Mchungaji huyo mstaafu alisema wito anaoutoa kwa Serikali kuboresha miundombinu unatokana na mambo makubwa anayoonyeshwa yatakayokuja wakati ambao Mungu ameupanga.

YAHYA JAMMEH AKUBALI KUNG'ATUKA MADARAKANI

Kiongozi wa muda mrefu nchini Gambia Yahya Jammeh, anasema kuwa ataondoka madarakani baada ya kukataa kukubali kushindwa.

Katika tangazo kwenye runinga, Jammeh alisema kuwa hakuna haja ya hata tone moja la damu kumwagika.

Taangazo hilo linakuja saa kadha baada ya mazungumzo kati ya bwana Jammeh na wapatanishi wa Afrika Magharibi. Hata hivyo hakuna taarifa zaidi kuhusu yale yayoafikiwa.

Bwana Jammeh alishindwa kwenye uchaguzi wa mwezi Disemba na mrithi wake Adama Barrow tayari amesha apishwa.
Gambia: Jammeh 'akubali k

Bwana Barrow amekuwa akiishi katika taifa jirani la Senegal kwa siku kadha. Wanajeshi kutoka nchi za magharibi mwa Afrika ikiwemo Senegal wametumwa nchini Gambia wakitisha kumtimua bwana Jammeh madarakani.

Uamuzi wa bwana Jammeh kuondoka ulikuja kufuatia mazungumzo na marais wa Guinea na Mauritania.

Thursday, January 19, 2017

BAWACHA KUPINGA UTEUZI WA MAGUFULI MAHAKAMANI.

Mwenyekiti wa Bawacha Taifa, Halima Mdee

Baraza La Wanawake Chadema (BAWACHA) limetangaza kufungua Kesi ya Kikatiba katika Mahakama Kuu ya Tanzania kuomba tafsiri ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 66 (1) kuhusu rais kuteua wabunge na kuwazuia walioteuliwa hivi karibuni kuapishwa.

Mpaka sasa Rais John Magufuli amekwisha teua wabunge nane ambapo kati yao wanawake ni wawili ambao ni Dk. Tulia Akson na Profesa Joyce Ndalichako huku wengine wanaosalia wakiwa ni wanaume.

Idadi hiyo ya wabunge nane waliokwisha kuteuliwa na rais inajumuisha uteuzi wa Januari 16, mwaka huu ambapo Profesa Palamagamba Kabudi na Alhaji Abdallah Bulembo waliteuliwa.

Akizungumza leo katika ofisi za Chadema Kanda ya Ziwa Victoria, Mwenyekiti wa Bawacha Taifa, Halima Mdee alisema kwa muda mrefu sasa toka kuingia utawala wa serikali hii ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli, kumekuwa na ukiukaji wa katiba.

Alisema awali ilianza kupigwa marufuku mikutano ya vyama vya siasa ambavyo vipo kwa mujibu wa Katiba ikiwa ni kumteua mmoja waliokuwa maofisa wa Jeshi la wananchi wa Tanzania (JWT) kuwa mtendaji wa chama japo baadaye walilazimika kutangaza kastaafu jeshini.

“Katika katiba yetu ibara ya 66 (1)(e) rais anayo mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi kumi kutoka miongoni mwa watu wenye sifa zilizotajwa katika aya za (a) na (c) za Ibara ya 67 (1) na kati yao anapaswa kuteua angalau wanawake watano,” alisema.

ADAMA BARROW NDIE RAIS MPYA WA GAMBIA

Rais mpya wa Gambia Adama Barrow

Adama Barrow, mtu aliyeibuka mshindi katika uchaguzi wa urais nchini Gambia ameapishwa rasmi kuwa rais wa taifa hilo. Alikula kiapo hicho katika ubalozi wa Gambia nchini Senegal huku akiwaagiza wanajeshi wa Gambia kusalia katika kambi zao.

Ametambuliwa kimataifa.Lakini aliyekuwa rais wa taifa hilo Yahya Jammeh amekataa kujizulu na muda wake wa kuhudumu umeongezwa na bunge. Viongozi wa Afrika Magharibi wameshindwa kumsihi bw Jammeh kuondoka mamlakani. Wametishia kumuondoa kwa nguvu.
 Bw Jammeh alishindwa katika uchaguzi huo wa Disemba mosi ,kulingana na tume ya uchaguzi nchini humo. Lakini anataka matokeo ya uchaguzi huo kufutiliwa mbali akidai makosa mengi katika uchaguzi huo.

 ''Mimi Adama Barrow, naapa kwamba nitatekeleza wajibu wangu katika afisi ya urais wa taifa la Gambia kwamba nitahifadhi na kutetea katiba''.

 Na katika hotuba yake ya kuapishwa, aliwaagiza wanachama wote wa jeshi la gambia kusalia katika kambi zao. ''Wale watakaopatikana wakibeba silaha watachukuliwa kuwa waasi'', alionya.

Wednesday, January 18, 2017

WAZIRI MKUU WA ZAMANI APIGWA KOFI HADHARANI

Waziri mkuu mstaafu wa Ufaransa Manuel Valls amekashifiwa alipokuwa akihamasisha katika kampeni za chama cha kisoshalisti katika uchaguzi mkuu wa kiti cha Urais nchini Ufaransa.

Alipokuwa akihutubia katika ukanda wa Magharibi mwa mji wa Brittany alipigwa kofi na kijana mdogo alipokuwa akisalimia kwa kushikana mikono.

Mlinzi binafsi wa Bwana Valls alimkamata kijana huyo kooni kisha akamtupa chini.

Manuel Valls hajajeruhiwa katika tukio hili. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz, pia tufollow instagram @jambotz.

ALIYETABIRI KIFO CHA MUGABE AKAMATWA....!!!

Mchungaji Patrick Mugadza 

Maafisa wa polisi nchini Zimbabwe wamemkamata na kumzuilia mhubiri aliyetabiri kwamba Rais Robert Mugabe atafariki mwezi Oktoba mwaka huu.

Mchungaji Patrick Mugadza alikamatwa akiwa mahakamani mjini Harare Jumatatu ambapo alikuwa ameenda kwa kesi nyingine dhidi yake, wakili wake Gift Mtisi ameambia wanahabari.
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe.

Mchungaji huyo alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kuvalia bendera ya taifa. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz pia tufollow instagram @jambotz.

Saturday, January 07, 2017

KLABU YA MBOWE YAZAMISHWA RASMI

nhc 
SHIRIKA la Nyumba la Taifa (NHC) limeanza kubomoa jengo la iliyokuwa Klabu Bilicanas na ofisi za Free Media inayomiliki gazeti la Tanzania Daima zinazomilikiwa na Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Taifa, Freeman Mbowe, lililopo makutano ya barabara ya Mkwepu na Indira Gandhi lenye kitalu namba 725-726/24 na hati namba C. T No. 186018/15 and C. T No. 186018/10. 

Ubomoaji huo ulioanza jana unafanyika wakati Mbowe ameingia katika mgogoro na NHC baada ya kampuni ya udalali ya Poster and General Traders kumtolea vyombo nje mwanzoni mwa Septemba, mwaka jana kwa kudaiwa Sh bilioni 1.2 ambayo ni deni la pango ya miaka 20.

Gazeti hili lilishuhudia ubomoaji huo ukiwa katika hatua za awali na baadhi ya vijana walionekana wakianza kuondoa vioo na vigae vilivyoezekwa katika jengo hilo wakiwa chini ya usimamizi wa walinzi.

Hata hivyo, walipoulizwa watu waliokuwa wakisimamia katika eneo hilo walidai kuwa ubomoaji huo ni wa kawaida na ulipangwa kufanyika muda mrefu na endapo waandishi watahitaji maelezo wawasiliane na uogozi wa NHC.

NANA AKUFO ADDO AAPISHWA RASMI KUWA RAIS WA GHANA

Nana Akufo-Addo akila kiapo wakati akiapishwa 
 
Viongozi kadha wa Afrika leo wamekusanyika katika mji mkuu wa Ghana, Accra, kuhudhuria sherehe za kutawazwa rais mpya, Nana Akufo Addo.

Maelfu ya wageni walialikwa kwenye sherehe katika Medani ya Uhuru mjini Accra. Bwana Akufo Addo, aliyewahi kuwa wakili wa haki za kibinaadamu, alimshinda Rais John Dramani Mahama, katika uchaguzi wa mwezi uliopita.
Madaraka yanakabidhiwa kwa kiongozi mwengine kwa salama, jambo linaloonekana kuwa mfano mwema wa demokrasi Afrika ambako katika baadhi ya nchi, viongozi hawataki kun'gatuka.

Baada ya kuapishwa kwa rais, sasa viongozi waliohudhuria sherehe hiyo, watajadili namna ya kuhakikisha kuwa Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, anaondoka madarakani. Kiongozi huyo amekataa kustaafu ingawa alishindwa katika uchaguzi wa Mwezi Disemba.

Tuesday, January 03, 2017

MKULIMA MWINGINE AJERUHIWA KWA SIME KILOSA

524332cd04985aff0de9f1e645398d62

MTU mmoja mkazi wa Kijiji cha Mamoyo, Kata ya Mabwerebwere, Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, Omary Sululu (52), amenusurika kifo baada ya kukatwakatwa na sime kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni wafugaji.

Taarifa zilizopatikana kijijini hapo, zinasema Sululu alijeruhiwa na wafugaji hao wakati alipokuwa akizuia mifugo isile mazao katika shamba lake.

Tukio hilo limetokea siku chache baada ya Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafugaji Tanzania, Joshua Lugaso, kutoa tamko la  kulaani matukio ya kikatili yanayofanywa  na  wafugaji dhidi ya wakulima wilayani Kilosa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii akiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kilosa, Sululu alisema alijeruhiwa Januari mosi, saa za mchana wakati alipokuwa katika shamba lake la mahindi na migomba. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

ANGALIA PICHA ZA BABU MWENYE MIAKA 77 MWENYE NGUVU ZA AJABU AKIVUTA GARI KWA SHINGO....!!!

meet-the-77-years-old-strongest-man-in-akwa-ibom-photos-2
 
Babu wa miaka 77 kutoka mji wa Akwa Ibom, nchini Nigeria ambaye ana uwezo wa kuvuta gari kwa kutumia shingo yake.

Babu huyo amefahamika kwa jina la Sampson, ila yeye anataka afahamike kwa jina la African Superman, ana uwezo pia wa kuweka mkono wake juu na wanaume 10 wakabembea bila kuushusha mkono wake chini.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 03, 2017 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

04dafa6a-93c3-49cf-be2f-ccff44ac58ae

PLUIJM AKARIBIA KUPEWA MIKOBA YA UKOCHA AZAM FC

Mabingwa watetezi wa Kombe la Kagame, Azam FC wamebakiza hatua chache kukamilisha mpango wa kumkabidhi timu hiyo aliyekuwa kocha wa zamani wa Yanga, Hans Pluijm.

Habari za kuaminika kutoka vyanzo makini ndani ya Azam zilithibitisha kuwa tayari Azam imekuwa na mazungumzo ya kina na kocha huyo Mdachi ambaye kwa sasa ni mkurugenzi wa ufundi Yanga.
Awali, Azam ilipanga kumpa timu hiyo kocha wa Majimaji, Kally Ongala ambaye amewahi kuitumikia klabu hiyo kama kocha msadizi, lakini wakabadilisha mawazo kutokana na kocha huyo kuwa na uzoefu mdogo na michezo ya kimataifa.

Mwenyekiti wa Azam, Nassoro Idrissa ‘Father’ amesema Pluijm ni kocha wa kiwango cha juu na amethibitisha hilo nchini kwa kuipa Yanga mataji manne tofauti, hivyo watafurahi kama atafanya nao kazi. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Sunday, January 01, 2017

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...